Yona F. Maro
R I P
- Nov 2, 2006
- 4,202
- 218
POWERED BY SASATEL WENGINE MKO WAPI
Wale ambao huwa wako maeneo ya mjini haswa jiji la dar es salaam lazima watakuwa wameona vibanda vya mawasiliano ya Internet ambavyo ni vya vodacom , eneo la mwenge kuliwahi kuwa na moja lakini kwa sasa limeshafungwa pale jijini dar es salaam kuna lingine liko Mtaa wa samora , Ukiingia ndani ya banda hilo kila siku mwendeshaji huwa na visingizio mara Mtandao uko down mara kuna virus vitu kama hivyo .
Wengine ambao tulitembelea maonyesho ya sabasaba mwaka huu tuliojionea wenyewe jinsi kampuni hizi zilivyoweka huduma za mtandao kwenye mabanda yao kwa ajili ya watu mbali mbali kuweza kuwasiliana na wenzao wanapokuwa ndani ya uwanja huo .
Nilibahatika kwenda kwenye banda la Tigo , Sasatel na Voda ila nilivutiwa zaidi na sasatel kwa sababu ndio ilikuwa iko sokoni kwa mara ya kwanza nilipenda kwenda kuona huduma zao Kulikuwa na huduma nzuri sema tatizo lilikuwa kwenye computer zao hazikuweza kukidhi mahitaji mengine ya watumiaji kama spidi , matatizo mengine kama virus kuna watu walikuwa wakiingia pale kutoka tu akienda nyumbani analia na virus , inaonyesha mtu aliyekuwa na wajibu wa kusimamia mambo yale pale hakuwa mwangalifu sana .
Pamoja na yote hayo kwenye siku za karibuni nimejaribu kuangalia kama huduma zile za vibanda kule ndani zinasambazwa sehemu nyingi na kwa uzuri zaidi , nimegundua kwamba Sasatel wanasambaza huduma zile kwa kasi zaidi kuliko kampuni nyingine yoyote kwa kipindi cha miezi michache toka Wakati Ule .
Nilivutiwa siku moja nilipopita sehemu nikakuta THIS INTERNET CAFÉ IS POWERED BY SASATEL , ikabidi niingie ndani kwenda kuona inakuwaje kwa zaidi ya masaa 5 hivi huduma zao zilikuwa nzuri , tatizo ni kama la hapo juu watu waliopewa kazi ya kusimamia internet café yenyewe ndio hawako vizuri katika mambo kadhaa .
Huduma hizi za SASATEL nimevutiwa nazo sana wangefanya mkakati wa kuzipeleka sasa huko vijijini na sehemu ambazo kupatikana kwa huduma za mawasiliano ni kazi , kampuni nyingine zimeshindwa ila kwa mwendo huu wa SASATEL unaoonyeshwa sasa hivi naamini huko watafikia .
Baada ya Wabunge kuendelea kupiga domo kuhusu huduma hizi ni wakati wao sasa kuongea na Kampuni kama hizi kwa ajili ya huduma za mtandao kwa wananchi wao haswa wale walio maeneo ya vijijini naamini wakiwa na mikataba maalumu kila mtu ataweza kufaidika na huduma hizi .
Hata wananchi ambao wamejiunga kwenye vikundi vya saccos wanaweza pia kuongea na kampuni kama hizi kwa ajili ya kuletewa huduma katika maeneo yao , itasaidia wanachama wa saccos kuwasiliana na makao yao pia saccos itaweza kutengeneza faida zaidi kwa kulipisha watu
Kama wananchi wanachanga pesa kwenye saccos kwanini wanashindwa kujipanga hivyo hivyo kupatiwa huduma za mawasiliano kama hizi huko vijijini mwao , Baada ya kuchangia Kwenye Vicoba .
Wale ambao huwa wako maeneo ya mjini haswa jiji la dar es salaam lazima watakuwa wameona vibanda vya mawasiliano ya Internet ambavyo ni vya vodacom , eneo la mwenge kuliwahi kuwa na moja lakini kwa sasa limeshafungwa pale jijini dar es salaam kuna lingine liko Mtaa wa samora , Ukiingia ndani ya banda hilo kila siku mwendeshaji huwa na visingizio mara Mtandao uko down mara kuna virus vitu kama hivyo .
Wengine ambao tulitembelea maonyesho ya sabasaba mwaka huu tuliojionea wenyewe jinsi kampuni hizi zilivyoweka huduma za mtandao kwenye mabanda yao kwa ajili ya watu mbali mbali kuweza kuwasiliana na wenzao wanapokuwa ndani ya uwanja huo .
Nilibahatika kwenda kwenye banda la Tigo , Sasatel na Voda ila nilivutiwa zaidi na sasatel kwa sababu ndio ilikuwa iko sokoni kwa mara ya kwanza nilipenda kwenda kuona huduma zao Kulikuwa na huduma nzuri sema tatizo lilikuwa kwenye computer zao hazikuweza kukidhi mahitaji mengine ya watumiaji kama spidi , matatizo mengine kama virus kuna watu walikuwa wakiingia pale kutoka tu akienda nyumbani analia na virus , inaonyesha mtu aliyekuwa na wajibu wa kusimamia mambo yale pale hakuwa mwangalifu sana .
Pamoja na yote hayo kwenye siku za karibuni nimejaribu kuangalia kama huduma zile za vibanda kule ndani zinasambazwa sehemu nyingi na kwa uzuri zaidi , nimegundua kwamba Sasatel wanasambaza huduma zile kwa kasi zaidi kuliko kampuni nyingine yoyote kwa kipindi cha miezi michache toka Wakati Ule .
Nilivutiwa siku moja nilipopita sehemu nikakuta THIS INTERNET CAFÉ IS POWERED BY SASATEL , ikabidi niingie ndani kwenda kuona inakuwaje kwa zaidi ya masaa 5 hivi huduma zao zilikuwa nzuri , tatizo ni kama la hapo juu watu waliopewa kazi ya kusimamia internet café yenyewe ndio hawako vizuri katika mambo kadhaa .
Huduma hizi za SASATEL nimevutiwa nazo sana wangefanya mkakati wa kuzipeleka sasa huko vijijini na sehemu ambazo kupatikana kwa huduma za mawasiliano ni kazi , kampuni nyingine zimeshindwa ila kwa mwendo huu wa SASATEL unaoonyeshwa sasa hivi naamini huko watafikia .
Baada ya Wabunge kuendelea kupiga domo kuhusu huduma hizi ni wakati wao sasa kuongea na Kampuni kama hizi kwa ajili ya huduma za mtandao kwa wananchi wao haswa wale walio maeneo ya vijijini naamini wakiwa na mikataba maalumu kila mtu ataweza kufaidika na huduma hizi .
Hata wananchi ambao wamejiunga kwenye vikundi vya saccos wanaweza pia kuongea na kampuni kama hizi kwa ajili ya kuletewa huduma katika maeneo yao , itasaidia wanachama wa saccos kuwasiliana na makao yao pia saccos itaweza kutengeneza faida zaidi kwa kulipisha watu
Kama wananchi wanachanga pesa kwenye saccos kwanini wanashindwa kujipanga hivyo hivyo kupatiwa huduma za mawasiliano kama hizi huko vijijini mwao , Baada ya kuchangia Kwenye Vicoba .