Elections 2010 Post-Mortem: Kwa Nini Dr. Slaa Na CHADEMA Wameshindwa

JK kaiba kura nyingi lakini Dr Slaa ndiye mshindi.
- Kachukua miji yote muhimu chini
- Anakubalika na sehemu kubwa ya vijana wakiwemo wanavyuo na wanafunzi msingi, sekondari
 
To me naona mainly inaweza kutokana na hofu ya wananchi juu ya fujo ukizingatia watz ni waoga leading to low turn over na kuwaachia wanachama 5mill wa CCM kutamba na kupiga kura
On the other hand wizi wa kura ambao umefanywa na taasisi zetu
 
pamojha na yoote Mliyoyasema,
yupo adui mmoja wa CHADEMA ambaye alijiingiza mwishoni japo watu walimpuuza alitaka kupunguza kura zetu, huyu Ni Askofu sijui Mchungaji Gamanywa na Genge lake la watu wa Mungu kama wanavyojiita, kujidai kuikemea CHADEMA kutumia kampeni za Udini, huyu Mchungaji akiitumia Radio yake kwa vipindi vya jioni , nimewahi kusikia mara mbili, alikua waziwazi akitoa angalizo kwa watu juu ya hatari ya damu kumwagika kama kutakua na rapid changes katik aregime ya Taifa, kwakua Kikwete ni chaguo la Muungu wake.
kwakweli hawa watu ni maadui wakubwa wa WATANZANIA, wapenda mageuzi, na mabadiliko.
 
Nisingetofautiana sana na William lakini nina ya kuongezea:
1) Hofu ya nini CHADEMA inasimamia: Pamoja na kuwa na ilani nzuri yenye mvuto, CHADEMA walipata shida sana kuielezea na kuwaaminisha wapiga kura ingetelezeka. Sio kwa kuwa hawakuwa na maelezo bali kwa sababu CCM kwa kutumia mtandao wake waliibeza kwa hisia kali na kuichafua. Mifano ni mingi! Hii ilihusu hasa mapendekezo ya sera kuhusiana na ujenzi wa nyumba kwa bei nafuu, elimu bure na sera za majimbo. Hata wasomi pale UDSM walisikika wakikituhuma kwa nguvu kabisa CHADEMA wanatafuata cheap popularity, na ni chama cha wachagga! Ndio walisema Slaa ni Mchagga na mwanzoni sikuona hii kama issue kubwa lakini kuna hisia kwamba Mchagga akichukua uongozi wa taifa basi taifa litakuwa limeisha au vile, lakin kweli kuna hofu! Na hawa wasomi (niwaite uchwara) wanakazia hoja yao kwamba haitowezekana kamwe mtu wa kabila la kichagga au kihaya akawa Raisi. Angalizo hapa ni SIASA TAKA ZA UKABILA na hofu iliyopandikizwa na wale ambao ni wapinzani wa Chadema.

2) Sio bahati mbaya kwamba CUF na CCM ilipata kukubalika zaidi maeneo ya Pwani, miji katika reli ya kati na kule kusini kwa mchomba(lindi na Mtwara). SIASA TAKA ZA UDINI zilitawala. CHADEMA walishindwa kabisa kusafisha madongo yalitupwa kwake kwamba mgombea wake ni Mdini na alikuwa ametumwa na Dini yake kugombea.

Ili Chadema wafanikie kuna kila sababu ya kutafuta jinsi ya kufuta hizi hisia ndani ya wapiga kura, pengine ni kuelekeza operesheni kama Sangara maeneo haya zaidi. Hilo la ukabila linazidi kupotea kwa kadiri CHADEMA wanalyozidi kupata wabunge na viongozi kutoka sehemu mbalimbali nchini. Kazi ya kupigana na CCM yenye mizizi na fedha nyingi, uchoyo wa madaraka na isiyo na haya kudanganya haikuwa rahisi hata kidogo. Ukifikiri ingekuwa rahisi kwa mpiga kura kuamini ahadi za CHADEMA kuliko kumwamini Kikwete na ahadi za Viwanja vya ndege, bandari, kujenga mto wa maji, reli nk. Lakini mashine ya propoganda za CCM ni kubwa!

Mkuu hizo ndio political mathematics. CCM wanajua vizuri kutumia mbinu za kisiasa kupata ushindi, mbinu safi na chafu, ili mradi ushindi. Sio siri kwamba CCM wanatumia unyonge wa watanzania kujikusanyia kura. Ukiangalia walikopata kura nyingi ni kule kwenye watu waliochoka, au watu waliochoka zaidi ndio waliorubunika na kuwapigia kura. Ni mbinu ya kisiasa, inafaa CHADEMA nao waanze kutumia watu kama hao kwenye chaguzi zijazo ili kujipatia kura.
 
Back
Top Bottom