Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,138
NINI MAONI YAKO?
Moses Mashalla, Arusha
JESHI la Polisi Mkoani Arusha limeendesha operesheni ya kukamata dawa za kulevya aina ya bangi wilayani Arumeru mkoani Arusha na kufanikiwa kukamata magunia 64 ya bangi ambapo kila gunia moja lina zaidi ya kilo 100 za bangi iliyohifadhiwa.
Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake Kaimu Kamanda wa jeshi hilo ambaye pia ni Mkuu wa upelelezi mjini hapa, Leonard Paul alisema bangi hiyo ilikamatwa katika vijiji viwili tofauti vya Kisimiri Juu na Lesenoni wilayani Arumeru.
Alisema operesheni hiyo ilianza juzi saa 7:00 mchana na kumalizika saa 2:30 usiku wa kuamkia jana ambapo jeshi hilo lilikamata magunia hayo yaliyokuwa yamehifadhiwa katika nyumba za watu mbaimbali kijijini hapo humo.
Kaimu kamanda huyo alibainisha kwamba magunia hayo ya bangi yalikuwa mbioni kusafirishwa kuelekea katika nchi za jirani na kusema katika operesheni hiyo jeshi hilo
halikufanikiwa kumkamata mhusika yoyote katika tukio hilo.
"Magunia hayo ya bangi yalikuwa yamehifadhiwa majumbani mwa watu katika vijiji hivyo hata hivyo tumebaini kwamba bangi hiyo ilikuwa mbioni kusafirishwa kuelekea nchi za jirani," alisema Leonard.
Akizungumzia changamoto katika operesheni hiyo, Leornad alisema polisi haikifanikiwa kuwakamata wahusika kutokana na wakazi wengi kuyakimbia makazi yao mara baada ya kubaini polisi kuanza operesheni hiyo.
Hata hivyo, alisema kwa sasa bangi hiyo imehifadhiwa katika chumba maalumu katika kituo kikuu cha polisi kati ikisubiri kuteketezwa huku mkakati uliopo sasa ukiwa kuwatafuta wahusika wake.
Katika tukio jingine jeshi hilo hilo limefanikiwa kuteketeza mashamba mawili ya mirungi yaliyopo katika kijiji cha Losirwa wilayani Longido . Kaimu kamanda huyo aliwaambia waandishi wa habari kwamba mashamba hayo yaliteketezwa katika operesheni iliyofanyika juzi wilayani humo ambapo mbali na hayo jeshi lake lilifanikiwa kuwakamata watuhumiwa wawili wamiliki wa mashamba hayo.
Moses Mashalla, Arusha
JESHI la Polisi Mkoani Arusha limeendesha operesheni ya kukamata dawa za kulevya aina ya bangi wilayani Arumeru mkoani Arusha na kufanikiwa kukamata magunia 64 ya bangi ambapo kila gunia moja lina zaidi ya kilo 100 za bangi iliyohifadhiwa.
Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake Kaimu Kamanda wa jeshi hilo ambaye pia ni Mkuu wa upelelezi mjini hapa, Leonard Paul alisema bangi hiyo ilikamatwa katika vijiji viwili tofauti vya Kisimiri Juu na Lesenoni wilayani Arumeru.
Alisema operesheni hiyo ilianza juzi saa 7:00 mchana na kumalizika saa 2:30 usiku wa kuamkia jana ambapo jeshi hilo lilikamata magunia hayo yaliyokuwa yamehifadhiwa katika nyumba za watu mbaimbali kijijini hapo humo.
Kaimu kamanda huyo alibainisha kwamba magunia hayo ya bangi yalikuwa mbioni kusafirishwa kuelekea katika nchi za jirani na kusema katika operesheni hiyo jeshi hilo
halikufanikiwa kumkamata mhusika yoyote katika tukio hilo.
"Magunia hayo ya bangi yalikuwa yamehifadhiwa majumbani mwa watu katika vijiji hivyo hata hivyo tumebaini kwamba bangi hiyo ilikuwa mbioni kusafirishwa kuelekea nchi za jirani," alisema Leonard.
Akizungumzia changamoto katika operesheni hiyo, Leornad alisema polisi haikifanikiwa kuwakamata wahusika kutokana na wakazi wengi kuyakimbia makazi yao mara baada ya kubaini polisi kuanza operesheni hiyo.
Hata hivyo, alisema kwa sasa bangi hiyo imehifadhiwa katika chumba maalumu katika kituo kikuu cha polisi kati ikisubiri kuteketezwa huku mkakati uliopo sasa ukiwa kuwatafuta wahusika wake.
Katika tukio jingine jeshi hilo hilo limefanikiwa kuteketeza mashamba mawili ya mirungi yaliyopo katika kijiji cha Losirwa wilayani Longido . Kaimu kamanda huyo aliwaambia waandishi wa habari kwamba mashamba hayo yaliteketezwa katika operesheni iliyofanyika juzi wilayani humo ambapo mbali na hayo jeshi lake lilifanikiwa kuwakamata watuhumiwa wawili wamiliki wa mashamba hayo.