Polisi wazima mapokezi ya Ndugulile

Huyu Ndugulile hajui analoliongea na siamini kama wapiga kura wake watamuunga mkono katika hili. Lazima atambue kuwa mama Tibaijuka japo yuko CCM ni mtu mabye anakubalika sana katika jamii nzima ya Tanzania na dunia kwa ujumula. Sioni mantiki ya kuzuia mradi ambao umedumu miaka zaidi ya 4 na sas tumepata Jembe, mama Tibaijuka ambaye katumia kila mbinu kukoa mradi ambao ulikuwa unaelekea kufa.

Nina mashaka kwamba huenda Mr.Ndugulile ametumwa na baadhi ya mafisadi wachache walioko huko kigamboni ili waendelee kuuteka na kuutawala mji huu wa Kigamboni kwan wao wameshajinyakulia maeneo kadhaa kwa njia isiyohalali ya kuwaonea wanyonge.

Hujui unachoongelea , huyo mama yako tibaijuka ndio fisadi nambari wani na huyo mpuuzi mwenzake alieanzisha huu mradi.

Kwa taarifa yako wakaazi wa Kigamboni majority labda nikufahamishe 99% HAWAUTAKI huu mradi, sasa sijui wewe umetoa wapi haya majibu! hebu fanyeni kura ya maoni ndio utakapobaini hili.

Tunafahamu kuwa Dar es salaam sasa maeneno yote yameisha, na mawaziri wanazaliwa wapya kila siku, leo tunasikia Kigamboni na Bwagamoyo esho wakizaliwa marais wa kipindi kijacho tutasikia Kongowe, mpak kwendea mbele. tunajua watu wa pwani tunaonewa kila kukicha na kinachotuponza ni bahari.

wameona maeneno yameisha sasa wanataka kuja kuipora Kigamboni wagawane viwanja, tunasema kwa kinywa kipana MRADI HATUUTAKI! mimi ni CCM damu ukiikata damu yangu inatoa chembe chembe za kijani, lakini MRADI HATUUTAKI, na wasipoangalia wasubiri nini kitatokea, wajue kuwa watu wameamka sasa sio enzi za ujima hizi na za nyerere watu wamesoma na wameenda shule na wameelimika.

Mwambie huyo mama yako kama amekutuma kuwa atafute sehemu nyingine ambayo haijaendelezwa akaiendeleze, ameshindwa UN habitat sasa huku anataka kuja kutulezea kitu gani? Alishindwa chiligati akaondoka na yeye mueleze kuwa nae ataondoka , HAPATAJENGEKA!

Mwambie sisi wakaazi wa Kigambni tuna Mwenye Ez Mungu, ambae ndio mmiliki wa ardhi na mbingu na vyote vilivomo, kama wanataka kudhulumu basi yeye mwenye Ardhi yake asubiri atawafanya nini, nakuapia utakuja kukumbuka haya maneno yangu, pale PATAJAA MAJI NA HAPATAJENGEKA! kama huamini sibiri na uone!
 
Mji mpya wa Kigamboni.

Kwa mujibu wa gazeti la mwananchi la Alhamis Julai 12,2012 uk.1 unamuonesha Prof Tibaijuka akiwasilisha bajeti ya Wizara yake ambapo zaidi nusu ya bajeti zilizotengwa kwa ajili ya kuendeleleza mji mpya wa Kigamboni, kwa mantiki hii haikuwa suala la busara kwa Mh.Ndugulile katika jimbo lake la uchaguzi kumpa sifuri (0) Mh.Prof Anna Tibaijuka kwa kazi yake hii nzuri.

Kwa hiyo hii ni ishara tosha kwamba Dr. Ndugulile hakuwa na agenda ya msingi. Wakati wabunge wengine wanawalobby mawaziri wapeleke maendeleo jimboni kwao, huyu yuko busy anamfukuza tena kwa matusi Mh.Prof Tibaijuka asilete maendeleo katika jimbo lake.

