Posho za wabunge zapanda kimyakimya!

Aisee hii ndo bongo zaidi ya uijuavyo
Zitto endelea na msimamo wako ipo cku watanzania watakuelewa
 
Kama Zitto angekaa na wabunge wenzake wa CHADEMA na kujadiliana nao kabla ya ku-issue hii statement kingeharibika nini? And what it the point ya ku-mtaja (kumpongeza January Makamba) kwenye hili?
 
Jamani lets be fair! Hivi kwa hali ya maisha ya sasa hivi posho ya kujikimu ya shilingi 80000 inatosha kwa mbunge au mtumishi yeyote wa Serikali? Kw kiwango hicho cha fedha Mbunge atakaa mahali decent na aweze kufanya kazi yake mliyomtuma? Mimi siafiki suala la kupandisha fedha za vikao maana vikao ndiyo kazi ya Wabunge, bali ninaafiki kupandishwa kwa posho ya kujikimu (perdiem) kutoka kiwango cha sasa hadi walau shilingi laki 3 kwa siku kwa watumishi wote. Tufahamu kuwa ni kutoka katika posh hii ndiyo mbunge anakula, kulala, kulipia stationeries na mengineyo. Ni maoni yangu tu.
 
Kama Zitto angekaa na wabunge wenzake wa CHADEMA na kujadiliana nao kabla ya ku-issue hii statement kingeharibika nini? And what it the point ya ku-mtaja (kumpongeza January Makamba) kwenye hili?
Kama wabishi afanyaje? We shibuda atamuelewa kweli zitto?
 
Mkuu anapoint ya msingi sana, hizi posho sasa zimezidi jaman juzi Ngelaja na Malima wamekula 8m kwa dk40 tu na bado wanapewa posho za bunge ila mkuu nadhan anatakiwa apumzike kidogo mana juzi katoka kwe operation ya eneo nyeti linalohusisha tafakuri zake...
 
Ndiyo maana hutasikia mamlaka yoyote ikiwachukulia hatua akina Jairo, Ngeleja...., kwa mtazamo huo huo!
 
Wabunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano, wameongezewa posho ya vikao kutoka sh 70,000/- hadi 200,000/- kwa siku. Likiwa ni ongezeko la 154%.



Source: Mwananchi
 
Nilitegemea wabunge wa Magwanda wangepinga ongezeko hili la kutisha lakini kimya sioni tofauti kati ya magwanda na Magamba wote sawa.

Wabunge wa Magwanda walipopinga posho kwenye kikao kilichopita, mliwabeza na kuwazodoa kwamba wanatafuta umaarufu. Leo posho imezidi kuongezeka mnawasema vibaya eti kwa nini wasipinge. Sasa mnataka wafanye nini, wakati wananchi wenyewe mnaotetewa hamtoi support? "ACHENI UNAFIKI WATANZANIA". Ushauri wangu kwa Magwanda pokeeni posho zenu hata kama zingekuwa milioni moja kwa siku. "If you can't fight them, join them".

 
Naanza maandalizi ya kugombea ubunge. Hakuna kazi inayolipa kama hii,
 
Nimeshtushwa sana na taarifa za kupandishwa kwa posho za vikao kwa Wabunge. Nimeshtushwa zaidi kwamba Posho hizi zimeanza kulipwa katika mkutano wa Bunge uliopita kabla hata Rais hajaamua maana maslahi yote ya Wabunge huamuliwa na Rais Baada ya kupokea mapendekezo ya Bunge kupitia Tume ya Bunge.

Wabunge wote watambue kwamba kuamua kujipandishia posho zao bila kuzingatia Hali ya maisha ya mwananchi wa kawaida ni usaliti usio na mfano. Mbunge yeyote ambaye anabariki Jambo hili au anaishi hewani haoni tabunza wananchi au ni mwizi tu na anaona Ubunge ni Kama nafasi ya kujitajirisha binafsi.

Kwa Wabunge wa Chadema, wajue uamuzi kuhusu posho ni uamuzi wa chama na ni uamuzi wa kisera. Mbunge yeyote wa Chadema anayepokea posho za vikao anakwenda kinyume na maamuzi ya sera za chama tulizoahidi wananchi wakati wa uchaguzi. Nimemwomba Katibu Mkuu wa chama kuitisha kikao maalumu cha Kamati Kuu ya chama kujadili suala hili.

Toka tarehe 8 juni mwaka 2011 nilikataa kupokea posho za vikao. Popote ninapohudhuria vikao huomba Risiti ya fedha ninazokataa. Baadhi ya Wabunge Kama Januari Makamba wamekataa posho na hata kwenye semina ya kamati ya nishati alikataa na tumeona kwenye vyombo vya habari jina lake likiwa limekatwa ilhali viongozi wakubwa kabisa wamechukua posho. Nampongeza kijana mwenzangu kwa uzalendo huu. Nawataka wabunge wengine wenye Moyo wa dhati kukataa sio tu ongezeko hili la posho Bali posho yote ya vikao. Kwa nini mbunge akubali kulipwa kwa kukaa?

Tazama nchi hii, juzi serikali ilipokea Msaada wa tshs 20bn kwa ajili ya Sensa ya mwakani wakati wabunge wanalipwa 28bn Kama posho za kukaa tu.

Tanzania inaagiza gesi ya matumizi ya nyumbani kutoka nje kwa kutumia mamilioni ya dola za kimarekani. Kuwanda cha kutengeneza LPG kinagharimu tshs 35bn tu, Wabunge peek Yao kwa mwaka wanatumia 28bn kwa posho za kukaa tu achilia mbali mishahara na marupurupu mengine.

Ipo siku Watanzania watatupiga mawe kwa usaliti huu dhidi yao

source: Msimamo wa Zitto Kabwe kuhusu taarifa ya kupandishwa posho za Wabunge kimyakimya - Wavuti
Nakubaliana na Mh.Zitto sidhani kama kwa nchi yetu kwa hali ilivyo kiuchumi huu ni wakati muaafaka kujipandishia posho "HAYA NI MATUSI KWA WALALAHOI"!!!!Imefanyika kimya kimya kwa sababu wanaelewa kuwa si uungwana na nini itakua reaction ya walalahoi kuhusiana na swala hili,hii inadhihirisha ya kua wao pia wanawasiwasi na aibu kwa uamuzi huu vinginevyo hakua na umuhimu wa usiri kwa jambo hili kama wanafikiri kua ni muhimu.Mbali na kupinga hatua hii,ninamapendekezo ya kua posho za wabunge ziwe zikitolewa kutokana na michango yao katika shughuli za bunge ili kuhepuka ulipwaji wa wabunge ambao wanaenda bungeni kuchapa usingizi kama Mh.Wassira.MUNGU IBARIKI TANZANIA,TUNUSURU NA MAAMUZI YA CHAMA(CCM)NA SERIKALI KWA MAAMUZI YAO YASIOKUA NA MANTIKI.
 
ili nchi iwe huru inahitaji kupita katika hatua kuu 4. 1. Amani 2.kutawaliwa 3. Vita ya kujikomboa 4. Amani na maelewano. Kwa Tanzania kuna hatua tumeiruka ndo maana tunaibiwa tu.. Chulukulia mfano rwanda na burundi ambao kwa sasa wanaishi kwa kuskilizana na kuheshimiana baada ya kupita hatua ya 3.
 
Kama Zitto angekaa na wabunge wenzake wa CHADEMA na kujadiliana nao kabla ya ku-issue hii statement kingeharibika nini? And what it the point ya ku-mtaja (kumpongeza January Makamba) kwenye hili?

Ulimwengu wa leo ni wa utandawazi. Litokeapo jambo lisilokubalika na umma hakuna kumung'unya na kulindana, litamkwe na kutolea msimamo wazi kabla halijaota mizizi. Kusubiri vikao ili Zito atolee kauli wakati hilo tayari linajadiliwa na vyombo vya habari tunaelekea wapi? Endelea hivyo hivyo zito.
 
Zitto's ostentatious nature is a reason behind his low popularity among his Chadema fellow high-profile figures. The guy is too bigheaded and think that he can stand on his own even in sober matters that seem to otherwise disturb Magamba's interests. His move to pressure on the Government to scratch sitting allowance was conspicuously plausible but only lacked his party's blessings before being mooted in the assembly. Unfortunately Zitto ignored the importance of his party's ratification of the issue and decided to take the task by his own, apparently for the sake of winning public approval. His plans have then proved failure and in the end sitting allowances have been increased.
 
Hamna noma 2015 waongeze nafasi za wabunge zifike hadi 10,000 au kila watu 3000 mbunge mmoja alafu unakaa vipindi viwili tu kwa mtindo huo tutakuwa tunagawana keki ya taifa. Maana huko ndiko kwa kuchumia au kutajirikia kwa wabongo.

Hahahaha mbona Zanzibar kila watu 2200 wananchi mbunge wao. Badala ya kushughulikia maslahi ya wananchi wanaowawakilisha, badala yake wao wanajineemesha kwa kufuru.
 
Hawa ndo wanasiasa wa TZ nilimsikia mh.Selasini wa CDM akichangia kuwa amegundua kuwa posho za wabunge ni ndogo sana na msimamo wa kupinga posho si wa CDM bali ni wa watu fulani wenye source zao nyingine za kupata pesa.

Hapa ndo huwa nawapa pole wanaojifanyaga wapenzi saaaaaaaaaana wa viongozi na vyama, jamani amkeni hawa wanawatumia tu, mtaishia kuandamana mpigwe, mfungwe wao wanaendelea kula raha tu.

Nakumbuka 1995 jamaa alikuwa shabiki mkubwa wa Mrema na alikuwa tayari kupigana msituni eti Mrema kaibiwa kura. After some years Mrema kwenye mkutano wa CCM anakiri kuwa CCM ni kiboko walimshinda mara 2. Niliishia kushangaa.

Zitto, usimungunye maneno, Mbowe, Lissu na wenzako wote Posho wamelamba na huna la kufanya wataendelea kulamba.
 
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni,alichosema Zito ni sahihi kabisa kama unapewa msaada wa 20b unashangilia and at the same time you are paying your own mp's 28b then where is the common sense here?!!!! Why are our leaders like this? If to have a plant of LPG is going to cost us 35b,why not investing this f***ng money so that we may be able to save few dollars that we get coz we not exporting anything!!!!!!!
Come on guys let us be serious in what palnet are we Tanzanian's living?!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!:embarassed2:
 
Back
Top Bottom