POPOBAWA ATUA Tena Bongo

Mwiba

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
7,607
1,744
Kuna tetesi kuwa yule Mdudu wa Kipemba ametua kwa mara nyengine katika mitaa ya Bongo ,mwandishi wetu aliekuwa akipita mitaa iliyoathiriwa na kiumbe huyo wa ajabu alikutana na watu tofauti ambao walikuwa na maelezo yanayosababisha athari za mdudu huyo aliyewahi kukatiza mitaa ya bongo kati ya mwaka 2005 na kutesa.
John Kilomwe wa mtaa wa Keko Magurumbasi alisema mwenzao mmoja alieathiriwa na mdudu huyo ilibidi atoe yaliyomkuta baada ya kurudiwa mara tatu na kufanyiwa kitendo cha aibu ,akizidi kusema sababu zilizomfanya ni kukataa kutoa aibu hiyo kwa marafiki zake na kuwaeleza majirani kitendo ambacho alieleza ni lazima baada ya kuhujumiwa upite kwenye mitaa ukiwaeleza watu jambo ambalo alisema hakuweza kulifanya kwa siku za mwanzo na alivyoona dudu hilo halichoki akaona ni bora awaeleze watu na hapo halikumrudia tena.

Na wakazi wa mtaa wa morogoro road wameanza kulala nje huku wakikoka moto ,dawa ambayo walielezwa kuwa inalifanya dudu hilo kuwa na mazingira magumu ya kuvamia mawindo yake ,hadi sasa hakujaelezwa ni kwa sababu gani dudu hilo limehamia katika mitaa ya bongo.
 
Sijuwi wamekerwa nini jamaa zangu mpaka wameanza tena kutembeza bakora.Huyu mdudu bora angelielekeza hujuma zake kwa mafisadi na kuwalazimisha waungame na warejeshe hela za wananchi, la si hivyo awe anawarudia mara kwa mara. Ingekuwa safi kweli kweli
 
hawa ni wajinga wanapaswa kutembelea watu walioiba kuanzia billion moja na kuendelea. au mnasemaje wanajf
 
acheni uchuro wenu......mwiba jamaa yako ndio wale wakina mark mosha hakua cha popo bawa..
 
Kuna tetesi kuwa yule Mdudu wa Kipemba ametua kwa mara nyengine katika mitaa ya Bongo ,mwandishi wetu aliekuwa akipita mitaa iliyoathiriwa na kiumbe huyo wa ajabu alikutana na watu tofauti ambao walikuwa na maelezo yanayosababisha athari za mdudu huyo aliyewahi kukatiza mitaa ya bongo kati ya mwaka 2005 na kutesa.
John Kilomwe wa mtaa wa Keko Magurumbasi alisema mwenzao mmoja alieathiriwa na mdudu huyo ilibidi atoe yaliyomkuta baada ya kurudiwa mara tatu na kufanyiwa kitendo cha aibu ,akizidi kusema sababu zilizomfanya ni kukataa kutoa aibu hiyo kwa marafiki zake na kuwaeleza majirani kitendo ambacho alieleza ni lazima baada ya kuhujumiwa upite kwenye mitaa ukiwaeleza watu jambo ambalo alisema hakuweza kulifanya kwa siku za mwanzo na alivyoona dudu hilo halichoki akaona ni bora awaeleze watu na hapo halikumrudia tena.

Na wakazi wa mtaa wa morogoro road wameanza kulala nje huku wakikoka moto ,dawa ambayo walielezwa kuwa inalifanya dudu hilo kuwa na mazingira magumu ya kuvamia mawindo yake ,hadi sasa hakujaelezwa ni kwa sababu gani dudu hilo limehamia katika mitaa ya bongo.

Hivi huyu popobawa haogopi ukimwi?Au haumhusu yeye?Au pengine anaueneza?Just thinking aloud.....
 
Back
Top Bottom