Polisi wafanye kazi yao ya kupambana na Wahalifu Dar

Ahsante sana Mkuu Nguruvi3, nakubaliana nawe katika yote uliyoyaandika kuhusu polisi kujihusisha zaidi na masuala ya kisiasa kuliko kupambana na uhalifu nchini.

Siku zote kuna polisi wa kutosha kupambana na wanasiasa ambao wanafuata katiba ya nchi kufanya kazi zao ikiwemo kufanya mikutano na maandamano sehemu mbali mbali nchini, lakini wakati huo huo kunakuwepo na "upungufu mkubwa" wa polisi inapokuja kwenye kupambana na wahalifu ambao huwaweka wananchi roho juu kwa kutishia usalama wa mali zao na hata uhai wao.
Utakumbuka matamko ya mkuu wa mkoa Makonda wakati wa mambo ya kisiasa. Polisi walitanda mitaani wakifanya mazoezi kwa ajili ya wanasiasa wanaofanya kazi zao za siasa. Kazi ya mwanasiasa ni kukutana na watu bila kuwadhuru. Ni hiari isiyomuumiza mtu

Leo tunasikia anapanda miti! Si kipaumbele chake na hiyo ni kazi yenye mamlaka zake

Wananchi wanaishi kwa hofu ya vibaka, akina mama wakiwa waathirika wakubwa wa unyama unaoendelea mkoa wa Dar es Slaam kupitia vibaka. Kesho utawasikia wanasiasa wakisema 'tulinde Amani na utulivu'

Hivi mtu aliyekatwa na wembe au kisu at bisubisu ambayo imetumika kwa watu wengine ana Amani gani?

Mtu huyo akifikiria magonjwa yanayoweza kupatikana kwa damu za watu ambaye yeye ni sehemu yake ana Amani na utulivu gani?

Amani na utulivu ni pale wanasiasa masilahi yao yanapokuwa salama. Huko mitaani watu wanalala roho juu juu, hawa wana Amani gani

Viongozi hawa wamepataikana kwa njia za kisiasa ndiyo maana utasikia tumejipanga

Hivi Makonda tangu aingie madarakani takribani mwaka bado anajipanga tu. Tatizo la uhalifu linajulikana lakini anaaminisha wananchi anajipanga. Likija la siasa hakuna cha kujipanga ni lake

Tulisema watafeli na Taifa lina feli. Huu ni mwanzo tu wa kufeli

Mkuu wa mkoa anapopanda miti barabarani watu wakichezea bisibisi, viwembe na mapanga ni kufeli kwa kiwango cha juu sana.

Wananchi hawana Amani, tunaambiwa nchi ina amni na utulivu!

Tunafeli kama Taifa kwasababu ya kuwa na viongozi wasiojali. Tunafeli ! tunafeli tunafeli

Wanafeli! mbwembwe na harakati zote sasa Tunafeli sana
 
Utakumbuka matamko ya mkuu wa mkoa Makonda wakati wa mambo ya kisiasa. Polisi walitanda mitaani wakifanya mazoezi kwa ajili ya wanasiasa wanaofanya kazi zao za siasa. Kazi ya mwanasiasa ni kukutana na watu bila kuwadhuru. Ni hiari isiyomuumiza mtu

Leo tunasikia anapanda miti! Si kipaumbele chake na hiyo ni kazi yenye mamlaka zake

Wananchi wanaishi kwa hofu ya vibaka, akina mama wakiwa waathirika wakubwa wa unyama unaoendelea mkoa wa Dar es Slaam kupitia vibaka. Kesho utawasikia wanasiasa wakisema 'tulinde Amani na utulivu'

Hivi mtu aliyekatwa na wembe au kisu at bisubisu ambayo imetumika kwa watu wengine ana Amani gani?

Mtu huyo akifikiria magonjwa yanayoweza kupatikana kwa damu za watu ambaye yeye ni sehemu yake ana Amani na utulivu gani?

