Polisi wanatoa leseni kama njugu kinyume cha taratibu

kwitega

Senior Member
Apr 10, 2012
166
49
Kila siku tunalia ajali za barabarani zimezidi mno na zinamaliza watanzania wengi. Kuanza kwa mfumo wa leseni mpya za udereva kulilenga kupunguza ajali hizo. Mapema mwaka huu JK alipokuwa akifungua mkutano Mkuu wa mwaka wa Maafisa waandamizi wa polisi mjini Moshi aliwaagiza wapunguze tatizo la kuongezeka kwa ajali za barabarani kabla halijawa janga la kitaifa. Lakini kilichopo ni kwamba; sasa leseni mpya za udereva zinatolewa kama njugu na hao hao Polisi wa kwa kushirikiana na baadhi ya watu wa TRA. Wakaguzi wa magari, na wakuu wa usalama barabarani katika baadhi ya Mikoa wanajua na wanahusika. Kwa mfano Leseni ya udereva daraja ABDE inatolewa kwa sh. 250,000 hadi 300,000/- kwa mtu ambaye hajawahi kabisa kuwa na leseni ya aina yoyote. Hakuna cha kufanyiwa test. Maana yake ni kwamba hata mtu ambaye si dereva kabisa anaweza kupata leseni. Leseni hii ni kwa ajili ya pikipiki, magari madogo na makubwa isipokuwa ya abiria.

Kwa upande wa leseni daraja C1, C2 hizi zinatolewa kwa sh. 400,000/- na watu wanamiminika kuzichukua. Vyeti vya VETA pia vinaghushiwa kwa kushirikiana na Polisi hao hao kwa malengo ya mhusika kupata leseni ya madaraja hayo. Kibaya zaidi wakaguzi hao wa magari wanadaiwa kupeleka return kwa baadhi ya vigogo wa Polisi Makao Makuu. Hapa maana yake nini? Hivi Polisi kwa nini wameamua kuwa wanyama kiasi hiki dhidi ya raia? Hapa ajali zitapungua au ndiyo zitazidi kutumaliza kutokana na baadhi ya watu kupata leseni na kuendesha magari yakiwemo ya abiria ilhali hawana ujuzi wala sifa za kazi hiyo? Usalama wa Taifa wako wapi? IGP hajui haya?, JK hajui haya? Au mpaka nani apate ajali kutokana na madereva wenye leseni za aina hii ndio wachukue hatua?
 
Kila siku tunalia ajali za barabarani zimezidi mno na zinamaliza watanzania wengi. Kuanza kwa mfumo wa leseni mpya za udereva kulilenga kupunguza ajali hizo. Mapema mwaka huu JK alipokuwa akifungua mkutano Mkuu wa mwaka wa Maafisa waandamizi wa polisi mjini Moshi aliwaagiza wapunguze tatizo la kuongezeka kwa ajali za barabarani kabla halijawa janga la kitaifa. Lakini kilichopo ni kwamba; sasa leseni mpya za udereva zinatolewa kama njugu na hao hao Polisi wa kwa kushirikiana na baadhi ya watu wa TRA. Wakaguzi wa magari, na wakuu wa usalama barabarani katika baadhi ya Mikoa wanajua na wanahusika. Kwa mfano Leseni ya udereva daraja ABDE inatolewa kwa sh. 250,000 hadi 300,000/- kwa mtu ambaye hajawahi kabisa kuwa na leseni ya aina yoyote. Hakuna cha kufanyiwa test. Maana yake ni kwamba hata mtu ambaye si dereva kabisa anaweza kupata leseni. Leseni hii ni kwa ajili ya pikipiki, magari madogo na makubwa isipokuwa ya abiria.

Kwa upande wa leseni daraja C1, C2 hizi zinatolewa kwa sh. 400,000/- na watu wanamiminika kuzichukua. Vyeti vya VETA pia vinaghushiwa kwa kushirikiana na Polisi hao hao kwa malengo ya mhusika kupata leseni ya madaraja hayo. Kibaya zaidi wakaguzi hao wa magari wanadaiwa kupeleka return kwa baadhi ya vigogo wa Polisi Makao Makuu. Hapa maana yake nini? Hivi Polisi kwa nini wameamua kuwa wanyama kiasi hiki dhidi ya raia? Hapa ajali zitapungua au ndiyo zitazidi kutumaliza kutokana na baadhi ya watu kupata leseni na kuendesha magari yakiwemo ya abiria ilhali hawana ujuzi wala sifa za kazi hiyo? Usalama wa Taifa wako wapi? IGP hajui haya?, JK hajui haya? Au mpaka nani apate ajali kutokana na madereva wenye leseni za aina hii ndio wachukue hatua?
Mh.... bure unawalaumu polisi. Unataka wafe njaa wakati maraisi, watoto wa marais, mawaziri, wabunge, nk wanakwapua kushoto, kulia, juu, chini?
 
