Polisi wavunja maandamano ya Wanafunzi UDSM; Watawanywa kwa mabomu ya machozi

mkwere anafanya vitu kama mbuni kukitokea tatizo anakimbia au anaficha kichwa ardhini! Hapa nilipo kila siku kuna mgao wa umeme kuanzia juzi wameuongeza tena yaani nina hasira kwa nini cdm au vyama vingine tusiandamane kupinga kutokupatikana kwa umeme? Hakuna umeme, maji ya bomba tushasahau yanavyotoka, bidhaa zote bei juu, elimu inazidi kuporomoka, wazee wa east africa hawalipwi wakati dowans wanataka kulipwa faster, mishahara haiongezwi etc matatizo yako mengi sana nchi hii, kuna watu wanatoa solution kama jinsi ya kupunguza foleni za magari kwa ku built fly over eneo za trafick light na njia za chini lakini hakuna viongozi anaye react. Mpaka watu wagome ndo watawa please hao, then wakitokea wengine wanagoma wakiwa wachache hawasikilizwi. Hivi mkwere & your co mnatutakia nini? Kama hela mnazo maisha ya anasa mnaishi lakini hata kutupa solution za matatizo yetu huwezi? Hivi ukienda ukakopa 2 billion US $ ukaja nazo ukatutengenezea steigler project inayoweza kuzalisha mw 2000 ili tupate umeme wa uhakika, itakuathiri nini ktk anasa zako? Hivi ukimwita Slaa na Mbowe na vichwa vingine mkaunda "think tank" jinsi ya kututoa hapa tulipo ili tusonge mbele itakufanya upungukiwe na nini? Kweli unasema unaanzisha miji ya viwanda wakati umeme hakuna? Watu wa migodi wanatumia ma generator yao wakati tuna eneo lina mw 2000? Hata kama litachukua ten years kuwa ready we will know you have solved the problem. Tuna madini mengi sana ushaenda Zambia ukauliza walifanyaje wakavunja mikataba yenye kodi ya kuwapendelea wawekezaji badala ya wananchi, nenda Botswana kaangalie walivyofanikiwa ktk kuinua pato la nchi kwa kutegemea madini. Kama unawaogopa isije ikawa mambo ya icc kwa nini Zambia waweze sisi tushindwe? Uliunda tume ikakupa majibu lakini wananchi hatuoni kitu. mkwere uwezo wa kututoa hapa tulipo kutupeleka mbele upo na bado ukaendelea na anasa zako, kama huwezi mpe Magufuli awe waziri mkuu kuliko huyo pinda ambaye ni "yes boss" unajua nikitafakari nashangaa ilikuwaje ccm wakakupa u president? Inakuwaje unajibu "hujui kwa nini watanzania ni maskini" hujui! Mi nakushauri weka urafiki pembeni linapokuja swala la taifa, unda "think tank" vikiwemo vichwa vyote Slaa, Mbowe, Magufuli, cuf etc, lets build our tz together.
 
Gari la kumwagia binadamu maji yenye sumu ya kuwasha mwilini. Sumu hiyo inanunuliwa kwa pesa nyingi za kigeni kutoka mataifa ya magharibi na marekani, cha ajabu hao wanaotuuzia hawatumii kabisa sumu hii ila sisi sasa...!

Samahani kukaa sana ughaibuni kunanifanya niwe mgeni na msamiati wa kawaida mtaani.
 
Unasema ulikua Chuo ila nina wasi wasi kama ni pale mlimani. Njia ya haki kwa wanafunzi ni moja tu. MGOMO.
Ukishaitwa mwanafunzi siku zote unaonekana mdogo tu! unaposema kitu bado unaonekana Mdogo.
Miaka yangu yote pale mlimani sijaona haki ikipatikana bila mgomo mkuu!!

MLACHAKE,
Nakubaliana na we kwa % zote,cjawai kuona tatzo limetatuliwa kwa diplomatic pale,mgomo ndo huwa suluwisho,lakin pia si hvyo tu,hata hyo hela kufikia elfu 5 ni kutokana na migomo na maandamano,mfano kuna mwaka kulikua na tatizo la maji udsm,wadau walivumilia siku 3,lakin walipoanza maandamano nyakat za usiku,ilipofika saa 8 usiku yaliletwa,na hadi namalza chuo,kila hall pale main campus lina matank ma 4 ya simtank tena ujazo wa lita elfu 5 hadi kumi,kwa hyo mgomo unasaidia
 
Sikatai nalipa tax ili wanafunzi wapewe mikopo wasome na taskforce ya Tanzania ikakua. Ila naumia pale ambapo tax zangu zikaenda kuilipa DOWANS wakati wahitaji wapo Tanzania na wanataabika. Shule haipandi.

