Posho mbili, Spika Sitta, Takukuru na Maadili yake!

Helo wanaJF kwanza ninawasalimu, hodi! Ndio naingia kwenye forum, nikaona ni vema nianze na hili lililoko mezani. Kidogo hata mimi ninakubaliana na kukosa imani na huyu mheshimiwa, lakini ukumbuke kuwa si siku nyingi walimweka kitimoto na kujaribu kupunguza hiyo speed and standard. Suala la Richmond kwa jinsi lilivyo tete alipaswa kulipa kipaumbele na hasa ikizingatiwa kuwa tuko kwenye crisis kama hiyo iliyopelekea kashfa hiyo kuibuka
 
agenda kubwa kwa spika sita ni kuwapendeza wabunge kwa maslahi. mishahara, posho, fungu la la majimbo nk. sasa pia anapigia debe posho mbili mbili na kuziita ukarimu wa kiafrika. masikini kukarimu matajiri kwa posho za kimtindo ambazo nazo kwa kawaida ni zaidi ya posho za bunge.

kwa kuwapendelea wabunge kwa maslahi yao binafsi anadhani hawezi kung'olewa ubunge.

macinkus

Sidhani kwamba bila kuungwa mkono na idadi kubwa ya wabunge Spika peke yake angeliweza kuzima hoja yoyote inayoletwa bungeni iwe ni kwa maslahi ya wabunge wenyewe, au hata kwa maslahi ya taasisi yoyote ile au hata taifa. Tusisahau kwamba hata Waziri Mkuu na Mawaziri wamo Bungeni na wao kama wangeliona hayo ya posho, mishahara n.k. hayana tija wangelipaswa kuwa wakweli na kusimama kukataa nyongeza ama posho hizo. tusimvike Spika zigo hilo peke yake. Hata Rais naye anapaswa kukemea au hata kupinga iwapo anaona yanayotendeka ndani ya Bunge si sahihi. Viongozi waliona sawa tu wabunge kuongezewa maslahi!
 
mmm. jamani tunakoelekea siko. mnamwonea spika wetu mnasema ni kinara wa ufisadi hii si kweli, mnamchafua mi ninichojua huyu baba ni mpiganaji, acha hizo
 
nilimwamini, nikamkubali, nikasema tumepata jasiri wa kusema kwa ajili ya wanyonge. Akaanza kwa mbwembwe za speed and standard,akatetea nyongeza ya mishahara ya wabunge,akasemwa,akatulia!

Lakini kwa namna anavyoshughulikia swala la richmond, halafu hashughulikii mengine kwa kasi hiyo, napoteza imani nae. Kama vile ana kisasi flani. Mbona kagoda haiundiwi tume? Meremeta? Tangold?

Mbona anatetea sana wabunge hata kwenye mambo ambayo yanaonekana wazi yanahitaji kuguswa?

Mbona ikiguswa ofisi yake anageuka mbogo? Au milioni sabini ni hela za chai kwake? Haoni kama zingewaletea maji wamasai wa ngorongoro? Mbona ofisi yake ikiguswa anawaka wakati ye ndo kinara wa ufisadi?

Kwa haya na mengine mengi, napoteza imani na huyu bwana, nadhani ndo maana wakina el na ra kila siku wanawaza kumpindua


wewe una lako jambo!
 
Kwa mara nyingine Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh Samwel Sita amezungumzia suala la Wabunge kulipwa posho zaidi ya moja kwa kuunga mkono Wabunge kupokea posho zaidi ya moja kwa kazi ile ile! Alisema wanaozungumzia suala hilo waonane nao majimboni na wanawaonea wivu kwamba wanafaidi! Cha kujiuliza ni kwamba kama Spika Sita aliwataka Wabunge wakahojiwe huku anaunga mkono wabunge hao kulipwa posho zaidi ya moja, sasa aliwataka wakahojiwe kuhusu nini? (Source: www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=15648).
 
Kwa mara nyingine Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh Samwel Sita amezungumzia suala la Wabunge kulipwa posho zaidi ya moja kwa kuunga mkono Wabunge kupokea posho zaidi ya moja kwa kazi ile ile! Alisema wanaozungumzia suala hilo waonane nao majimboni na wanawaonea wivu! Cha kujiuliza ni kwamba kama Spika Sita aliwataka Wabunge wakahojiwe huku anaunga mkono wabunge hao kulipwa posho zaidi ya moja, sasa aliwataka wakahojiwe kuhusu nini? (Source: www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=15648).