Kwa hiyo maendeleo ya jimbo hili yakipatikana huyu asijekutudanganya kwamba amechangia chochote.
 
au kuna plan za kutaka kugombea tena?

Kwani kuna ubaya gani akitaka kugombea tena? kuna wabunge wangapi tokea tunatambaa mpaka tunatembea, tunakuwa tumesoma nursery, primary, secondary, university na sasa tupo makazini bado wameng'ang'ana kwenye viti vyao! ajabu gani NDugulile akigombea tena, Mbunge gombea tutakuchagua !
 
Dk. ndungulile uko sahihi 100% wanaokimbia kukutana na wananchi wakiwemo madiwani ndio wana ajenda ya siri. kama mradi ni wa wananchi kwa nini viongozi wote msirudi kwao wananchi? kulikoni madiwani wanaibukia wizarani?
 
Kwa wakazi wa kigamboni baada ya kutoelewana bungeni kati ya mbunge na madiwani walitegemea madiwani kufanya kama wewe mbunge kuitisha vikao na wananchi lakini wamefika kigamboni na kujificha lakini wewe kwa sababu ni mkweli uliona busara kuongea na wananchi.

Taarifa ziko wazi kwamba madiwani walifanya vikao vya ndani kuhujumu mkutano wako.

Kwa kuwa vikao vyao havikufanyika mbinguni bali kwenye jamii tunayoishi hakuna siri.
 
Sheria ya Mipango Miji no.8 ya 2007 inayosimamia mchakato wa Mji Mpya wa Kigamboni imekiukwa. Vipengele vinavyohitaji ushirikishwaji wa wananchi vimerukwa na hivyo kufanya mchakato huu hadi sasa kuwa batili.
Suluhu ni kuanza upya mchakato huu kwa kufuata sheria.

Hongera sana mbunge wewe ni jembe la wanakigamboni
 
Ili kupata ufahamu ni vyema kuisoma na kuielewa sheria ninayoongelea ya Mipango Miji no.8 ya 2007. Kuna vipengele zaidi ya nane vya sheria havikufuatwa. Wananchi wanalalamika hawakushirikishwa kikamilifu na pia mchakato umekuwa ni wa muda mrefu kinyume ya kifungu na 24 cha sheria hii.

well said,

kama tutajadili mradi wa kigamboni kwa kufuata vifungu vya sheria tutakuta mgogoro unakwisha. sheria ni msumeno ndio maana wanaokupinga hawataki kuzungumzia sheria bali njia za mkato. kulikoni?
 
Sheria ya Mipango Miji no.8 ya 2007 inayosimamia mchakato wa Mji Mpya wa Kigamboni imekiukwa. Vipengele vinavyohitaji ushirikishwaji wa wananchi vimerukwa na hivyo kufanya mchakato huu hadi sasa kuwa batili.
Suluhu ni kuanza upya mchakato huu kwa kufuata sheria.

Mheshimiwa, karibu sana kwenye jukwaa hili. Mimi ni mmoja wa watu wanaopendezwa na kazi zako.

Mtu kwao, madiwani wameogopa nini kukushitaki mbunge kwa wananchi kama wewe ulivyokatazwa na polisi kuwashitaki?

Umechelewa sana kujiunga nasi hapa. Karibu sana.
 
Suala la mbagala sio la kigamboni walipopigwa na milipuko ya mabomu ulifanya kazi kubwa, barabara inayojengwa hadi mbagala rangi tatu kwa kiwango cha lami tunaiona.

Tatizo la mbagala haliwezi kukufanya kushindwa kuongelea tatizo la kigamboni.

barabara ya mbagala ilikuwa chini ya kiwango na tulikusikia ukiisemea bungeni.
 
Mji mpya wa Kigamboni.

