Polisi wapiga stop maandamano ya wanafunzi

Polisi walimzuia Sharpton kwa kuzingatia kuwa kuandamana wakati watu bado wana majonzi ya kifo cha Sean Bell potentially kuna weza kufanya baadhi yao kumalizia hasira zao kwa raia wengine na/au mali zao. Hii inaeleweka na inakubalika. Mimi napinga flimsy excuses zinazotumika kuzuia maandamano hapa kwetu. Excuses kama hii yaati kwa sababu chombo cha wanafunzi kimesajiliwa kama kampuni na si NGO basi maandamano NO! Excuses kama hizi ambazo wengine wanazitoa, ati wangefuata taratibu na kukaa kwanza na uongozi wa Chuo. Uongozi ambao hata kuwatambua hauwatambui! Mimi sijaona ni namna gani raia mwingine au mali zake zinaweza kuwa "harmed" na maandamano ya hawa wanafunzi. Kuwaambia ati watimize sheria kwanza ni kuwaonea maana hamna jinsi wanaweza kutimiza kama Polisi hawataki hayo maandamano. Kuwaambia ati wangoje mpaka bunge wazibadilishe na kwenyewe ni kuwa disingenious. Ikiwa mtu kama Nyalali aliweza kutaja wazi sheria kibao za kigandamizi na serikali ikampuuza itakuwa hawa? Hapana umefika wa kuwaeleza hao polisi kuwa wao ni watumishi wa wananchi na moja ya wajibu wao ni kulinda uhuru wake wa kueleza kutoridhishwa kwake na jambo lolote.

Amandla......
 
Polisi walimzuia Sharpton kwa kuzingatia kuwa kuandamana wakati watu bado wana majonzi ya kifo cha Sean Bell potentially kuna weza kufanya baadhi yao kumalizia hasira zao kwa raia wengine na/au mali zao. Hii inaeleweka na inakubalika. Mimi napinga flimsy excuses zinazotumika kuzuia maandamano hapa kwetu. Excuses kama hii yaati kwa sababu chombo cha wanafunzi kimesajiliwa kama kampuni na si NGO basi maandamano NO! Excuses kama hizi ambazo wengine wanazitoa, ati wangefuata taratibu na kukaa kwanza na uongozi wa Chuo. Uongozi ambao hata kuwatambua hauwatambui! Mimi sijaona ni namna gani raia mwingine au mali zake zinaweza kuwa "harmed" na maandamano ya hawa wanafunzi. Kuwaambia ati watimize sheria kwanza ni kuwaonea maana hamna jinsi wanaweza kutimiza kama Polisi hawataki hayo maandamano. Kuwaambia ati wangoje mpaka bunge wazibadilishe na kwenyewe ni kuwa disingenious. Ikiwa mtu kama Nyalali aliweza kutaja wazi sheria kibao za kigandamizi na serikali ikampuuza itakuwa hawa? Hapana umefika wa kuwaeleza hao polisi kuwa wao ni watumishi wa wananchi na moja ya wajibu wao ni kulinda uhuru wake wa kueleza kutoridhishwa kwake na jambo lolote.

Amandla......