Kipengele kipi kna halalisha posho hizo na kwa PCCB ni kipengele kipi ninazuia posho mbili ?
 
0006


Haya ndio maswala ya kuangalia na pengine kuchunguzwa na Takukuru...
 
Kipengele kipi kna halalisha posho hizo na kwa PCCB ni kipengele kipi ninazuia posho mbili ?

Kipengele cha ubadhirifu wa fedha za umma kinyume na kifungu cha 28 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, 2007, Na. 11/2007!
 
Buchanan,
Mkuu ubadhirifu huo ni baada ya mkaguzi wa mahesabu kutoa taarifa yake..PCCB hawawezi kufuata sheria hiyo ikiwa hakuna ushahidi tosha na sio kuutafuta ushahidi ktk kosa ambalo hawajui kama lipo au halipo.
 
Buchanan,
Mkuu ubadhirifu huo ni baada ya mkaguzi wa mahesabu kutoa taarifa yake..PCCB hawawezi kufuata sheria hiyo ikiwa hakuna ushahidi tosha na sio kuutafuta ushahidi ktk kosa ambalo hawajui kama lipo au halipo.

Ushahidi unapatikana baada ya uchunguzi! Unataka kusema CAG akibariki hesabu ndio hazina matatizo? Kama PCCB itasubiri mpaka CAG aseme kuwa kuna ubadhirifu sasa wao wapo kwa ajili ya nini? Wake up pls!
 
roho inaniuma sana jamani, Viongozi wanapotetea ujinga. Ndio maana gap between rich and poor linazidi kuongezeka. Hizo 6.9 m hapo bado hajalipwa mshahara, na posho hazijalipwa marahaba mbili! du!?!ukiongelea mshahara wa mwalimu, hiyo ni topic nyingine ambayo mmh, acha tu.
 
Sasas mafuta kwa nini wanapewa kwa bei ya TShs 2500 kwa lita ? why? Na je Takukuru wanaliona hili? Kwa sababu lita moja ni wazi sio Tsh 2 500. Kwa hiyo wabunge wote wahojiwe tetehteh.Kwa upande wa hizi posho nyingine nadhani wa kuhojiwa ni anayetoa posho... kwamba je uliwapa hizi posho kwa misingi ipi?
Na kwenye mafuta iulizwe serikali kuwa je kwa nini mafuta unalipa Tzs 2 500 badala ya Tzsh 1 600 ? Kwa kuwa serikali ndio inayowalipa wabunge kwa hiyo hili ni swali la Pinda .. Je unajua bei ya littre moja ya mafuta? mbona umelipa zaidi? Kama ni audit querry inatakiwa ianzie kule walipolipa posho .. na kwa hii ya mafuta ni serikalini..Takukuru kazi hiyo ..changamke..issue nje nje ...
 
Mpokeaji wa posho ndiye anajua amepokea wapi na wapi! Mtoaji atajuaje kama mpokeaji amepokea posho nyingine? Kwa mfano mtumishi akiitwa kwenye semina aliyemwita atamlipa posho. Endapo mtumishi amelipwa alikotoka hakuna haja ya kulipwa tena mara ya pili! Kumbuka serikali ni ile ile, kwa hiyo haiwezekani ikamlipa mtumishi yule yule kwa kazi moja!
 
roho inaniuma sana jamani, Viongozi wanapotetea ujinga. Ndio maana gap between rich and poor linazidi kuongezeka. Hizo 6.9 m hapo bado hajalipwa mshahara, na posho hazijalipwa marahaba mbili! du!?!ukiongelea mshahara wa mwalimu, hiyo ni topic nyingine ambayo mmh, acha tu.

Sure, kuna haja ya kufuatilia juu ya mafuta vile vile (TSh 2,500 badala ya 1,600)! Sasa hivi watapewa fedha kwa ajili ya Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo, tutasikilizia vijimambo hapo!
 
Ndugu zangu lazima kila kitu kiwe na mwanzo wake. Kama kuna udanganyifu unafanywa na wabunge uanikwe na ukemewe. Kama wabunge is mafisadi kwanini wagushi risiti? Kwanini walipwe mara mbili kwa kazi moja? Wanaosema kwamba ni kwa sababu ya wao kuibana serikali kuhusu Richmond haina mantiki yoyote. Wote wanaohisiwa wahojiwe na wale watakaokua na hatia warudishe hizo hela zetu na wengine ikibidi waburuzwe mahakamani. Baadhi ya wabunge wanaficha maovu yao kwenye kivuli cha kupambana na ufisadi.

Nanu,
Kulipwa mara mbili inaweza ikawa ni kosa la kimfumo au utendaji, ambalo uongozi wa Bunge unaweza kulishughulikia, lakini sidhani kama ni rushwa hasa ukitilia maanani kuwa halikuanza kwenye Bunge la sasa. Huu ni utaratibu wa siku nyingi na upo pia serikalini.

Serikalini watu wanalipwa posho za vikao hata kama vinafanyikia maofisini mwao.

Takukuru wanatakiwa kutumia muda wao kushughulika na rushwa zinazoiyumbisha nchi kama za EPA, Radargate, Richmond n.k.

Kwa wao kuhangaika na mambo ambayo sio ya rushwa inaonyesha wazi kuwa wana nia tofauti na ile ya kupambana na rushwa.
 
Dr. Slaa alishalalamika hili juu ya mapato makubwa ya wabunge.

Wakamwijia juu kama Mazimwi waliotishiwa kunyang'anywa nyama zao.

Ili nchi iwe safi inabidi kwanza kusafisha BUNGE. Hapo ndipo kwenye mzizi wa fitina.

Mambo yanaanzia pale. Wizi unaanzia pale. Ufisadi unaanzia pale.

Bunge imara, hata RAIS ataliogopa. Wataweka sheria na vyombo vya kulinda maslahi ya TAIFA. Kama bunge limelala, basi kila kitu ni ZII. Haitasaidia kuwa na Mkapa au Kikwete au nani sijui. Bunge ndiyo mwanzo na mwisho wa Tanzania.

Tulisafishe lile bunge na mengine yoote yatafanikiwa. Hawa wabunge wa Ndiyo Afande hawatakiwi tena. Ila huwezi shangaa wanakuwa Yes Sir kama wao wameingia kwa RUSHWA. Aseme no akione.
 
Ukisoma ile barua ya waziri Mkuu inaonyesha hizo taasisi zinalalamika kuwa wao hawana fungu kwa ajili ya posho za wabunge.. kwa hiyo kimsingi walilipa kitu ambacho hakipo kwenye budget zao na sio utaratibu wao.. sasa swali ni kwa nini walilipa? si wangesema hatuna hata kama wabunge walidai?Hatat hivyo hii haindoi jinai kwa wanunge kulipwa mara mbili .. lakini kimtiririko ilitakiwa waulizwe waliolipa..
 
Siasa za Tanzania ni za kijinga sana,watu wanazungushana tu wakati maskini wanazidi kuumia. Hata hatuna haja ya viongozi tena kwani viongozi tulionao ni kama majitu ambayo hayakuumbwa na Mungu. Ukimchagua kiongozi maana yake akutumikie umlpe na si wewe umtumikie na kisha umlipe. Hiyo ndio inayoendelea Tanzania. Ndio maana vifo vyao vinatokeaga kiajabu ajabu lakini hawajawahi kungamua ni kwa nini, kumbe ni huyo roho mchafu wa wizi na unyang`anyi anawaangaisha.Wageni wafikapo Tanzania wanakuwa na rights kuliko alizonazo raia, wakati huku ugenini sisi hata katika huduma mzawa anahudumiwa kwanza ndio wanakuangalia wewe. Tanzania Mzungu anaiweza kuingia hata Ikulu bila hata ya appointment. Im juz crying for poor people of Tanzania. God here my Prayer for ur people.
 
Waheshimiwa gani hawa wasiojiheshimu! Na sisi tuanze kwa kukataa kuwaita "waheshimiwa".

Amandla.......
 
Back
Top Bottom