Mpasuajipu
JF-Expert Member
- Oct 22, 2010
- 836
- 49
Wanajamvi sijui km nimetua ukumbi husika, km sio mtanisahihisha.
Napenda kujua hawa ndg zetu waliwahi kuvuma sana enzi zao katika sanaa.
Power Mabula alikuwa na nguvu za ajabu kuuia au kuvuta magari km Scania n.k au hata gari kupita kifuani kwake bila kudhurika.
Mzee Moris Nyunyusa hadi leo ngoma zake zinapigwa kabla ya taarifa ya habari ya TBC, ile midundo aliipiga yeye. Mzee Moris aliwahi kuonyesha maajabu ya kupiga ngoma kumi kule Japan hadi Mbaraka Mwinshehe akamtungia wimbo ule wa "Maonyesho japani yalifana sana,.....
Mzee Mwinamila pia alikuwa msanii maarufu sana enzi hizo za TANU na wanasiasa wengi walimtumia katika kuburudisha jamiii.Mzee huyu alikuwa na uwezo wa kupiga samasoti kama kijana kabisa.
sasa nauliza kwa wale wanaojua hawa wazee TZ imewaenzi vipi au taha familia zao tu, au ndio mtu akitoweka ndio anasahaulika kabisa?
kwangu mie, naona hawa walikuwa ni ma-celebrities wa ukweli hapa bongo.
nawasilisha km nimekosea sehemu mnisahihishe sio kunishambulia.
wasaalaaam.
Napenda kujua hawa ndg zetu waliwahi kuvuma sana enzi zao katika sanaa.
Power Mabula alikuwa na nguvu za ajabu kuuia au kuvuta magari km Scania n.k au hata gari kupita kifuani kwake bila kudhurika.
Mzee Moris Nyunyusa hadi leo ngoma zake zinapigwa kabla ya taarifa ya habari ya TBC, ile midundo aliipiga yeye. Mzee Moris aliwahi kuonyesha maajabu ya kupiga ngoma kumi kule Japan hadi Mbaraka Mwinshehe akamtungia wimbo ule wa "Maonyesho japani yalifana sana,.....
Mzee Mwinamila pia alikuwa msanii maarufu sana enzi hizo za TANU na wanasiasa wengi walimtumia katika kuburudisha jamiii.Mzee huyu alikuwa na uwezo wa kupiga samasoti kama kijana kabisa.
sasa nauliza kwa wale wanaojua hawa wazee TZ imewaenzi vipi au taha familia zao tu, au ndio mtu akitoweka ndio anasahaulika kabisa?
kwangu mie, naona hawa walikuwa ni ma-celebrities wa ukweli hapa bongo.
nawasilisha km nimekosea sehemu mnisahihishe sio kunishambulia.
wasaalaaam.