Sawasawa kabisa fundi hapo tuko pamoja.Hiyo sheria inayotumiwa na polisi wakati wa maandamano sio kwamba polisi wanaombwa kibali cha kuandamana,kuna watu wanachanganya mambo hapo.Polisi wanaombwa kutoa ulinzi kwa waandamanaji sio kutoa kibali cha maandamano.Ndio kusema kuwa kila watu wanapotaka kuandamana wakajisajili kwanza kama NGO ndipo
waandamane?kwani hao TGNP, HAKIELIMU, EDITORS FORUM si wamesajiliwa kama makampuni lakini bado wamekuwa wanaandaa maandamano na wanakubaliwa.Watanzania wenzangu niwakumbushe kuwa wakati TAHLISO ikiwa ndio kwanza imeanzishwa June 2003 iliweza kuitisha maandamano ya kupinga sheria ya kuanzishwa kwa bodi ya mikopo na tuliruhusiwa kuandamana.Tulipopeleka barua kwa afande tiba alichofanya ni kutuita ofisini kwake tukazungumza nae hatimaye tukaruhusiwa kuandamana, suala la usajili halikuwa kitu cha lazima na sheria iliyotumiwa na afande tiba ndo hiyo hiyo inayompa shida kova.Kwahiyo kilicho dhahiri hapa ni kwamba aidha kova anatekeleza matakwa ya wakubwa ama hajui kutafsiri sheria.Hata kama hawa wanafunzi watafanya kila wanaloambiwa na polisi ili waruhusiwe kuandamana, alimuradi hakuna nia ya kuwaruhusu, hawatakubaliwa kamwe kuandamana!!!
ccm na serikali yake wanajua fika kuwa wameichezea vya kutosha elimu ya juu na wanafunzi wakiandamana watafunua mambo mengi hivyo ujumbe utawafikia watanzania na kwahiyo uchaguzi wa 2010 utakuwa mgumu zaidi kwao.Kilichofanyika hapa ni siasa hakuna cha sheria.
Halafu nimkumbushe FMes na wanaowaza kama yeye kwamba atambue kuwa sasahivi watawala wa vyuo sashivi ni mawakala wa CCM na sio wanataaluma kama tunavyowaona.Wala hawana sababu ya kukaa na kujadiliana na wanafunzi na hata wakikaa kujadiliana na wanafunzi ni kuwaghiribu tu hakuna utekelezaji wowowte labda liwe ni suala dogo sana.Nawakumbusha mkaitafute ile ripoti ya kamati ya mama sinare iliyochunguza vyanzo na sababu za migomo ya vyuo vya elimu ya juu muone mapungufu waliyoyabaini kuanzia wizarani hadi vyuoni.Kisha mjisomee mapendekezo waliyoyatoa muone kama ni mangapi serikali imeyatekeleza.Na kwakuwa watu wengi tunautazama huumvutano wa wanafunzi na serikali katika mtazamo wa kisiasa na siasa zetu za bongo ni uadui, ndio maana wengi wanawanyooshea kidole wanafunzi kwa kuwa tu wamesikia kuwa CHADEMA ilihusika kuwachochea wanafunzi
.
 
--------------------------------------------------------------------------------

1.
Polisi walimzuia Sharpton kwa kuzingatia kuwa kuandamana wakati watu bado wana majonzi ya kifo cha Sean Bell potentially kuna weza kufanya baadhi yao kumalizia hasira zao kwa raia wengine na/au mali zao. Hii inaeleweka na inakubalika.

- You see, sasa tupo pamoja hapa ni kwamba mimi ninachosema ndio hasa unachokubali hapa kwamba polisi sio wetu tu hata wa US huwa wana haki kisheria kukubali au kukataa kutoa kibali cha maandamano,

- kuhusu sababu za kukubali au kukataa kwao yani polisi hiyo ni another subject by itself kwa ajili ya thread yake kamili, lakini kimsingi tukubalinae kua polisi wana haki kisheria kukataa au kukubali kutoa kibali cha maandamano, iwe bongo au majuu hili linaeleweka na kukubalika.

- Sasa tunaweza kuanzisha a new debate kuhusu sababu, binafsi I am not interested na hii subject maana najua kutakua na ishus ambazo sio profitable kwa wananchi na hasa taifa. Mimi huwa sina uhaklika na hawa wanafunzi hasa pale walipotishia nyau halafu wakavaaa uniform za CCM na kuhutubiwa na rais I was done na hizi type of ishus za wanafunzi.

Ingawa kimsingi niwe mkweli tu naipongeza sana serikali yetu on uhuru wa kuongea na maoni, maana looking back tulikotoka na hii ishu as a nation na tulipo sasa, Mungu Aibariki Tu Tanzania.

Thanxs!
 
UDSM ni mpasuko

Habari Zinazoshabihiana
• Mrema aipa dole CCM kusuluhishana na CUF 24.12.2006 [Soma]
• Mpasuko wa kisiasa Z'bar wawa mwiba 27.07.2006 [Soma]
• 'Hali ya Zanzibar kisiasa si sawa na ya Kenya' 14.04.2008 [Soma]

*Uongozi wawapuuza maprofesa wake
*Mhadhiri amdhamini Rais DARUSO
*Polisi wapiga marufuku maandamano

Na Joyce Magoti

SIKU moja baada ya Umoja wa Wahadhiri Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDASA) kuutaka uongozi wa chuo hicho kuwarejesha wanafunzi wote chuoni kwa ajili ya kuendelea na masomo, uongozi wa chuo hicho umepuuza shinikizo hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Huduma za Jamii wa UDSM, Prof. Amandina Lihamba alisema uongozi wa chuo hicho utaendelea na msimamo wake wa kuwarudisha chuoni hapo wanafunzi wale tu watakaotimiza masharti ya udahili.

