superfisadi
JF-Expert Member
- May 22, 2009
- 553
- 52
kwa kuanza hizo posho zao cdm ziingie kwenye mfuko maalum kila mwaka wazipangie matumizi kwenye maeneo yaliyopotezewa na bajeti ya serikali huo utakuwa mwanzo mwema
Chadema wanapigania kubadilisha mfumo wa hayo malipo sio kususia mtu mmoja mmoja, mbona wewe mgumu kuelewa Mkuu? Unasusia na mfumo unaendelea utakuwa umefanya nini? Nimewasikia hata akina Chiligati na Nape wakizungumza kama wewe na hii inaonyesha kuwa hata viongozi wenu hawaelewi CHADEMA wanazungumzia nini. SHAMEUsanii mtupu mbona milioni 90 Chadema waliramba!
Chadema waonyeshe mfano kwa hili na kama magamba ya kikataa wapate pointi ya kutoka nayo kwa wananchi baada ya bunge. Hii itawapa pointi nzuri sana wao wakomae nao tu!
Na tungoje kama hoja itapenyeza mjengoni
Serikali inatarajia kutumia Sh. trilioni 12.8 kwa mwaka wa fedha wa 2011/2012, kati ya hizo Sh. trilioni 8.8 ni kwa matumizi ya kawaida, yaani posho na mishahara na ulaji mwingine, wakati fungu la maendeleo ni Sh. trilioni nne tu.
Utaratibu wa kupitisha bajeti ya ulaji umekuwa ni utamaduni wa taifa hili, kwani hata mwaka huu wa fedha unaomalizika serikali ilipitisha bajeti ya Sh. trilioni 11.6, kati yake Sh. trilioni 7.7 zilikuwa kwa fungu la kawaida na Sh. trilioni 3.8 kwa ajili ya maendeleo.
Soma maoni yetu ukurasa wa sita
hivi tunairudishaga ccm madarakani kwa sasbabu sisi ni wajinga au kwa sababu hatujui au ka sababu hatuna elimu ya kutosha
Nimevutiwa sana na pendekezo la wabunge wa CHADEMA kuwa posho ya vikao ifutwe ili pesa zipelekwe katika kuboresha huduma za jamii.
Huo ni uzalendo wa hali juu kwa waheshimiwa wabunge katika kipindi hiki ambacho taifa letu linapitia katika mawimbi makubwa ya kuwepo kwa matatizo ya kiuchumi na kijamii.
Nachukua fursa hii kuwaomba waheshumiwa wakiongozwa na ZITO waepuke kupokea posho za vikao katika bunge la bajeti na pesa husika zifunguliwe mfuko maalum kwa kusaidia jitihada za wananchi kujiletea maendeleo. Kama tujuavyo wawapo DODOMA wabunge wetu wanapata posho za aina 2; za vikao na kuishi, hivyo living allowanze waendelee kupokea ili jioni waonekane PAKO NI PAKO na viwanja vingine. ILA SITTING ALLOWANCE WAIEPUKE.
Kuchezwa kwa ngoma, kuanzishwa na mpigaji!