Posho mbili, Spika Sitta, Takukuru na Maadili yake!

Hawa watu mbona wanafiki sana. Hivi wanataka kutuambia ni wabunge ndio wamekuwa wakidai wapewe posho hizo au ni taasisi zenyewe zinaamua kutoa? Kama mbunge kupokea posho hiyo ni kosa (rushwa?), kwa nini serikali kupitia taasisi hizi haziwajibishwi pia kwa kutoa rushwa hiyo? (Tunaambiwa hata takukuru pia imewahi kutoa posho hizo!).

Nadhani takukuru wangeanzia kwenye hizi taasisi (hususani takukuru yenyewe) ili kujua ni kwa nini wanatoa posho hizi huku wakijua fika kwamba wabunge tayari wanapewa posho na bunge.
 
Solution ni kuwafilisi sio kuwahoji kama ushahidi wa hizo posho za mara mbili mbili dhidi ya wabunge upo. Hao TAKUKURU nao wasijifanye miungu watu nao pia lazima wawajibishwe. Habari ya Richmond inachosha. Na Don Rostam anajua mwakani watamtafuta tena kwa hiyo lazima alindwe na asafishwe.

By the way kuna taarifa zisizokuwa rasmi/tetesi kwamba jamaa wa ikulu wamefukua pesa zilizokuwa zimefukiwa chini kwenye Ma -Sim tank huko Monduli na kuzirudisha serikalini.(sina uhakika nazo ila nazileta jamvini najua wapo wanaojua humu kuhusu hiyo ishu)
 
Mwakyembe Mwakyembe - Duh!
Hivi huyu jamaa anadhani yeye ni mkubwa sana kiasi cha kuwaona vijana wa TAKUKURU kuwa hawana uwezo wa kumhoji? How do you know someone is just a junior?

Kwani alitaka ahojiwe na Dr. Hosea mwenyewe au?? Mi naona inafika wakati hadi naona vitu vyote vinavyoendelea nchi hii ni maigizo tu!

Mungu Ibariki Tanzania
 
Spika Sitta kigeugeu
• Akana kauli zake, barua rasmi ya ofisi yake

na Charles Mullinda



Alipoulizwa kuhusu uhusiano wake na Katibu wa Bunge, Kashililah kama ni wa shaka kiasi cha kuandika barua nyeti inayoomba msaada wa taasisi nyingine pasipo kumtaarifu, Spika Sitta alisema haamini kama Kashililah aliandika barua hiyo na kama aliandika, basi alilazimishwa na viongozi wa juu wa serikali.

Katika hatua ya kushangaza, Spika alitoa kauli nyingine kuwa hata kama Kashililah aliandika barua hiyo, basi alikuwa anatekeleza majukumu yake ya kiutalawa hivyo anaweza asimtaarifu lakini TAKUKURU walipaswa kutochukua hatua zozote kulingana na barua hiyo kabla ya kumtaarifu.

"Mambo ya utalawa sishiriki kila jambo, mhusika mkuu ni katibu na nadhani alilichukua kiutawala zaidi. Lakini TAKUKURU kabla ya kuanza kuifanyia kazi barua hiyo ni lazima wangenitaarifu kwanza Spika.

"Hili jambo tumelijadili sana jana na juzi, tumebaini kuwa Katibu wa Bunge alitishwa sana. Watu wakubwa serikalini wamekaa vikao vingi tu, wamemtisha sana katibu kuwa ni lazima aandike barua hiyo, oh… eti ni maagizo ya rais, wakamlazimisha kuandika barua ile. Hili mimi siliafiki na tumefikisha malalamiko kwa waziri mkuu leo.

"Bunge haliwezi kuendeshwa kwa vitisho, serikali iache kabisa kulitisha Bunge…. Bunge litakataa. Kama mbunge anatuhumiwa kuna Kamati ya Maadili ya Bunge, itashughulikia tuhuma hizo, si mambo haya yanavyofanyika sasa. Ni njama tu, lakini kamwe hatulegezi kamba, Bunge litaendelea na kazi yake pamoja na vitisho vyote," alisema Spika Sitta.

Wakati Sitta akitoa kauli tatanishi kuhusu barua iliyoandikwa na Kashililah kwenda kwa Hoseah huku akisisitiza kutoifahamu, Tanzania Daima Jumatano imefanikiwa kuiona barua hiyo yenye kumbukumbu namba CEB.50/155/05/81 ikiwa na kichwa kinachosomeka: ‘Baadhi ya kamati za Bunge kuomba takrima serikalini na katika mashirika ya umma.'

Sehemu ya barua hiyo inasomeka hivi: ‘Tafadhali rejea mazungumzo kati ya Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Bunge kuhusu suala tajwa hapo juu.
‘Nimepokea malalamiko kuhusu mwenendo usioridhisha wa kamati za Bunge kuomba takrima kutoka kwa watendaji wakuu serikalini na mashirika yake wanapohojiwa na kamati za Bunge.
‘Hivyo ili kuepuka athari zaidi, ilionekana kuwa ni busara jambo hili likatazamwa kwa kina ili kuainisha chimbuko lake linaanzia wapi, nani wahusika wakuu, hatua gani zichukuliwe na kwa utaratibu upi. (Rejea nyongeza ya nane ya kanuni za Bunge za toleo la 2007 kuhusu mgawanyo wa kazi wa kila kamati).
‘Ni tegemeo langu kuwa suala hili utalipatia kipaumbele na kulitazama kwa ungalifu mkubwa, kwa kuzingatia aina ya makundi yanayohusika na nafasi yake katika jamii ya uongozi wa nchi, ili pamoja na kulitafutia ufumbuzi, bali pia kuwa makini katika kulishughulikia.'
Barua hiyo pia imenakiliwa kwa Katibu Mkuu Kiongozi na Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa.
Spika alipoulizwa kuhusu barua aliyoandikiwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Mei 26 mwaka huu ikimtaarifu kuwa amepokea malalamiko kuwa wabunge wanadai posho wanapotembelea ofisi za serikali, taasisi na mashirika ya umma, Spika Sitta alikana huku aking'aka na kuhoji kwa nini mwandishi anambana kwa maswali magumu.

"Kwa nini una mambo magumu sana wewe, mwandishi gani huridhiki na maelezo unayopewa, kila ukijibiwa unaendelea kuhoji hoji tu, basi andika unavyotaka, mimi sijaona barua niliyoandikiwa na Waziri Mkuu ikielezea kuwapo kwa jambo hilo," alisema kwa ukali Spika Sitta.
Wakati Spika Sitta akikana kuiona barua hiyo, Tanzania Daima Jumatano imefanikiwa kuiona barua hiyo yenye kumbukumbu namba PM/P/2/567/33, yenye kichwa kinachosomeka: ‘Malipo ya posho kwa wabunge wanapotembelea kikazi ofisi za serikali, taasisi na mashirika ya umma.'
Sehemu ya barua hiyo inasomeka hivi: "Kwa muda mrefu sasa zimekuwapo taarifa mbalimbali kwamba baadhi ya kamati za Bunge zinapotembelea wizara, mikoa, taasisi za serikalki na mashirika ya umma, ama zinaomba au zinadai kulipwa posho mbalimbali. Posho hizo ni pamoja na posho za kujikimu, posho za kikao na takrima.
"Nimepewa taarifa kuwa wizara ambazo maofisa wahasibu walitakiwa kufanya malipo hayo ni pamoja na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maji na Umwagiliaji, Afya na Ustawi wa Jamii, Maliasili na Utalii, Nishati na Madini, Kilimo, Chakula na Ushirika na Viwanda, Biashara na Masoko.
"Nimeona ni busara nitoe taarifa hii kwako ili uweze kutumia njia zako za kiofisi kuwaasa waheshimiwa wabunge wachache wanaofanya hivyo waache, kwani mambo kama haya yanaweza kulipuka siku yoyote na yakalifedhehesha Bunge letu tukufu."
Barua hiyo ambayo imesainiwa na waziri mkuu mwenyewe, imenakiliwa kwa Rais Jakaya Kikwete na Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo.

Wakati huo huo, Spika Sitta jana alimtetea msaidizi wake, Christopher Ndallu, kuwa hahusiki na upotevu wa aina yoyote ya fedha za Bunge wala hajashindwa kurejesha masufuru kama ilivyoelezwa na Kamati ya Hesabu za Serikali.
Akizungumza kupitia simu yake ya kiganjani kuhusu tuhuma hizo zilizoelekezwa kwa msadizi wake huyo, Spika Sitta alisema si kawaida yake kuzungumzia mambo ya kitoto kama hayo ya msaidizi wake kushindwa kurejesha masurufu kwa fedha anazochukua, lakini amelazimika kufanya hivyo kwa sababu jambo hilo linakuzwa.
Alisema, kamati hiyo ina chuki binafsi, jambo linalodhihirishwa na uamuzi wake wa kuamua kuhoji matumuzi ya safari zake wakati akiwa nje ya nchi na msaidizi wake aliyetuhumiwa naye akiwa hayupo.
"Mimi sichukui masufuru, hilo kwanza lieleweke. Lakini Spika ana mambo mengi sana, hivyo fedha inayozungumzwa ni ndogo mno. Ninahudumiwa na serikali kwa safari zangu za ndani na nje ya nchi, nyumbani kwangu na ofisini kwangu, sasa milioni 70 kweli zinaweza kuwa gumzo kwa hadhi ya Spika? "Mambo ya kurejesha masurufu yana matatizo makubwa, Ndallu ana kila kitu, anazo risiti zinazodaiwa hazionekani na ushahidi mwingine wote. Ni majungu tu, hii kamati ina chuki binafsi, ndiyo maana wameamua kuhoji hili mimi nikiwa sipo na Ndallu pia. "Nimeamua kuzungumza hili kwa sababu limekuzwa sana, lakini huwa siongelei mambo ya kitoto namna hii. Milioni 70 kwa hadhi ya Spika wapi na wapi, nahudumiwa na serikali safari zangu, walinzi wangu, wasaidizi wangu, nyumbani na ofisini kwangu, sasa hiyo pesa unayohoji, kweli haya yote kwa Spika! Mbona hawahoji kwa Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu au Jaji mstaafu. Kwa nini Spika tu?" alisema Spika Sitta
.


If true, that interview smacks of outright arrogance, snobbishness, insensitivity and conceit. For crying out loud, what "hadhi" does the Rt.Hon Speaker thinks he has? One to belittle a claim, regardless of its validity, of a misappropriation of public funds to the tune of TSh. 70 mil?

That's a lot of money and some respect of public finances will be appreciated.
 
Naendelea kujiuliza uwezo wa kufikiria wa watu walioko kwenye ofisi nyeti za nchi yetu ukoje. Hii ni mbinu nyingine ya kulizima bunge lisijadili hoja za rushwa serikalini. Kama kweli ikulu ina nia njema na nchi yetu, iache kuagiza vyombo vyake kufanya mambo yanayoonekana ni kinyume na interest za utawala bora.Hii ni mbinu nyingine ya kuzima wabunge midomo ila ni strategy ambayo kwenye zama zetu hizi haiwezi kufanya kazi maana ni kujitafutia aibu.People are well informed
 
Demusa!

Hold on kinachogomba hapa sio swala la nani ni mkubwa! Watz bwana? Akili za kupepea. Mh. Mwakyembe anasema kuna taratibu za kumhoji mtu anayetuhumiwa kudai/kupokea au kutoa rushwa. Kumpigia mtu simu na kumwita is one of the dragonian tactics za kutishia watu.

Hao vijana wa TAKUKURU walitakiwa kufuata utaratibu wa kumpelekea mtuhumiwa wito. Na kama hilo lingefanyika Dr. Mwakyembe akiwa ni mtaalam wa sheria asingeweza kuwakatalia. KWA KUMPIGIA SIMU ni kujaribu kumtisha and at this juncture left or right Dr. Mwakyembe remains right mpaka wampelekee summon ya kisheria.

