Mkuu tuarudi pale pale.
Mkuu Nguruvi3
Ninakubaliana kwa kiwango fulani katika angalizo lako lakini pia kumbuka ulinzi unaanzia ndani ya familia zetu.
Badala ya kuanza kulaumu polisi, ingefaa kwanza kuangalia kwa upana malezi ya hao watenda maovu.
Kama kuna broken families/society usitegemee polisi wanaweza kumaliza hilo tatizo hata kama wanatenda kile ambacho unakisema kwa sababu broken families/society ni kiwanda cha kuzalisha watoto ambao wanakuwa wezi au majambazi ya kesho.
Ni sawa na kujaribu kuzuia madawa ya kulevya kwa kumatama wauzaji au watumiaji wakati mashamba au viwanda vya kuzalisha vikiwa vinaendelea kuzalisha.
Tatizo ninaloliona hili suala unaliangalia kwa kutumia macho ya matokeo badala ya kutumia macho ya chanzo.
Kama mmonyoko wa maadili utaendelea kuzalishwa kuanzia kwenye familia tusitegemee polisi wanaweza kumaliza hili tatizo la vijana kujiingiza kwenye kazi za wizi au ujambazi.
Mbona kwenye kuzuia UKUTA walitosha ?Kupambana na uhalifu ni jukumu la kila mmoja ukiwemo wewe mtoa bango.Polisi waliopo ni wachache kuliko mahitaji halisi.
Wewe unapingana na Mh Raisi? Alisema police wapo wa kutosha kabisa, tena kasema police jamii waondolewe kabisa. Hali ni mbaya sana huku kwetu MJOMBA, maeneo yote ya kipunguni, machimbo, Moshi bar, Kwamkoremba, KWA Diwani, bomba mbili, KWA Mpemba nenda hadi Chanika ni hatari sana hasa KWA wageni wanaohamia na kufungua biashara ni lazma wasulubiwe na nao vibaka, tena wanakuvamia Kundi kubwa hata majirani hawazubutu kutoka ni shida sana, kesho LA police wanabidi wafanye juhudi za maksudi haraka sana kinyume cha hapo KWA kweli hali inazidi kuwa mbaya kila siku.Kupambana na uhalifu ni jukumu la kila mmoja ukiwemo wewe mtoa bango.Polisi waliopo ni wachache kuliko mahitaji halisi.
Watashughulikiwa utoe ushirikiano km ulivyoutoa hapa JFWewe unapingana na Mh Raisi? Alisema police wapo wa kutosha kabisa, tena kasema police jamii waondolewe kabisa. Hali ni mbaya sana huku kwetu MJOMBA, maeneo yote ya kipunguni, machimbo, Moshi bar, Kwamkoremba, KWA Diwani, bomba mbili, KWA Mpemba nenda hadi Chanika ni hatari sana hasa KWA wageni wanaohamia na kufungua biashara ni lazma wasulubiwe na nao vibaka, tena wanakuvamia Kundi kubwa hata majirani hawazubutu kutoka ni shida sana, kesho LA police wanabidi wafanye juhudi za maksudi haraka sana kinyume cha hapo KWA kweli hali inazidi kuwa mbaya kila siku.
Mkuu yale mazoezi ya askari mitaani, pikipiki, maderaya n.k. yalilenga nini ?
Pili, malezi ni suala moja, usimamizi ni suala jingine. Yuko wapi Makonda wa UKUTA? Yuko wapi kamishna wa operesheni maalum za Polisi? Yuko wapi kamanda wa kanda maalumu? Yuko wapi IGP?
Yuko wapi waziri wa mambo ya ndani? Yuko wapi Rais?
Mbona walikuwepo wakati wa UKUTA wakitumia kila resources?
Leo inageukaje suala la malezi?
Mkuu wa mkoa anapopanda miti , watu wakicharangwa mapanga ina picha gani?
Mkuu wa mkoa anaposema wanajipanga, walikuwa wapi siku zote?
Mkuu tatizo si malezi, hayo ni sehemu tu ya jamii.
Tatizo ni viongozi kujishughulisha na mambo trivial na kuacha majukumu yao.
Hakuna mtu aliyekufa katika mikutano ya siasa mwaka huu mzima.
Ni wangapi wamekufa kwa ujambazi? Ni wangapi wamekufa kwa ajali?
Haya yanaeleza kufeli na lazima tukubali kusimama pamoja na kuwaambia, wanafeli na tuna feli kama Taifa
Tuwaambie wazi, mikutano ya jangwani si tatizo, tatizo ni mapanga , visu wanavyopambana navyo wananchi kule mitaani.
Ni akina hofu waliyo nayo akina mama kule mitaani. Hata kutembea na pochi katika nchi wanayolipa kodi sasa ni 'privilege' .
Leo askari wetu yupo Lugalo si kwasababu nyingine bali vibaka wa nchi yetu. Inauma sana. Tunafeli hatukubali
Wanafeli, tunafeli kama Taifa, inasikitisha sana!
Tukubali kuwa tunafeli , tukae pamoja kuangalia kwanini tuna feli. Lakini ukweli kuwa yunafeli hatuwezi kuukwepa!
Unaejidanganya ni wewe mpiga vigeregereUsijidanganye
Mkuu yanatokea hakuna anayejisughulisha. Ingalikuwa suala la upinzani tungeona kila aina ya mazoezi na silaha. Hili jambo linasikitisha sanaMkuu Nguruvi3 ukipata nafasi pita mtaa huu.
Mkuu yanatokea hakuna anayejisughulisha. Ingalikuwa suala la upinzani tungeona kila aina ya mazoezi na silaha. Hili jambo linasikitisha sana
Tuliambiwa wapo waliokwenda Jordan, picha zikaonekana na misuli ya nguvu
Leo ujambazi umekuwa maisha ya kawaida kana kwamba hakuna ulinzi na usalama
Hawajali, haiwahusu. Wanajali masilahi yao ya kisiasa yanapoguswa! Utawasikia kila siku redioni na katika TV
Uhalifu wowote ni lazima ushughulikiwe kwakua uhalifu ni uhalifu tu.Na si kuvaa vizubao kukimbiza na bodaboda na kukama motor vehicle za magari