Majambazi NMB Temeke yanaswa
Yumo askari wa JWTZ kikosi cha Mgulani
na Sophia Maghembe
SIKU chache baada ya Jeshi la Polisi nchini kutangaza donge la sh milioni 5 kwa watakaofanikisha kutiwa mbaroni kwa majambazi waliovamia Benki ya Taifa ya Microfinace (NMB), tawi la Temeke, jijini Dar es Salaam, tayari watuhumiwa 13 wamekamatwa kwa nyakati tofauti.
Akizungumza jana na waandishi wa habari ofisini kwake, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi, Suleiman Kova alisema, wamefanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao, akiwemo askari wa Jeshi la Wananchi (JWTZ). Watuhumiwa hao wamekamatwa wakiwa na magari manane pamoja na bunduki mbili.
Aliongeza kuwa, walikuwa na bastola moja na SMG iliyoporwa kwa polisi mmoja siku ya tukio.
Kova aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni askari wa JWTZ SGT Mathew (42), mwenye namba MT 55935, mkazi wa Kibaha, Musa Abdallah (30), mkazi wa Yombo Buza jijini Dar es Salaam na Obadia Gabriel (23) waliokufa katika mapambano na polisi wakati wakijihami.
Wengine waliokamatwa ni Antony Jeremia (30), mkazi wa Dodoma, Issack Swai, maarufu kama Fataki (23), Deogratus Masawe (30) ambao ni wakazi wa Moshi, Salum Yasin maarufu kama Jibaba (28), Yusuf Rajabu (44), Boniface Joseph (34), Japo Salimu (27) na Saidi Hamisi (30), wote wakazi wa jijini Dar es Salaam.
Aliongeza kuwa, watuhumiwa wawili ambao hakuwataja kwa majina kwa sababu za kiupelelezi, mmoja yupo Arusha na mwingine Kigoma.
Wengine wawili wapo Kituo cha Polisi Kati jijini Dar es Salaam ambapo magari yote yatafikishwa jijini Dar es Salaam kwa utambuzi kujua wamiliki wake halali.
Alisema watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani kujibu mashitaka yanayowakabili, na wengine wawili ambao hawajatambulika, watatambuliwa hivi karibuni katika gwaride la utambulisho baada ya upelelezi kukamilika.
Katika tukio hilo, majambazi saba walivamia benki hiyo na kurusha mabomu matatu ya kutupwa kwa mkono na kuua mlinzi wa kampuni binafsi ya ulinzi, Seif Mwikwike, kujeruhi wengine wanne na kupora sh milioni 60.
Source: Tanzania Daima
Yumo askari wa JWTZ kikosi cha Mgulani
na Sophia Maghembe
SIKU chache baada ya Jeshi la Polisi nchini kutangaza donge la sh milioni 5 kwa watakaofanikisha kutiwa mbaroni kwa majambazi waliovamia Benki ya Taifa ya Microfinace (NMB), tawi la Temeke, jijini Dar es Salaam, tayari watuhumiwa 13 wamekamatwa kwa nyakati tofauti.
Akizungumza jana na waandishi wa habari ofisini kwake, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi, Suleiman Kova alisema, wamefanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao, akiwemo askari wa Jeshi la Wananchi (JWTZ). Watuhumiwa hao wamekamatwa wakiwa na magari manane pamoja na bunduki mbili.
Aliongeza kuwa, walikuwa na bastola moja na SMG iliyoporwa kwa polisi mmoja siku ya tukio.
Kova aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni askari wa JWTZ SGT Mathew (42), mwenye namba MT 55935, mkazi wa Kibaha, Musa Abdallah (30), mkazi wa Yombo Buza jijini Dar es Salaam na Obadia Gabriel (23) waliokufa katika mapambano na polisi wakati wakijihami.
Wengine waliokamatwa ni Antony Jeremia (30), mkazi wa Dodoma, Issack Swai, maarufu kama Fataki (23), Deogratus Masawe (30) ambao ni wakazi wa Moshi, Salum Yasin maarufu kama Jibaba (28), Yusuf Rajabu (44), Boniface Joseph (34), Japo Salimu (27) na Saidi Hamisi (30), wote wakazi wa jijini Dar es Salaam.
Aliongeza kuwa, watuhumiwa wawili ambao hakuwataja kwa majina kwa sababu za kiupelelezi, mmoja yupo Arusha na mwingine Kigoma.
Wengine wawili wapo Kituo cha Polisi Kati jijini Dar es Salaam ambapo magari yote yatafikishwa jijini Dar es Salaam kwa utambuzi kujua wamiliki wake halali.
Alisema watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani kujibu mashitaka yanayowakabili, na wengine wawili ambao hawajatambulika, watatambuliwa hivi karibuni katika gwaride la utambulisho baada ya upelelezi kukamilika.
Katika tukio hilo, majambazi saba walivamia benki hiyo na kurusha mabomu matatu ya kutupwa kwa mkono na kuua mlinzi wa kampuni binafsi ya ulinzi, Seif Mwikwike, kujeruhi wengine wanne na kupora sh milioni 60.
Source: Tanzania Daima