Ahaa, unafurahia ajali zinazotokea kwa sababu ya upuuzi kama huo? Huna hata huruma. Nitafurahi na kufarijika sana iwapo siku moja utapanda basi linaloendeshwa na dereva aliyepata leseni kwa njia hizi, kisha basi hilo liache njia na kupinduka. Kati ya abiria wote watakaokuwa kwenye basi hilo; UFE wewe mwenyewe wala asiwepo majeruhi yeyote. Hicho ndicho unachostahili.
 
we umelijua leo hili!Mbona ni kawaida hata tushaacha kuongelea!Ukitaka usiipate hiyo leseni basi fuata utaratibu wa serikali!
 
Ahaa, unafurahia ajali zinazotokea kwa sababu ya upuuzi kama huo? Huna hata huruma. Nitafurahi na kufarijika sana iwapo siku moja utapanda basi linaloendeshwa na dereva aliyepata leseni kwa njia hizi, kisha basi hilo liache njia na kupinduka. Kati ya abiria wote watakaokuwa kwenye basi hilo; UFE wewe mwenyewe wala asiwepo majeruhi yeyote. Hicho ndicho unachostahili.
Bwana n'logo kwanini unakuwa mgumu kuelewa. Mimi ujumbe wangu ni mmoja tu..... raisi legelege huzaa mawaziri legelege ambao huzaa serikali legelege. Hivyo ukianza kujifanya unawakomalia hawa wa chini wakati walio juu wanakula na kunya hapohapo kama nzige hutafika popote. Tuanzie juu. Sasa hilo la kusema nafurahia ajali mh... mimi nasema HAPANA. Siwezi hata siku moja kufurahia ajali ila NIMEKUONYESHA LILIPO TATIZO, ili usiendelee tena kupapasa kizani. Understand?
 
Unataka kikwete akasimame barabarani kama trafic. Kila kitu raisi . Mpaka itafika siku dadako asipolala nyumbani utasema kisa raisi
 
Haya yote ni kwasababu watz tumekubali akili ndogo itawale akili kubwa (ujinga utawale ujuzi/ knowledge) na kukubali kuendelea kuwa dhaifu hata katika upuuzi!!!!
 
Kila siku tunalia ajali za barabarani zimezidi mno na zinamaliza watanzania wengi. Kuanza kwa mfumo wa leseni mpya za udereva kulilenga kupunguza ajali hizo. Mapema mwaka huu JK alipokuwa akifungua mkutano Mkuu wa mwaka wa Maafisa waandamizi wa polisi mjini Moshi aliwaagiza wapunguze tatizo la kuongezeka kwa ajali za barabarani kabla halijawa janga la kitaifa. Lakini kilichopo ni kwamba; sasa leseni mpya za udereva zinatolewa kama njugu na hao hao Polisi wa kwa kushirikiana na baadhi ya watu wa TRA. Wakaguzi wa magari, na wakuu wa usalama barabarani katika baadhi ya Mikoa wanajua na wanahusika. Kwa mfano Leseni ya udereva daraja ABDE inatolewa kwa sh. 250,000 hadi 300,000/- kwa mtu ambaye hajawahi kabisa kuwa na leseni ya aina yoyote. Hakuna cha kufanyiwa test. Maana yake ni kwamba hata mtu ambaye si dereva kabisa anaweza kupata leseni. Leseni hii ni kwa ajili ya pikipiki, magari madogo na makubwa isipokuwa ya abiria.

Kwa upande wa leseni daraja C1, C2 hizi zinatolewa kwa sh. 400,000/- na watu wanamiminika kuzichukua. Vyeti vya VETA pia vinaghushiwa kwa kushirikiana na Polisi hao hao kwa malengo ya mhusika kupata leseni ya madaraja hayo. Kibaya zaidi wakaguzi hao wa magari wanadaiwa kupeleka return kwa baadhi ya vigogo wa Polisi Makao Makuu. Hapa maana yake nini? Hivi Polisi kwa nini wameamua kuwa wanyama kiasi hiki dhidi ya raia? Hapa ajali zitapungua au ndiyo zitazidi kutumaliza kutokana na baadhi ya watu kupata leseni na kuendesha magari yakiwemo ya abiria ilhali hawana ujuzi wala sifa za kazi hiyo? Usalama wa Taifa wako wapi? IGP hajui haya?, JK hajui haya? Au mpaka nani apate ajali kutokana na madereva wenye leseni za aina hii ndio wachukue hatua?


Uliyasema yote ni sahihi wala mtu asije kutaka tutoe ushahidi!! Yote haya ni matunda ya uongozi na serikali iliyo DHAIFU!!! Kwa uzembe na ujinga wao wanaaliangamiza Taifa hili pole pole!!
 
Unataka kikwete akasimame barabarani kama trafic. Kila kitu raisi . Mpaka itafika siku dadako asipolala nyumbani utasema kisa raisi
Tz imefikia hapa kwa sababu ya watu kama wewe na huyu kikwete wako
 
Free market system hiyo! Hata picha hakuna haja ya kupeleka unashangaa wanakuletea tu!
 
kupata leseni legally imekua NGUMU vibaya mno. bila hawa jamaa kujitolea kusaidia kutoa leseni expressly sijui ingekuwaje.
 
Back
Top Bottom