Pombe na sigara vyaleta mtafaruku katika ndoa...

Kashaijabutege

JF-Expert Member
Oct 20, 2010
2,696
740
Kuna rafiki yangu kaniambia kuwa mkewe amemuomba watengane vitanda kwa kuwa mama hataki harufu ya pombe na sigara. Rafiki yangu hataki kufanya hivyo kwa kudai ndoa ni kuvumiliana; na zaidi kuwa walipooana miaka 10 iliyopita pombe na sigara halikuwa tatizo; isipokuwa kuanzia mwaka jana ambapo mkewe alimpokea Bwana Yesu na kuyaacha ya kale. Rafiki yangu anasema yuko tayari kuoa mwanamke mwingine badala ya kuacha mazoea yake au kulala vitanda viwili wakiwa wanandoa.

Mnawashaurije wanandoa hawa?
 
Huwezi kuwatumikia mabwana wawili kwa wakati mmoja!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
basi mshauri aache sigara....pombe inavumilika kidogo....khaaaa
 
Inabidi na huyu mwanaume ampokee bwana ni kweli harufu ya pombe na sigara ni kero kama wewe si mtumiaji
 
Kuna rafiki yangu kaniambia kuwa mkewe amemuomba watengane vitanda kwa kuwa mama hataki harufu ya pombe na sigara. Rafiki yangu hataki kufanya hivyo kwa kudai ndoa ni kuvumiliana; na zaidi kuwa walipooana miaka 10 iliyopita pombe na sigara halikuwa tatizo; isipokuwa kuanzia mwaka jana ambapo mkewe alimpokea Bwana Yesu na kuyaacha ya kale. Rafiki yangu anasema yuko tayari kuoa mwanamke mwingine badala ya kuacha mazoea yake au kulala vitanda viwili wakiwa wanandoa.

Mnawashaurije wanandoa hawa?





Napata mashaka sana na uamzi wa kutengana vitanda! Kama mama amempokea Bwana Yesu, abebe mzigo wa maombi ili mume wake naye abadilike. Fikiria hivi:

Kabla mama hajampokea Bwana Yesu ==>> ndoa haina matatizo
Mama kampokea Bwana Yesu ==>> anataka watengane vitanda na mumewe eti kwa kuwa mumewe bado ni mtu wa sigara+pombe

Huyu mwanamume ambaye hajampokea Yesu, si atakuwa na mashaka ya kumpokea Yesu kwa kuzingatia hayo matokeo?? Anajifunza nini juu ya Yesu? Hii si ni sawa na kulifanya jina la Yesu litukanwe?

Huyo mama kama kweli kampokea Bwana Yesu na akayaacha ya kale; anyenyekee, aongeze upendo kwa mume wake, amwombee kwa dhati sana mume wake. Ageuke kabisa 180 degrees kumwelekea Yesu, na awe anamshirikisha mume wake hatua kwa hatua katika kujifunza neno la Mungu. Naamini kabisa kumpokea Bwana Yesu siyo sababu ya kutengana vitanda - hii ni kinyume na haipendezi kabisa. Mungu anakuchukia kuachana.
 
Back
Top Bottom