Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,268
- 33,041
NA SULEIMAN JONGO
KADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), mkoani Arusha, Daniel ole Porokwa, aliyetangaza nia ya kuwania ubunge Monduli katika uchaguzi mkuu wa Oktoba, mwaka huu, amejiondoa kwenye kinyang'anyiro hicho. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam jana, Porokwa alisema amefikia uamuzi huo baada ya kushauriwa na wazee.
Kwa mujibu wa Porokwa, wazee wamemshauri asipambane na mbunge wa sasa wa jimbo hilo, Edward Lowassa, ambaye pia aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kwa kuwa ni kiongozi mkuu wa kimila. Porokwa alisema baada ya kutangaza nia ya kuwania ubunge katika jimbo hilo, alikwenda jimboni kuona jinsi wapiga kura walivyopokea kauli yake, ndipo alipopata maombi ya kumtaka asubiri.
Alisema akiwa katika ziara hiyo, alifuatwa na viongozi wa kimila wa Kimasai, ambao walimshauri asitishe uamuzi wa kugombea ubunge katika jimbo hilo kwa sasa na kumpa Lowassa nafasi ya kumalizia miaka mitano ijayo.
"Baada ya kuutafakari kwa kina ushauri huo ambao nilipewa na viongozi wa kimila na kushauriana na familia na marafiki zangu, nimeamua kwa moyo mweupe kusitisha uamuzi wa kugombea," alisema Porokwa.
Alisema pia alifikia uamuzi huo baada ya kutambua ukweli kwamba, Lowassa ndiye kiongozi mkuu wa kimila wa wazee wa Kimasai (Malaigwanani), hivyo kupambana naye ni kitendo kisichofaa.
Porokwa alisema licha ya kutumia haki yake ya kikatiba kutangaza nia, ni ukweli usiopingika kuwa, chini ya Lowassa jimbo hilo limepiga hatua kimaendeleo na kwamba, safari hii ndiyo itakuwa ngwe yake ya mwisho.
"Natambua yatasemwa mengi kutokana na kujiengua, kwani hata nilipotangaza nia wapo waliosema nimefanya hivyo kwa kutumwa na wapinzani wa Lowassa kisiasa. Nimefanya hivyo bila shinikizo la mtu yeyote," alisema.
Porokwa akacha kumvaa Lowassa
KADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), mkoani Arusha, Daniel ole Porokwa, aliyetangaza nia ya kuwania ubunge Monduli katika uchaguzi mkuu wa Oktoba, mwaka huu, amejiondoa kwenye kinyang'anyiro hicho. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam jana, Porokwa alisema amefikia uamuzi huo baada ya kushauriwa na wazee.
Kwa mujibu wa Porokwa, wazee wamemshauri asipambane na mbunge wa sasa wa jimbo hilo, Edward Lowassa, ambaye pia aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kwa kuwa ni kiongozi mkuu wa kimila. Porokwa alisema baada ya kutangaza nia ya kuwania ubunge katika jimbo hilo, alikwenda jimboni kuona jinsi wapiga kura walivyopokea kauli yake, ndipo alipopata maombi ya kumtaka asubiri.
Alisema akiwa katika ziara hiyo, alifuatwa na viongozi wa kimila wa Kimasai, ambao walimshauri asitishe uamuzi wa kugombea ubunge katika jimbo hilo kwa sasa na kumpa Lowassa nafasi ya kumalizia miaka mitano ijayo.
"Baada ya kuutafakari kwa kina ushauri huo ambao nilipewa na viongozi wa kimila na kushauriana na familia na marafiki zangu, nimeamua kwa moyo mweupe kusitisha uamuzi wa kugombea," alisema Porokwa.
Alisema pia alifikia uamuzi huo baada ya kutambua ukweli kwamba, Lowassa ndiye kiongozi mkuu wa kimila wa wazee wa Kimasai (Malaigwanani), hivyo kupambana naye ni kitendo kisichofaa.
Porokwa alisema licha ya kutumia haki yake ya kikatiba kutangaza nia, ni ukweli usiopingika kuwa, chini ya Lowassa jimbo hilo limepiga hatua kimaendeleo na kwamba, safari hii ndiyo itakuwa ngwe yake ya mwisho.
"Natambua yatasemwa mengi kutokana na kujiengua, kwani hata nilipotangaza nia wapo waliosema nimefanya hivyo kwa kutumwa na wapinzani wa Lowassa kisiasa. Nimefanya hivyo bila shinikizo la mtu yeyote," alisema.
Porokwa akacha kumvaa Lowassa