Kwa mujibu wa gazeti la mwananchi la Alhamis Julai 12,2012 uk.1 unamuonesha Prof Tibaijuka akiwasilisha bajeti ya Wizara yake ambapo zaidinusu ya bajeti zilizotengwa kwa ajili ya kuendeleleza mji mpya wa Kigamboni, kwa mantiki hii haikuwa suala la busara kwa Mh.Ndugulile katika jimbo lake la uchaguzi kumpa sifuri (0) Mh.Prof Anna Tibaijuka kwa kazi yake hii nzuri. Kwa hiyo hii ni ishara tosha kwamba Dr. Ndugulile hakuwa na agenda ya msingi. Wakati wabunge wengine wanawalobby mawaziri wapeleke maendeleo jimboni kwao,huyu yuko busy anamfukuza tena kwa matusi Mh.Prof Tibaijuka asilete maendeleo katika jimbo lake. Kwa hiyo maendeleo ya jimbo hili yakipatikana huyu asijekutudanganya kwamba amechangia chochote.

Kama umetumwa changanya na akili zako.

Ndungulile hapingi mradi wa kigamboni wala hapingi Mama Tiba kutenga fedha hizo anapinga mchakato unaoonyesha kukiuka sheria jambo linalompa hofu mbeleni. Sheria ikikiukwa hasara itakula kwa wananchi ambao ni wakazi wa kigamboni.
 
ili kupata ufahamu ni vyema kuisoma na kuielewa sheria ninayoongelea ya mipango miji no.8 ya 2007. Kuna vipengele zaidi ya nane vya sheria havikufuatwa. Wananchi wanalalamika hawakushirikishwa kikamilifu na pia mchakato umekuwa ni wa muda mrefu kinyume ya kifungu na 24 cha sheria hii.
karibu mbunge jamvini tutetee watu wa kigamboni kwani tunataka kuishi sehemu nzuri tutaishia kuhamishiwa mabwepande sie.
 
Naomba niulize huo mradi Uanze Upya Ili iweje wakati walishatangaza muda mrefu na picha na majina walipita kuangalia majengo.

sheria inasema baada ya tathmini ya kwanza baada ya miezi sita fidia inatakiwa kulipwa. Hii ni kuepusha kupanda kwa gharama mbalimbali eg. gharama za ujenzi zinabadilika kutokana na wakati, ardhi inapanda bei, kuepusha usumbufu kwa wakazi wa eneo la mradi ambao wanasimamisha maendeleo kupisha mradi, nyumba zilizo kwenye mradi hazikopesheki na mabenki nk.

Tathmini ya Kigamboni ilifanyika mwaka 2009 je unapotaka mbunge asiseme kitu una maana ipi?
 
karibu mbunge jamvini ila sera za ccm tutetee watu wa kigamboni kwani tunataka kuishi sehemu nzuri tutaishia kuhamishiwa mabwepande sie.

mwanzoni mradi ulionyesha wananchi hawatahamishwa lakini dalili na ishara zinaonyesha sivyo.
 
images


images





Kiagamboni city itakavyoonekana baada ya ujenzi kukamilika

kila mtu anapenda kigamboni ionekane kama hivyo lakini pia ikiwezekana Tanzania nzima iwe nzuri namna hiyo.

ndungulile anajadili namna ya kelekea kigamboni nzuri hapingi anajadili haki ya wananchi/wakazi wa kigamboni ili kupisha mradi
 
Ili kupata ufahamu ni vyema kuisoma na kuielewa sheria ninayoongelea ya Mipango Miji no.8 ya 2007. Kuna vipengele zaidi ya nane vya sheria havikufuatwa. Wananchi wanalalamika hawakushirikishwa kikamilifu na pia mchakato umekuwa ni wa muda mrefu kinyume ya kifungu na 24 cha sheria hii.
Mh Dr Ndugulile,
Kwanza nakupa pole kwa adhabu uliyopewa na agwe Ndugai. Adhabu hiyo ni adhabu kwa wananchi wa jimbo lako pia. Hivyo Ndugai hawezi kukuppokonya watu wako waliokuchagua.

