Polisi yawasaka wahariri wa gazeti la Mawio

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,172
23,975
Magazeti yanahabarisha, Jeshi la Polisi linawasaka wahariri wa gazeti la Mawio kutokana na habari mbali mbali ambazo wamekuwa wakizichapisha.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Siro alisema wahariri hao wanatafutwa kwa ajiri ya kusaidia uchunguzi unaofanyika kuhusu habari mbali mbali walizokuwa wakiziandika ambazo zina utata.

Kamanda Siro amesema taarifa kamili kuhusu msako wa wahariri wa Mawio itatolewa leo.

12540337_1024777137586744_1175433069_n.jpg


Wakati huo huo, Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amelifungia maisha Gazeti la Mawio kutokana na kushindwa kujirekebisha katika uandishi wa habari ambao unachonganisha jamii, uchochezi na kuhatarisha amani ya wananchi na nchi kwa ujumla.

Hii hatua imekuja baada ya kuandikiwa barua mara nane na msajiri wa Magazeti nchini kuanzia Juni 2013 mpaka January 2016 ya kuwataka wajirekebishe lakini wamekaidi na kudharau.

Uamuzi huu umetolewa kwa mujibu wa sheria ya Magazeti Sura 229, kifungu cha 25(1) na pia kwa mujibu wa sheria ya mawasiliano ya kielektroniki na posta Sura ya 306.

Nape ametolea mfano wa magazeti mengine mengi kama Mwananchi, Mtanzania, Mzalendo ambayo kila yanapokumbushwa wajibu wao na msajiri wa magazeti huchukua jukumu la kujirekebisha.

VIDEO:
 
hii nchi ya ajabu simuwafungulia kesi mahakamani waziri anakuwa hakimu wa uhuru wa vyombo vya habari acheni mahakama ifanyekazi yake,kubenea atawahenyesha sana tena yupo bungeni si alimwagiwa tindikali unatarajia aandike ccm oye
Uhuru usio na mipaka ni uvunjaji wa sheria........

Hata kwenu baba yako alikupa uhuru wa kufanya utakalo lkn ilikua ni marufuku kurudi usiku wa manane na pia ilikua ni lazima muda wa kula uwe nyumban

Mbona hukuwahi kumuambia baba yako anakunyima uhuru??

Changia ila pia kamba ya uzalendo uwe umeikamata, usichangie kama ntarahamwe ambao hawana uchungu na nchi yao
 
hii nchi ya ajabu simuwafungulia kesi mahakamani waziri anakuwa hakimu wa uhuru wa vyombo vya habari acheni mahakama ifanyekazi yake,kubenea atawahenyesha sana tena yupo bungeni si alimwagiwa tindikali unatarajia aandike ccm oye
Ni kweli hii ni nchi ya ajabu kwa sababu imeweza mpaka kukupa uhuru wa kuandika hata andiko lenye fikra za kijinga, kipumbavu na uchochezi!

Sheria za nchi hazibadilishwi kwenye keyboard/keypad! Mwambia Kubenea akakusaidie kubadilisha sheria ya uhuru wa vyombo vya habari!

Kwa kukusaidia, Bunge ni sehemu ya kutunga sheria na siyo sehemu ya kuhenyesha watu!

Kazi ya kuhenyesha watu inafanywa na Magereza!
 
Ni mkakati wa Serikali ya Chama Cha Majipu(CCM)kujaribu kuwanyamanzisha waandishi makini ili wabaki wale wanaokesha kwenye mageti ya Wizara na Ikulu ili kupiga picha na kuripoti ziara za kustukiza.

Ni aibu kwa Serikali na vibaraka wake,Wanashindwa kumkamata Jecha na kundi lake la mahafidhina wa ccm,wanakimbizana na Gazeti.Kwani serikali ina nini cha siri ambacho inahofia Gazeti la mawio lingekianika hadharani?

Serikali makini inayoendeshwa kwa kufuata Sheria,kamwe haikimbizani na kivuli chake.Genge la wapigadili lililojivika mwamvuli wa serikali ndiyo pekee linaloweza kuruka unyasi likidhani limekutana na joka la makengeza.

Bahati mbaya kwa serikali na wakataviuno wote waitikiao pambio zake,hakuna hata moja lililosirini ambalo halitajulikana kwa Umma.Wale waliotuambia kwamba watalala usingizi wa pono eti kwa Sababu wamemuweka mtu wao,walijidanganya.Bado kitambo kidogo matendo yao ya jinsi walivyolifukarisha Taifa hili yatawekwa dhahiri.Hapo ndipo itakapokuwa fedheha kwao,kwani hata ndege wa angani watashiriki kuwazomea.
 
Back
Top Bottom