"Sisi hatuwezi kusema chochote kuhusu kauli ya UDASA lakini msimamo wetu ni ule ule wa kuwadahili na kuwarejesha chuoni wale tu watakaotimiza masharti ya udahili labda muende mkawaulize wao kuwa wanasemaje kuhusu hili," alisema Prof. Lihamba.

Kuhusu kuwepo ulinzi mkali uliopo chuoni hapo bila ya kuwa na hali yoyote ya vurugu pamoja na kuzuiwa njia inayotumiwa na wakazi wa jirani na eneo hilo, Prof Lihamba alisema ulinzi huo ni lazima uwepo kutokana na kuwepo kwa kauli za uchochozi na uvunjifu wa amani.

Katika tamko lao juzi UDASA walitaka uongozi wa chuo hicho na Serikali kwa ujumla kufanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa katika Kamati iliyoundwa mwaka jana na wahadhiri hao ambayo ilibainisha chanzo cha migogoro hiyo na pia namna bora ya utekelezaji wa Sera ya Elimu ya Juu nchini.

Pamoja na taarifa hiyo rasmi ya UDASA kushinikiza wanafunzi wote warejeshwe, kumekuwepo na tetesi za kuwepo mgomo wa wahadhiri hao, hata hivyo hakuna upande huru uliothibitisha habari hizo.

Naye Peter Masangwa na Grace Ndossa wanaripoti kutoka Dar es Salaam kuwa, Jeshi la Polisi nchini limezuia maandamano ya wanafunzi wa elimu ya juu yaliyokuwa yafanyike Dar es Salaam leo, chini ya Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP).

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam, Bw. Suleiman Kova wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandamano hayo.

Bw. Kova alisema kuwa TSNP si asasi isiyo ya kiserikali kama ilivyojieleza katika barua ya kuomba kuandaa maandamano hayo bali ni kampuni iliyosajiliwa kwa jina la Tanzania Students Networking Programme Limited yenye namba ya usajili SO 42386 tangu Oktoba 23 mwaka 2001.

''Sheria ya Asasi zisizo za Kiserikali ya mwaka 2002, Sehemu ya Tatu kifungu cha 11(3) inaeleza kwamba asasi yoyote lazima ipate hati maalumu ya usajili kabla haijaanza kufanya kazi,'' alisema Bw. Kova na kusisitiza kuwa shirikisho hilo la wanafunzi halikusajiliwa kwa mujibu wa sheria hiyo.

Pia alieleza sababu nyingine ya kutoruhusu maandamano hayo ni kutokana na haja ya kutaka udahili unaendelea kuwa wa amani na utulivu.

Katika hatua nyingine inayoonesha kuwa baadhi ya wahadhiri chuoni hapo hawakufurahishwa na hatua mbalimbali za uongozi wa chuo, Mwandishi Grace Michael anaripoti kuwa mmoja wa wahadhiri chuoni hapo, Dkt. Azavel Lwaitama ameibuka na kumdhamini Rais wa Serikali ya Wanafunzi (DARUSO), Bw. Antony Machibya ambaye alikuwa anasota rumande kutokana na kukosa dhamana.

Mbali na Bw. Machibya kudhaminiwa, wanafunzi wengine ambao walikuwa wakisota rumande nao wamekamilisha masharti ya dhamana hivyo wako nje kwa dhamana hadi Februari 2, mwaka huu kesi yao itakapotajwa.

Wanafunzi hao walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu siku ya Jumatano wakikabiliwa na mashitaka ya kuandaa mkutano usio rasmi.

Washitakiwa hao ni pamoja na Katibu Mkuu wa Mtandao wa Vyuo vya Elimu ya Juu Tanzania, Bw. Stephen Owawa, Bw. Sabinian Prince, Bw. Titus Ndula na Bw. Paul Issa ambao wamesota rumande kwa muda wa siku tatu.

Walidaiwa kuwa January 19 mwaka huu, saa 3.45 asubuhi katika maeneo ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa nia ya kutenda kosa, waliandaa mkutano usio halali na kubeba mabango.


Chanzo: MAJIRA


Prof. Baregu, Dk. Mvungi walia na Bodi ya Mikopo

2009-01-24 16:08:16
Na Sharon Sauwa, Jijini


Baadhi ya wahadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, UDSM, wameshauri kufanyiwa kwa marekebisho kwa utata uliopo katika sera ya uchangiaji wa elimu ili kuepusha migomo inayotokana na utaratibu wa utoaji wa mikopo kwa wanafunzi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti Jijini Dar es Salaam, wamesema kuna matatizo katika suala la uchangiaji katika elimu ya juu ambapo hivi sasa linaonekana kutonufaisha zaidi taifa.