Pili napenda nikupe pongezi kwa kazi nzuri unayofanya, kuwatetea watu wako wanyonge. Serikali yetu sasa imekuwa kama mtu aliyekula nyama ya mtu, au mtu aliyeonja asali na kuchonga mzinga. Sera za serikali sasa ni kupokonya kile kidogo walicho nacho watu wanyonge na kuwadhulm. Hili ni chukizo hata mbele za Mungu.

Mimi nakutia shime, songa mbele na usisikilize miluzi ya wanufaika wa dhulma, kwani wapo hata hapa JM na watakushambulia kila utowapo maelezo yako. Usitishwe! Wapuuze kama kinyesi tu!

Tuko pamoja sana...
 
Ili kupata ufahamu ni vyema kuisoma na kuielewa sheria ninayoongelea ya Mipango Miji no.8 ya 2007. Kuna vipengele zaidi ya nane vya sheria havikufuatwa. Wananchi wanalalamika hawakushirikishwa kikamilifu na pia mchakato umekuwa ni wa muda mrefu kinyume ya kifungu na 24 cha sheria hii.

kaka bora ungeendelea kula shushu bondeni. Hizi siasa zimekuwa za maji taka siku hizi
 
ndungulile anafanya kazi ya mbunge na madiwani hawafanyi kazi ya diwani.

Wakati ndungulile anakwenda bungeni alipita kwa wananchi (rejea mikutano ya hadhara) na kuomba maoni na ushauri kwa wananchi nini akawasemee bungeni kwa maana hiyo anayosema ndungulile ni maneno ya wakazi wa kigamboni.

Madiwani waliondoka kwa kificho hawakukutana na wananchi lakini walikwenda dodoma kwa mission maalum...

Madiwani kwa madaraka wako chini ya mbunge jimboni inakuwaje wanatoka jimboni bila mbunge kujua wanakutana bungeni? nini siri ya safari yao (madiwani) ambao mbunge hakuijua wala wananchi wa kigamboni?
 
Mh Dr Ndugulile,
Kwanza nakupa pole kwa adhabu uliyopewa na agwe Ndugai. Adhabu hiyo ni adhabu kwa wananchi wa jimbo lako pia. Hivyo Ndugai hawezi kukuppokonya watu wako waliokuchagua.

Pili napenda nikupe pongezi kwa kazi nzuri unayofanya, kuwatetea watu wako wanyonge. Serikali yetu sasa imekuwa kama mtu aliyekula nyama ya mtu, au mtu aliyeonja asali na kuchonga mzinga. Sera za serikali sasa ni kupokonya kile kidogo walicho nacho watu wanyonge na kuwadhulm. Hili ni chukizo hata mbele za Mungu.

Mimi nakutia shime, songa mbele na usisikilize miluzi ya wanufaika wa dhulma, kwani wapo hata hapa JM na watakushambulia kila utowapo maelezo yako. Usitishwe! Wapuuze kama kinyesi tu!

Tuko pamoja sana...

nukuu ya busara,

wapo wanaopindisha hoja kwamba ndungulile anakataa mradi ili tu kukwepa hoja, utawaona wengi nje na ndani ya JF.

kwa suala la kigamboni unakisaidia sana chama chama kuwa imara na kupendwa na wananchi lakini madiwani wanataka chama kichukiwe kwa sababu zao binafsi.
 
Nadhani Katiba itabidi liongelee vizuri sana hili suala la uwezo wa polisi kupiga marufuku mikutano au maandamano ya watu na viongozi wao. Hata sasa sijui utaratibu sahihi ni upi!!, Askari anapewa taarifa tu, na ni jukumu lao kutoa ulinzi au kuepusha lolote linaloweza kuhatarisha amani sio kuzuia mkutano au maandamano. Haya mambo inaonekana kuna mtu tu anaamua kufanya hivyo kwa kuhofia maslahi yake. Tunahitaji kuamka sana kwenye hili.
 
Back
Top Bottom