Naumia pia pale ambapo tax zangu zinatumika kununua mabomu ya machozi ili sauti za wanafunzi zisisikike. Ina uma ila ufanyeje?.

Je polisi wamepiga hesabu zipi kuhusu watu waliopo mwenge kituoni wanataka kwenda makazini? Je watu hao wakichukia na wakajiunga na wanafunzi? Haya matatizo ya wanafunzi huko mikoani? Wamefikiria lipi la kuwasaidia. Matatizo haya yapo kotekote.

Kwa Rais kutoa ahadi zisizotekelezeka na zisizoangalia uhalisia wa maisha kwa wanafunzi na wanafunzi kuamini kuwa msaada utatokea serikalini tu. Ila palipo na haki basi hata sauti zao zisikike.
 
Migomo sasa imezidi jamani. Inabidi tufanye mjadala wa kitaifa kujadili suala hili la migomo vyuoni.

hawa wanasiasa uchwara wanataka kuvamia suala la migomo ili kujipatia umaarufu au kuziba udhaifu wa serikali ya chama chao kuongoza nchi hawatusaidii kumaliza migomo zaidi ya kuiendeleza.

Kwa upande mwingine serikali inasuluhisha kiupendeleo, kuna vyuo wanafunzi wakigoma mawaziri wanaenda wengi tena kwa ndege za kukodi na wakati mwingine anaenda waziri mkuu mwenyewe. Vyuo vingine wakigoma wanaachiwa wayamalize wenyewe. Upande mwingine wanafunzi nao wanachangia migomo.

Saikolojia ya migomo niliyoiona mimi wakati niko chuo ni kwamba miezi kama hii wakati wanafunzi wengi wameishiwa boom na masomo yamechanganya sana test zinalia kila siku ya UE ndo inakaribia kumalizia semista halafu akaja mtu akakushawishi kugoma, hata kama ni kwa sababu ndogo kiasi gani unakuta watu wanaingia kugoma haraka sana. Uvumilivu unahitajika kwa upande wa wanafunzi ili pia wasome na kumaliza semista kwa wakati.

Mfano mgomo wa kuongezewa boom kuwa 10,000 ni muhimu lakini hautekelezeki kwa bajeti iliyopo so wangeweka presha kwa serikali ili bajeti ijayo wapewe pesa. Ila kwa ujumla migomo ni mizuri sana kwani inamuonyesha kila mtu kuwa Mkwere ni kiongozi dhaifu kuliko wote waliowahi kuongoza nchi hii, anafikiri kukaa kimya kama kobe itasaidia kumaliza tatizo kumbe ndo linaongezeka.

Sasa hivi utasikia shule za sekondari zinaanza migomo.


Acha upuuzi wa kuandika ujinga,niambie kwa maisha ya sasa unaweza kuishi kwa shillingi 5000.Tuulize sisi wenye watoto tunavyopata shida.

Msiwe mnaongea kwa upeo mdogo mlionao.Kama wako tayari kulipa Dowan maana pesa ipo.
 
Pole sana mjomba jk na kibarua kigumu cha kugeuza bongo kuwa uwanja wa migomo.
 
Mkuu!! Hawajakurupuka! Wasiojua wanaweza kuwaona wahuni na wasiochanganua mambo! Kwa ufupi ni kwamba malalamiko ya kuongeza boom yaliaanza tangu mwaka jana serikali inapuuzia tu!! Iliyokuwa Tahliso ilishapeleka hiki kitu mezani kwa waheshmiwa!