``Nafikiri tuwaamshe wote. Kuna matatizo katika sera ya uchangiaji wa elimu ya juu. Inatupasa wadau wote kukaa kwa pamoja na kujadili kuhusiana na sera hii,`` akasema Profesa Mwesiga Baregu.

Akasema suala la elimu limebaki kuwa ni manufaa kwa mtu binafsi badala ya umma mzima wa Watanzania, jambo ambalo amesema linahatarisha uhai wa taifa.

``Sasa hivi, suala la elimu linaonekana kama lina manufaa ya mtu binafsi badala ya taifa,`` akasema.

Akaongeza kuwa sasa, ni lazima Watanzania wawe na elimu ya kutosha ili kukabiliana na changamoto mbalimbali zilizopo duniani.

Akaongeza kuwa ili taifa liweze kuendelea na kukabiliana na changamoto za elimu, inatakiwa wananchi wajengewe mazingira ya kuelimika mpaka mwisho wa upeo wao.

Kwa upande wake, Dk. Sengodo Mvungi amesema viongozi wa vyuo vikuu wasiwe wanachaguliwa na wanasiasa.

Akasema ili kupata viongozi wazuri wa vyuo vikuu ni muhimu wakapatikana kwa njia ya kuchaguliwa na wanataaluma wenyewe.

``Wanataaluma watumike katika kuwachagua viongozi wa vyuo, maana wao ndio wanaowajua viongozi wazuri na sio wanasiasa kama ilivyo sasa,`` akasema Dk. Mvungi.

Pia akashauri kuwa shughuli za uendeshaji wa Bodi ya Mikopo Nchini, kutenganishwa na shughuli za vyuo vikuu ili kuepusha migomo inayoweza kujitokeza kwa sababu mbalimbali, hasa madai yanayoelekezwa kwa taasisi nyingine.

Hata hivyo, akasema kuwa mgomo wa mwaka jana ambao ulisababisha chuo kufungwa tangu mwezi Novemba, anaamini ulisababishwa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu na si uendeshaji wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Mwishoni mwa mwaka jana wanafunzi wa vyuo vikuu vya umma nchini waligoma kushinikiza Serikali kufanyia marekebisho sera ya uchangiaji wa elimu ambayo walidai kuwa inaleta ubaguzi.

Hali hiyo ilisababisha vyuo vingi vya umma kufungwa na hadi sasa, uongozi wa chuo hicho umelazimika kutumia Jeshi la Polisi katika kusimamia ufanikishaji wa zoezi la kuwadahili upya wanafunzi wote wa chuo hicho.


SOURCE: Alasiri
 
Hawa wahadhiri ni vema kupitia UDASA wakajikita katika kutimiza maudhui ya uwepo wao badala ya kuingilia shughuli za uongozi wa chuo. Ni vema UDASA wakafahamu kuwa uongozi wa Chuo Kikuu Dar es Salaam ni mmoja tu, kwahiyo basi, UDASA wauachie uongozi ili uweze kutimiza kazi zake.
Si vema kwa UDASA kufanya kazi kisiasa kwani Uongozi wa Chuo upo kwa mujibu wa sheria na taratibu za kuendesha Chuo.
In the other way wananchi wa kawaida tunapata hisia kuwa kuna mkono wa kisiasa unaotumika kutoka kwa wahadhiri kwenda kwa wanafunzi na huenda jambo hili inawezekana ndiyo tatizo la vurugu za hapo UDSM kila mara.
Tuongee ukweli kwa kutafuta vyanzo vya matatizo yetu.
 
Hivi nyinyi vipi? Hivi mlitegemea maandamano yaruhusiwe wakati huo huo udahili ulikuwa unaendelea halafu ulionekana kuwa umedhibitiwa vizuri na serikali? Iweje Serikali hiyo hiyo ijihujumu kwa kuyaruhusu ili sumu yake isambae na kuharibu hata udahili ambao serikali ilionekana kuwa iko on top of things? No no. Haiwezekani. Alichofanya Kova kama msimamizi na mlinzi wa amani ni sahihi kabisa. Halafu nimesikia hata office bearers/directors wa huo mtandao sio wanafunzi. Ni akina Zito Kabwe, John Mnyika na wengineo ambao wote ni viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani. Since 2001 walipokuwa students. Hiyo ndiyo habari yenyewe. Mmeelewa sasa.
 
Back
Top Bottom