Polisi wamezionyesha 'silaha' walizokutwa nazo waandamanaji wa Chadema?

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234



Ni kujisahau, kujiamini au nini? Hivi polisi wamezionyesha ‘silaha’ walizokutwa nazo waanadamanaji wa Chadema kusapoti uhalali wao (wa polisi) kutumia risasi za moto dhidi yao?

Polisi wetu wamewahi kufanya hivyo huko nyuma:

• Mwaka 1998 katika vurugu za Mwembechai Polisi walionyesha kwa waandishi wa habari ‘silaha’ walisodai zilizokutwa kwa waandamanaji au zilizotupwa katika maeneo ya vurugu kuonyosha kwamba polisi ilibidi kutumia risasi za moto kuwaua waanadamanji wanne. ‘Silaha’ hizo zilikuwa ni mvisu, mawe, miti ya bendera n.k.
• Mwaka 2001 katika mauaji ya makumi ya wana-CUF kule Pemba, polisi walionyesha ‘silaha’ walizodai zilikutwa kwa baadhi ya waandamanaji au kuzitupa kwenye maeneo ya vurugu. ‘Silaha’ zilikuwa ni mapanga, mawe, fimbo, viberiti n.k.

Katika matukio yote hayo mawili hakukuwepo silaha zozote za moto kama vile bunduki au bastola. Swali ni vipi huko Arusha polisi hawakuja na kitu kama hicho kutilia nguvu hoja yao ya ulazima wa kuuwa kwa kutumia risasi? Walisahau?
 
Wamesahau kwa vile walipata taharuki kubwa. Lakini angalau kwa hilo, safari wamekuwa wakweli -- hawakutaka kuwasingizia.
 
'Nguvu ya Umma' ni kama kimbunga ambao hakuna anayeweza kukishika wala kukiona ila kwa mitikisiko yake haizuliki; miti ya mbuyu hung'ooka, nyumba za udhalimu huanguka na silaha za moto za mafisadi kugeuka kimya ka maiti ya ndugu zetu mashujaa wa Arusha ndani ya friji.

Hivyo kama kuna mtu anatafuta aina ya silaha wanayoitumia CHADEMA basi asipate sana taabu; jina la silaha hiyo inaitwa 'AK 47 Nguvu ya Umma' sembuse Kikwete anakuja na silaha aina ya
'Gobole UFISADI' kupambana na 'adui fikra huru'!!

Kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu wananchi tutashinda vita dhidi ya MAFISADI kwa kutumia silaha hatari ya 'AK-47 Nguvu ya Umma' na kujazwa risasi zisizokauka nguvu aina ya 'Fikra Huru' ili kuleta Tanzania mpya na kuulinda umoja wetu wa kitaifa.
 
Na kizuri zaidi tumejua ubora na udhaifu wao,polisi iliishiwa mabomu na risasi,maana yake ni kwamba tukiandamana siku tatu mfululizo watakuwa hawana kitu tena,aluta continua
 
Back
Top Bottom