President George Bush to visit Ethiopia, Tanzania and Zambia

Kaazi kweli kweli. Tujifunze kuwa watu wa kujitegemea. Hakuna dharau mbaya kama tulipodharau dhana nzima ya nchi yenye kujitegemea. Tumekuwa goigoi, wenye kusubiri huruma ya wahisani kwa karibu kila kitu. They will put middle finger on our ***!
 
wakuu!!
leo rais mstaafu wa marekani anawasili Tanzania. lakini cha kushangaza ziara hii imekuwa ni siri mno hakuna chombo cha habari hata kimoja kilicho tangaza hii ziara ya huyu muheshimiwa.
mimi ni mwanafunzi wa Muhimbili kwa sasa niko ocean road kwa clinical studies na inasemekana atakuja kutembelea leo hospitali ya ocean road.
kinacho nisikitisha ni kwamba hapa ocean road wagonjwa huwa wanalala nje kutokana na ukosefu wa vitanda na maanisha hata wodi hazitoshi. leo hakuna mgonjwa nje sasa sielewi wagonjwa wamepelekwa wapi. nachoona leo ni bendera za Tanzania tu na mauwa ndo yameshamiri huku ocean road.
je nini kilichomleta huyu rais mstaafu wa usa? au anekuja kuangalua maedeleo ya freemasons na ile miradi yake ya kigamboni?

naomba niwasilishe mwenye kujua zaidi kuhusu ziara ya siri ya huyu mueshimiwa atujuze.

Viongozi wa serikali ni WEZI, walikaribisha mwizi mwenzao BUSHI awekeze nchini ili waibe vizuri. Walimwandalia mazingira mazuri ya kuiba, na juzi tu wanatuhadaa watanzania, hasa nilipomsikiliza Bakari Mwapachu akidanganya kuwa migodi ya BUSHI-BARRIC imeiachia TZ mapesa kibao, halafu anasema zinabaki kupititia mishahara ya wafanyakazi nikasema huyu mtu tahira kwelikweli,

kwa nini asiseme makusanyo ya BARRICK yamejenga miundombinu ya maji, barabara, hospitali, kusomesha watoto shule na vyuo na kuboresha mishahara ya watumishi wa umma?

Inawezekana kabisa wanamkakati mwingine wa kutuchakachua, kwani bao tunachakachulika

 
Alshabab wako wapi waniondolee taka taka hiyo
mali ya mungu we kweli kiboko,alshabab wapo kenya na wamejua kama bush yupo tzania,sababu kuu ya kufichwa nakufanywa siri kwa ziara yake ni kuwaogopa alshabab,pia anatakiwa akamatwe apelekwe the hegue ktk mahakama yauhalifu wakivita,ameua mamilioni ya wairaki,waafghanstan,wapakistan,wapalestina nahata wasomali,na wacongomani,huyu ndie wakupelekwa the hegue,sio gbagbo wanamuonea tu.
 
Hivi kweli kabisa inaingia akili Rais Mstaaf anakuja Tanzania anashukia Serengeti kabla ya kumuona Mwenyeji wake!!!,

Ni kama mtu anakuja nyumbani kwako anapumzika kwenye garden yako alaf ndo anakuja kubisha hodi umkaribishe chakula.

Btw I wish to know how close H.E. Bush and H.E. Mkapa are....
 
Karibu sana Tanzania. Huyu jamaa alifanya kazi nzuri sana kwa masuhala ya usalama wa dunia. Kata funua wahuni,magaidi na wafadhili wao!

ww utakua umerogwa na aliyekuroga alishakufa c bure
 
Kama mambo yapo hivi ****** kwanini hatutaki kutoa! Wanaume wenzangu tuanze kutembea na sabuni ili maumivu yasiwe makari! Ndio tunasema tanzania amani ipo na viongozi wanajinadi vifua mbele!? Amakweli ukipenda dezo wanakudezo kwa raha zao! Harafu eti tunajiita vidume kifua mbele!

hatutaki kutoa nini?
tutembee na sabuni ya nini baba?
maumivu gani hayo?

Mbona mi sielewi wandugu?
 
Ukiwa kihiyo ukafikri kimasaburi unaweza kujikimambi hivi hivi , tusikubali wakileta ngebe tuwadito mapema kabla hawajatukolimba,
kuwekeza sio tatizo tatizo tunafaidikaje, lakini kwa kuwa marekani imeonyesha nia ya kutusaidia tungoje tuone.
 
............Huyu ana ukurugenzi kwenye kampuni Ya BARICK

Kuna tetesi kuwa amewekeza kwenye Uranium huko Namtumbo! Na itapigwa lami ya hatari huko maana kuna watu wanaishi Mtwara,na ili waende Songea,lazima waende Dar kwanza ndiyo wapite Mikumi,Kitonga,Makambako, Njombe,hadi Songea...!
 
naona mitambo inazengua hata hivyo wanasema mahojiano ni kuanzia saa 12 kamili jioni ya leo...oyaa naona mzungu anahesabu 1-13 kama sehemu na sound testing
 
Wadau, angalieni tbc kwa wenye access ya tv, kuna live broadcast ya mkurlu wa kaya na Bush wa united states ov america...hopful wataongelea uranium yetu inayochimbwa bila kibali cha watanzania..
 
kuna anayeweza kuniambia ni nini hiki ninachokiona na kukisijkia?
 
Wadau naona raisi wenu yupo na G bush katika mdahalo, naona kakazana kukremu chakuongea while mwenzie yupo so comfortabla kwenyekiti anafurahi...!
 
nipo najiuliza kuna sauti inasikika sijuhi inatoka USA via satellite?
 
Hakuna jipya zaidi ya Tanzania bila Ukimwi inawezekana, na blah blah blah nyingi za hapa na pale. Hakuna inshu, wafundishe watoto homework zao usipoteze muda wako kumsikiliza JK na Bush.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom