Posho za Ubunge nazo zifutwe

Posho zote pamoja na ruzuku kwa vyama vya siasa ni wizi na ujambazi usiovumilika. Tunaomba posho na ruzuku vifutwe mara moja.

1.Mbunge ama mfanyakazi atayelalamika kufutwa kwa posho ajiwajibishe mwenyewe kwa kukubali kuwaachia wengine watao kubali fanya kazi chini ya mshahara husika.

2. Chama cha siasa kitakacholalamika kufutwa kwa ruzuku ama kushindwa kujiendesha kwa michango ya wanachama wake, ina maana chama hicho hakikubaliki, ni halali yake kijifie, kwanini kuendesha chama kwa jasho la watu wengine ambao hawana vyama? Hii ni sawa na mahakama ya kadhi ama baraza la maaskofu kuendeshwa na kodi ya wananchi.

Nakumbuka tulipokuwa kule (kabla ya uchaguzi wa 2005) BCS......nilisema hili jambo...........ee bana eee baadhi ya watu walipinga sana.........sababu kubwa ni eti CCM itakuwa na advantage zaidi ya vyama vingine......nashukuru sana Mkuu kwa kuileta tena hii hoja..........
 
Wakuu, tunaenda kasi sana, na soon issue hii italeta matatizo.

Sitting Allowance, nakubali ZIONDOLEWE.

Lakini hatuwezi kuwa na wabunge tunaotazamia washiriki kuleta maendeleo majimboni, na kutetea maslahi ya wananchi maskini, halafu Marupurupu yao yawe madogo chini ya 8million (USD 5400) kwa mwezi.

Nadhani tuongelee swala la FLAT mishahara, kwa madaraja yote walimu, Madaktari, polisi, wahasibu blah blah na kusiwe na posho, ila mishahara iwe bora kwa wote.

Sasa kweli kuanza kufikiri kumlipa mbunge 2.3 million kwa mwezi, THIS IS A JOKE.
 
Moelex, hatuwezi kukata mishahara na marupurupu ya wabunge na kuacha vitu vingine vibakie constant. Uzuri ni kuwa tukianzia na wabunge wao wenyewe ndio watatunga sheria za kusimamia wengine accordingly. Ni lazima tuusahihishe uchumi wetu kwa sababu it is unsustainable. Hivi, unafikiri wafadhili wakiamua kuondoa fedha wanazotumwagia watawala wetu wangeweza kusustain the current payment regime for even a month?
 
Sasa kama hujui hao wengine wanalipwa au hawalipwi hizo posho, hapo unawa compare na wabunge au unafanya nini? What's the point? Why raise the issue of other professions' perks?
Are you a doctor?
 
Salaam,

Posho za Vikao zinapingwa kwa sababu zinakataa mantiki- Mbunge kutokana na nafasi yake ni wazi atahudhuria vikao mbalimbali vinavyoendana na majukumu yake hivyo kumlipa posho kwa kuhudhuria vikao hivyo haiingii akilini na kama wengine walivyosema ni "wizi" wa wazi. Tukikubali mantiki hiyo lazima tuangalie kile kinachoitwa "posho ya Ubunge"

Mbunge analipwa posho ya Ubunge kwa vile yeye ni Mbunge- sijui kama kuna Posho ya Urais au ya Udiwani! Na sina uhakika kama Madaktari wanalipwa "posho ya udaktari" na wahasimu wa serikali wanalipwa "posho ya Uhasibu" au yumkini kuna posho ya weledi fulani ambayo mtu analipwa. Siwezi kushangaa ipo posho ya "ualimu" au ya "udereva". Lakini kwa vile sijui hayo mengine nigusie hii ya "ubunge".

Mbunge anapogombea Ubunge anagombea nafasi ya ajira na anapopata analipwa mshahara wa Mbunge. Siyo kazi ambayo alilazimishwa au kupewa baada ya kushikiliwa bunduki kichwani. Aliiomba kazi hiyo na alijua inakuja na majukumu mbalimbali. ni kwa sababu hiyo Mbunge analipwa mshahara na ameweka maslahi mengine tofauti kama Mbunge (mkopo mkubwa wa gari, nasikia wanajengenewa nyumba - sitashangaa wakauziwa kila mwisho wa term)). Lakini kumpa posho ya Ubunge tena!?

Posho ya vikao iondoke na pamoja (siyo ikifuatiwa) na posho ya Ubunge kwani zote mbili zinakataa mantiki.
POSHO ZA MADIWANI
Mimi kama Diwani nalipwa (sio mshahara) kwa mwezi shilingi laki moja na ishirini (Tzs 120,000).

Posho ya Kikao cha Halmashauri ni 50,000 x 4
Posho ya Vikao vya Kamati 50,000 X 4
Posho ya vikao vya ALAT 65,000

POSHO ZA WABUNGE

Posho ya mafuta 2500 kwa Lita 1000 = 2,500,000
Posho za Kikao = 100,000
Posho za ukarabati wa gari – 1,000,000
Posho za Dereva – 400,000 (mbunge anaamua amlipe kiasi gani dereva)
Posho za Jimbo – 450,000 (nje ya Mfuko wa Jimbo)

(I stand to be corrected)

Mwanakijiji

Namekuwa nachangia hapa kwenye hii mada katika threads mambalimbali na kuonesha kutofautiana na members wengine hasa kwenye hili la sitting allowance ambayo Zitto na wenzake wanataka kuupotosha umma kuwa wao ni wazalendo kwa kukataa posho ya 70,000(sitting allowance)

Mshahara wa Mbunge ni 2.3ml basic plus 5ml posho ya ubunge which makes 7.3 ml kwa mwezi as a gross salary.

Mshahara wa mtumishi wa umma au mfanyakazi wa kima cha chini kwenye sekta binafsi ni kiasi gani????!!!

Huu mchezo wa Ziitto na wenzake ni wa hatari sana(NI WALAGHAI/WAONGO)
 
Hivi ikiondolewa sitting allowance tatizo la posho na matumizi mabaya ya fedha za umma litakuwa limeondolewa? Lets reform the whole allowance system.
 
Hvi wabunge wangekuwa wanalipwa kama mwalimu wa shule ya msingi kuna ambae angegombea?Hizi fujo za ubunge zingekuwepo?
 
Hivi karibuni kumekuwa na mjadara mkali kuhusu posho za wabunge kufutia pendekezo la mh Zitto Kabwe kutaka zifutwe, Kwa mara kazaa nimepata kuona msimamo wa spika kupitia vyombo vya habari, na pia kupitia mwanachi ya leo nimepata kuona msimamo wa serikari kupitia waziri mkuu Mh Mizengo Pinda(mtoto wa mkulima) yote ya mejikita kuelezea posho kwa hatua hii sipendi kuamini either chadema au zito wametumia hoja hii kama mtaji wa kisiasa, najaribu kushawishika kwamba ni masrahi ya Taifa ndiyo yamewasukuma kufikia kutoa pendekezo hilo.

sasa najiuliza nguvu nyingi zinata pasina kuangalia zinalenga kurinda masrahi ya Taifa, ya watubinafsi kwa maana ya wabunge au ya chama fulani.

Ningeshauri hoja itumike kuonyesha uhalali wa kulipa posho wakati tanzania iko karne ya ishirini na moja lakini maadui wa maendeleo (kwa maana ya Maradhi na ukosefu wa elimu Bora vikishika kasi kila kukicha)

Vivyo hivyo kwa watoa hoja Chadema, nami pia niliamini hoja ya kufuta posho imekuja wakati muafaka lakini nahisi haikuingia mahara pake kwani ni dhaihili itakuwa imetamkwa either kwenye sheria mama inayosimamia shughuri za bunge au kanuni za bunge, hivyo basi kwa uelewa wangu mdogo niliamini kama kweli hii hoja inasukumwa kwa dhati ya nafsi zetu, napengine kuangalia masrahi ya walala hoi, nilitegemea muheshimiwa Zitto aipeleke kama hoja binafsi bungeni(Private motion) kuomba bunge lilidhie mabadiliko ya kanuni za Bunge ausheria mama, kwani kwa marumbano ya kuandikiana barua au kupitia vyombo vya habari au maandamano yanaweza kuwa yasiwe na tija.

lakini pia pesa hizo zimewekwa kwenye kasima ya serikali kuzikataa inaweza sisilipwe lakini bado zikatumika ndivyo sivyo, hivyo ni jukumu la Bunge na wabunge kusimamia swala hili pasina kujali masrahi ya Chama au mtu binafsi, wakitanguliza uzalendo, uhalisia wa maisha na masrahi ya watnzania mbele.

Moderator, Naomba kutoa hoja
 
Kama wabunge wanaweza kugombea kuhusu posho badala ya kujadili mambo ya msingi yanayomkabili mpiga kura wao unafikiri tuna wabunge wa aina gani, wabunge wanawaza maslahi yao binafsi na matumbo yao ndio maana wanapiga kelele za posho wabunge wa namna hii ndio wale wakirudi majimboni mwao wanawachangisha wapiga kura wao wajenge shule badala ya kuwasaidia na kuwapa mbinu mbadala
 
Ndugu zangu wadanganyika waziri mkuu jana kaeleza kuwa posho za wabunge zinaishia nje tu kwa kuwasaidia jamaa zao.
Hivi ni kweli unaweza kuonana na waziri mkuu hivihivi tu kwa kuomba msaada wa pesa kama hujala kirungu cha polisi?
 
Ile sababu haina uzito wowote wa kupinga mada ya posho. Wale watu ni matokeo ya wao kujilipa vizur na kusahau raia wengine weny maisha magumu.
 
Ile sababu haina uzito wowote wa kupinga mada ya posho. Wale watu ni matokeo ya wao kujilipa vizur na kusahau raia wengine weny maisha magumu.

Watu ambao wapo kwenye uongozi Tanzania hawakudeserve kabisa kuwa hapo walipo. Hebu fikiria waziri mkuu anatetea hoja ya posho kwa kusema kuwa the moment mbunge anapoipokea inaishia nje kuna watu wanasubiri kusaidiwa.

Anazungumza hivyo bila aibu kabisa. Yawezekana na yeye hajaelewa kabisa mantiki ya kuondoa posho hizo kama ilivyo kwa mtoto wa Malecela au ni ufisadi uliomkaa kichwani kiasi cha kupofushwa independent thinking yake, i just do not know.

Mie nasema hawa jamaa bila ya kuwafukuza madarakani tunatafuta maafa tu.
 
Yaani pinda ni boga sijawahi kuona ..anatoa sababu as if ni katibu tarafa..hivi hii nijitu mingine inakuwaje viongozi.?? yaani mawazo utadhani muuza kashata..aghhhh
 
Yaani pinda ni boga sijawahi kuona ..anatoa sababu as if ni katibu tarafa..hivi hii nijitu mingine inakuwaje viongozi.?? yaani mawazo utadhani muuza kashata..aghhhh
eti mtoto wa mkulima!!!huyu??!
hiyo kichwa yake ni kama ilivyo kuwa yangu nilipokuwa chekechea!!
huwezi kutuambia hizo posho wanazitumia kuwasaidia ndugu hapo mlangoni!!
anamaanisha sisi tusio na posho hatuwasaidii ndugu zetu!!!
kwani matumizi ya mshahara yanazuia kuwasaidia ndugu!!!!
aaaagggghhh!
 
huyu na dada yake wapo wapo tu.
hapo ndo naona DAWA YA SABUNGE KWA BABUU HAIKUMSAIDIA,
Serikali gani ukienda kila sehemu unakutana na mabogus isipokuwa kwa MAGUFULI TUU!
yAANI HILI LICHAMA HATA LIKIFA LEO SAWA TUU!
siipendi ccm hata wanaovaa nguo za kijani woote nawachukia,
 
Ndugu zangu wadanganyika waziri mkuu jana kaeleza kuwa
posho za wabunge zinaishia nje tu kwa kuwasaidia jamaa zao.
Hivi ni kweli unaweza kuonana na waziri mkuu hivihivi tu kwa kuomba msaada wa pesa kama
hujala kirungu cha polisi?

Mungu ibariki Tanzania!
 
Back
Top Bottom