Uncle sawa kabs, lakini kuna kamtego hapo! unajua UE V/S mogomo relationship? frustration na mambo kama hayo, mm naunga mkono kudai haki kwa nguvu pale ninaona sina njia mbadala,!! kama unenisoma pamoja na kuadress ishu ya Shekeli waambatanisha na madai ya tibaya matatizo ya msingi kama kuporomoka kwa maadili ya viongozi, nchi kushindwa kuweka vipaumbele ikiwemo elimu nk. Basi wangegoma leo kuhusu DOWANS kulipwa, Mfumuko wa bei ambao ungeweza kufanyiwa kazi kama serikali ingekuwa makini, serikali kuwajibisha watendaji wabovu nk, halafu baada ta UE wadai hela inayodaiwa

after all 5000 mnasema haitoshi hivi unajua watumishi wanalipwa sh 150,000 per month na wana familia na wanasavaivu, nyie mnaona 5000 ni ndogo, daini kuboreshewa mazingira ya elimu, hostels, maabara, maktaba viendane na viwango vya kimataifa. sasa nyie manadai hela ya kuweka matumboni na kuendea madisco, sisemi wote ila kuna baabdi ya wanafunzi..... think twice
 
maandamano yamefikia wapi wadau tunapenda kujua na hao askari wameshaumiza wangapi


hawa jamaa wana akili sana nawaona wanatembea kila mtu kivyake as if nothing is going on but they have a turget ahead kuwapumbaza polisi njaa.
 
JK hana habari atakuwa bize na toothpick baada ya kula misambusa na chai ya maziwa anaanza kusoma magazeti ya leo ...wala hana habari kabaisa kwamba kuna matatizo ...polisi kama kawaida watasema wana taarifa za kiitelijensia
teh teh teh teh tehhhhhhhhhhhh,,,,,
 
wanataka waendelee kwenda kuchukua dada zetu palee! Ijumaa palee! Waondoke nao palee! Kurudi ni jumatatu palee! Ukiwapa msimbazi palee! Watakuwa hawakubali palee. Hahahahahahahahahah
we nawe chizi au unarap?
 
Uncle sawa kabs, lakini kuna kamtego hapo! unajua UE V/S mogomo relationship? frustration na mambo kama hayo, mm naunga mkono kudai haki kwa nguvu pale ninaona sina njia mbadala,!! kama unenisoma pamoja na kuadress ishu ya Shekeli waambatanisha na madai ya tibaya matatizo ya msingi kama kuporomoka kwa maadili ya viongozi, nchi kushindwa kuweka vipaumbele ikiwemo elimu nk. Basi wangegoma leo kuhusu DOWANS kulipwa, Mfumuko wa bei ambao ungeweza kufanyiwa kazi kama serikali ingekuwa makini, serikali kuwajibisha watendaji wabovu nk, halafu baada ta UE wadai hela inayodaiwa

after all 5000 mnasema haitoshi hivi unajua watumishi wanalipwa sh 150,000 per month na wana familia na wanasavaivu, nyie mnaona 5000 ni ndogo, daini kuboreshewa mazingira ya elimu, hostels, maabara, maktaba viendane na viwango vya kimataifa. sasa nyie manadai hela ya kuweka matumboni na kuendea madisco, sisemi wote ila kuna baabdi ya wanafunzi..... think twice
Mfanyakazi kulipwa 150000 ni kwa sababu ya kukosa muungano. Wafanyakazi ndo chanzo kabisa cha kushuka kwa uchimi wa taifa letu. Watu waliosaida sana katika kutafuta uhuru wa nchi yetu ni wafanyakazi wa kipindi kile, lakini siku hizi wafanyakazi ndo hata hana hili wala lile. Acha wakome tu. Tena wangelipwa chini ya hapo ili wakome kabisa na familia zao, maana ni wazi kabisa mtu anayelipwa 150000 na anamtegemezi mmoja tu lazima mtu huyu atakuwa mwizi ama la atakuwa na madeni kila mahali. Binafsi naomba hali iwe ngumu zaidi hata mara 3 ili watu watumie vichwe vyao.
 
Chadema wanawaharibu hawa watoto. Wameonyesha mfano mbaya wa kuleta chaos zisizo kuwa na tija kwa taifa. Au ndio muendelezo wa kulifanya taifa lisitawalike? Lakini wakiongezewa boom si watakwenda Bils! na wazee wa chama fulani watanufaika? I can smell fish here!!!!
Acha mawazo mafupi ndugu yangu. Si wanafunzi wote wanaenda Bills. Na ni ngumu kuchambua ni yupi anayeenda Bills usimpe na asiyeenda umpe mkopo. Kumbuka hata Mungu huwanyeshea mvua wema na waovu pia. So kama swala ni kuongezewa lazima waongezewe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom