MVUMBUZI
JF-Expert Member
- Jan 8, 2011
- 5,182
- 2,304
Ilikuwa kama sinema ya bure hapa NMB Clock tower jioni hii polisi wawili walipoacha lindo na kutimua mbio live waliposikia sauti za kundi kubwa la vijana waliotokea kwenye mkutano wa Chadema. Vijana hawa zaidi ya 2000 walikuwa wakisukuma gari ya Lema kutokea viwanja vya NMC huku wakiimba"bila Lema patachimbika". Walipofika round about ya clock tower wakawaona polisi waliokuwa pale benk na kupiga kelele haooo!!.Ghafla polisi wale 2 walinyanyuka na silaha zao wakatimua mbio bila kukimbizwa na mpaka naondoka eneo la tukio lindo lilikuwa bado limetelekezwa. Akina mama waliokuwepo eneo hilo walishikilia mbavu zao kwa kicheko kwani hii ni mara ya kwanza kuona polisi wenye silaha wakiwakimbia raia kwa spidi kubwa mithili ya wanariadha.