Sasa kama sio danganya toto ya Dr. HOSEA kwa nini wasichukue hatua na kwenda kupiga porojo kwenye magazeti ambayo wamiliki wake ni watumwa wa ROSTAM & COMPANY. Kustaafu kwa Mwanyika kunatuachia mwanya wa kushughulikia mafisadi lakini bado yuko Feleshi ambaye ni Mtumwa wao. Ithink we need a change tupate DPP ambaye hana uhusiano na Don Andy Chenge the kin pin Mafioso. Akina Mwakyembe mkomae hao akina Mwanyika na Arthur lazima wafuate nyayo za Mramba na Mgonja pia ua vinginevyo patachimbika!!! Kama mtawasahau Karamagi na ile kashfa ya Buzwagi ,TICTS na Tanga Cement!!! sijui. Itabidi CCM watumie another 200bn mwakani kununua ushindi as in 2005.
 
we will know it all huyu Mwakyembe ni another generation ya mafisadi hana lolote makelele tu ..anapayuka kuhusu Richmond kumbe na yeye alikuwa na kampuni yake kwenye dili hizo hizo za umeme wa dharura..aaaahgggggg .asihojiwe yeye nani kwani?

Sikujua kama JF kuna watoto wa mafisadi kama wewe, naona mmeguswa mwaka huu inakula kwenu na baba zenu, kama Dr.mwakyembe ni fisadi wa umeme mbona hujamwambia baba yako fisadi ampeleke mahakamani, mwaka huu inakula kwenu.Watanzania wengine sijui mmezaliwa mwaka gani na siku gani, bado hamjaona wabunge wetu machachali wanafanya nini mpaka sasa hivi.Tuwasamee bure nyinyi watoto wa mafisadi lakini mwaka huu ni wa mwisho kwenu.
 
Nadhani PM anakosea kutetea msimamo wake kwa kusema kuwa Rais ameagiza kwasababu Rais ni muhimili wa dola kama Bunge lilivyo kwa hiyo sidhani kama Rais ana mamlaka ya kuagiza wabunge wahojiwe na kama ndivyo basi hapo katiba imechemsha inatakiwa irekebishwe. Wabunge wanaweza kumwajibisha Rais kwa kupigia kura ya kutokuwa na imani naye, na Rais anaweza kuwawajibisha wabunge kwa kuvunja Bunge, Je? Bunge linaweza kuamuru Rais ahojiwe? kama hapana Vivyo hivyo Rais hawezi kuamuru wabunge wahojiwe.

Alafu watu mkumbuke kuwa Rais ana kinga sawa sawa na Wabunge, huwezi kumtuma Kopolo kumhoji Rais, Mbunge napigiwa Saluti (sikumbuki mpaka cheo gani) kwa hiyo mtu anayenipigia saluti kwa mujibu wa Itifaki hawezi kunihoji. Kwa hiyo 6 yupo sahihi kwenye suala la kiprotocol.

Tuachambue hoja za kisheria zinazogongana hapa, naona watu wengi tunaongelea feeling, Ndio maana watu wanalia kuwa katiba imekaa vibaya ibadirishwe, na hapa tunaona wazi mgongano wa kikatoba, ambapo waziri mkuu anadhani kuwa bosi wake Rais yupo juu ya chombo cha kutunga sheria(Sik!). Mihimili ya Dola Serikali (Rais) Mahakama (Jaji Mkuu) na Bunge (Spika) hawa watu walipaswa wawe na nguvu sawa kwenye uwiano wa mzani ili demkrasia ya kweli iweze kuprevail kwenye nchi.
Mkuu hapo sijakupata kisawasawa,sijaisoma katiba kisawasawa,lakini mimi kama mwanajeshi nachojua mbunge anapigiwa saluti akiwa bungeni tu,na hii ni baada ya wenyewe kuidai sana.Pili nachojua Rais ni amiri jeshi mkuu,so ana mamlaka hata ya kumtuma askari mdogo akamkamate(sembuse kumhoji) mtu anayempigia saluti.Na nachoelewa pccb wako chini ya ofisi ya rais,so anaweza kuwaagiza wakamhoji mtu.Mwisho mkuu wangu kasome kwenye katiba madaraka ya huyu rais wa tz ndo utachoka alivyo na power.
 
Jamani, kilicho MUHIMILI ni BUNGE sio WABUNGE. Posho(rushwa) hizi wamezipokea nje ya BUNGE kinyume na taratibu. Sasa wanataka ziitwe TAKRIMA/UKARIMU ni mambo ya kijinga kwa kweli. BUNGE letu litaisimamiaje SERIKALI na TAASISI zake endapo kila wanakoenda wanahongwa kwa staili na mitindo tofauti?
 
Hapa ni suala la mipaka na kufanya kazi ovyo ovyo tu. Tangu lini suala la kupokea posho mara mbili mbili limekuwa rushwa? Kama lipo na likathibitika kuna taratibu za kufuata na si hii ya kuburuzana kwenda kuhojiana. Posho zote zinatolewa kwa kusainiana. Kuna tatizo gani kukusanya ushahidi huu bila kumhusisha mtuhumiwa maana nakala za malipo zitakuwepo katika ofisi husika? Kama ushahidi wanao wa mtu amesaini mara mbili kwa kazi hiyo hiyo basi ataarifiwe muajiri wake kwa hatua zaidi. Muajiri wake ndiye atakayemhoji mtuhumiwa na si Takukuru. Huku ni kupotezeana muda na kutafuta cheap popularity. Kwa kufanya walivyofanya wanaonekana vindictive badala ya wapigania haki.

Amandla.........
 
Uongozi wa nchi umekosa credibility. Dr. Hosea hana budi kuachishwa kazi kama kamati ya bunge ilivyobainisha ili kazi zifanyike. Sio kwamba wabunge hawataki kuhojiwa au kuchunguzwa. Issue ni kwamba anayewachunguza yuko madarakani kinyume cha sheria. Takukuru inatakiwa iwe nyeupe kama theluji ili iweze kupenya popote bila ya kisingizio chochote. Hata mimi wakija kwangu kujifanya wananichunguza nitawatoa bomba na mshale.

PCCB iko pale ku-serve interest za mafisadi au? Ni kwa nini order ya kuwahoji wabunge imetokea Ikulu? Hawajui kazi zao mpaka wapewe orders? Tunayeyushana tu, wabunge kataeni ujinga ujinga kama huu. Hosea aondolewe, PCCB isafishwe, mafisadi wote washtakiwe - then PCCB safi iendelee na kazi yake ya kuchunguza na kuhoji bila kinyongo, kisasi wala hofu.
 
Hosea hawezi kubanwa wazee hapa midanganyika tunachezewa shere, kama order imetoka ikulu that means kuna watu wanjilinda na richmond jamani,hili linaonekana, sawa posho hizi ukufuatilia ni serikali yoote inafanya the same thing, nakumbuka nilishafanya kazi ya ukaguzi kipind flani, ukifika tu unapewa chakula, hotel, mapokezi 100% na mkiondoka kuna bahasha mbele ya safari utaifungua, hii ikawa ni mazoea yamekuwa tabia sasa!Wizarani mnakaa kikao the same office mnalipana sitting allowance!?one hr meeting?mh? so hapo IKULU wana jambo, kuna vigogo wanafunika kombe mjinga akatize.Nchi hii bado bado ssaaana tuu! long way to go! so tuwatoe tu madarakani ndo deal
 
Kwa kasi hii ya jamaa kukabana koo basi lazima nyumba iungue kwa maji ya moto .Sina comments ila naangalia sarakasi hizi .Ikulu imeamuru kama alivyosema Pinda kuhusu posho ila imeshindwa kuamuru kwenye mambo mengine ?
Hizi sarakasi zinatia Kinyaa maana wananch wasojua vizuri wanaweza kupotoshwa sana na baadae tukaendelea kuumia hii nchi.
Hivi ni mambo mangapi ya watu wasio katika madaraka yanafichwa na kukumbatiwa, halafu Mengine yanaibuliwa Ghafla na kufanyiwa Kazi. Ila hizi sarakasi zinatupeleka pabaya sana. Sijui hiyo mwakani itakuwaje, maana hadi sasa Maafisa kilimo hwaendi tena mashambani eti mafuta hamna, mishahara inachelewa huku pesa zingine zimefungiwa DECI maamuzi hayapo. Maamuzi ya kuwafunika midomo wabaya wa Ikulu yanafanyika haraka sana, TUTAFIKA?
 
Uongozi wa nchi umekosa credibility. Dr. Hosea hana budi kuachishwa kazi kama kamati ya bunge ilivyobainisha ili kazi zifanyike. Sio kwamba wabunge hawataki kuhojiwa au kuchunguzwa. Issue ni kwamba anayewachunguza yuko madarakani kinyume cha sheria. Takukuru inatakiwa iwe nyeupe kama theluji ili iweze kupenya popote bila ya kisingizio chochote. Hata mimi wakija kwangu kujifanya wananichunguza nitawatoa bomba na mshale.

PCCB iko pale ku-serve interest za mafisadi au? Ni kwa nini order ya kuwahoji wabunge imetokea Ikulu? Hawajui kazi zao mpaka wapewe orders? Tunayeyushana tu, wabunge kataeni ujinga ujinga kama huu. Hosea aondolewe, PCCB isafishwe, mafisadi wote washtakiwe - then PCCB safi iendelee na kazi yake ya kuchunguza na kuhoji bila kinyongo, kisasi wala hofu.
Hivi mwajua kuwa Akina Mwakyembe wana hali mbaya sana, maana Lowasa Bado ni mtu mkubwa nchi hii,- wao wamemtibua adi akajiuzulu, Hosea naye yupo katikati ya JK ndo maana hamtoi- wao wameng'ang'ana kutaka awajibishwe- Pinda naye yupo katika kiti kilekile na hao jamaa, na hawezi kuchmoka.
JE, hAWA AKINA SPIKA NA MWAKYEMBE WATAKUWA WAPI MSIMU UJAO????
 
Uongozi wa nchi umekosa credibility. Dr. Hosea hana budi kuachishwa kazi kama kamati ya bunge ilivyobainisha ili kazi zifanyike. Sio kwamba wabunge hawataki kuhojiwa au kuchunguzwa. Issue ni kwamba anayewachunguza yuko madarakani kinyume cha sheria. Takukuru inatakiwa iwe nyeupe kama theluji ili iweze kupenya popote bila ya kisingizio chochote. Hata mimi wakija kwangu kujifanya wananichunguza nitawatoa bomba na mshale.

PCCB iko pale ku-serve interest za mafisadi au? Ni kwa nini order ya kuwahoji wabunge imetokea Ikulu? Hawajui kazi zao mpaka wapewe orders? Tunayeyushana tu, wabunge kataeni ujinga ujinga kama huu. Hosea aondolewe, PCCB isafishwe, mafisadi wote washtakiwe - then PCCB safi iendelee na kazi yake ya kuchunguza na kuhoji bila kinyongo, kisasi wala hofu.

kWAKWELI MKUU HAPA SINA LA KUONGEZA HII IKULU Imekosa kazi na takukuru ni walewale wala si chombo kama kinavyotajwa. Ni uozo mtupu. HOSEA Kalindwa sana hivyo hajui hata kazi ya mwezi ujao ni ipi adi aambiwe. Docta mzima! Namsifu Mwakyembe ni Critical thinker. Watu inabidi tuwe tunahoji kabla ya kukubalitu eti hili latoka IKULU.
 
Hivi mwajua kuwa Akina Mwakyembe wana hali mbaya sana, maana Lowasa Bado ni mtu mkubwa nchi hii,- wao wamemtibua adi akajiuzulu, Hosea naye yupo katikati ya JK ndo maana hamtoi- wao wameng'ang'ana kutaka awajibishwe- Pinda naye yupo katika kiti kilekile na hao jamaa, na hawezi kuchmoka.
JE, hAWA AKINA SPIKA NA MWAKYEMBE WATAKUWA WAPI MSIMU UJAO????

wananchi tutawachagua, acha woga wewe,huo ni mpambano mazee
 
Back
Top Bottom