Amani na utulivu ni pale wanasiasa masilahi yao yanapokuwa salama. Huko mitaani watu wanalala roho juu juu, hawa wana Amani gani

Viongozi hawa wamepataikana kwa njia za kisiasa ndiyo maana utasikia tumejipanga

Hivi Makonda tangu aingie madarakani takribani mwaka bado anajipanga tu. Tatizo la uhalifu linajulikana lakini anaaminisha wananchi anajipanga. Likija la siasa hakuna cha kujipanga ni lake

Tulisema watafeli na Taifa lina feli. Huu ni mwanzo tu wa kufeli

Mkuu wa mkoa anapopanda miti barabarani watu wakichezea bisibisi, viwembe na mapanga ni kufeli kwa kiwango cha juu sana.

Wananchi hawana Amani, tunaambiwa nchi ina amni na utulivu!

Tunafeli kama Taifa kwasababu ya kuwa na viongozi wasiojali. Tunafeli ! tunafeli tunafeli
Mkuu kuna aliyesema Makonda ni mpiga debe mzuri sana, yeye anasubiri amri ya dereva.
 
hao hawana hatari kuliko mikutano na maandamano ya vyama vya sihasa....
 
jaman hao no polis wa dar lakin pilisi wa mikoan big up San wanazuia na kupamban na wahalifu man to man
 
Vipaumbele vya hawa wanasiasa vimekaa kinyume nyume Mkuu. Utadhani hawaishi katika maeneo ambayo wananchi wanaishi kwa hofu kubwa kutokana na hawa wahalifu wanaotishia usalama wa raia na mali zao.

Wananchi wanalipa kodi kubwa sana Serikalini ili kupata huduma mbali mbali muhimu ikiwemo hii ya kuhakikishiwa kuishi kwa amani na usalama wa mali zao, lakini cha kustaajabisha kodi zinaongezeka kila mwaka lakini huduma muhimu ikiwemo hii ya usalama wa raia na mali zao zikizidi kudorora au kukosekana kabisa katika maeneo mengi nchini hivyo kusababisha Watanzania wengi kuishi kwa hofu kubwa sana.

Utakumbuka matamko ya mkuu wa mkoa Makonda wakati wa mambo ya kisiasa. Polisi walitanda mitaani wakifanya mazoezi kwa ajili ya wanasiasa wanaofanya kazi zao za siasa. Kazi ya mwanasiasa ni kukutana na watu bila kuwadhuru. Ni hiari isiyomuumiza mtu

Leo tunasikia anapanda miti! Si kipaumbele chake na hiyo ni kazi yenye mamlaka zake

Wananchi wanaishi kwa hofu ya vibaka, akina mama wakiwa waathirika wakubwa wa unyama unaoendelea mkoa wa Dar es Slaam kupitia vibaka. Kesho utawasikia wanasiasa wakisema 'tulinde Amani na utulivu'

Hivi mtu aliyekatwa na wembe au kisu at bisubisu ambayo imetumika kwa watu wengine ana Amani gani?

Mtu huyo akifikiria magonjwa yanayoweza kupatikana kwa damu za watu ambaye yeye ni sehemu yake ana Amani na utulivu gani?

Amani na utulivu ni pale wanasiasa masilahi yao yanapokuwa salama. Huko mitaani watu wanalala roho juu juu, hawa wana Amani gani

Viongozi hawa wamepataikana kwa njia za kisiasa ndiyo maana utasikia tumejipanga

Hivi Makonda tangu aingie madarakani takribani mwaka bado anajipanga tu. Tatizo la uhalifu linajulikana lakini anaaminisha wananchi anajipanga. Likija la siasa hakuna cha kujipanga ni lake

Tulisema watafeli na Taifa lina feli. Huu ni mwanzo tu wa kufeli

Mkuu wa mkoa anapopanda miti barabarani watu wakichezea bisibisi, viwembe na mapanga ni kufeli kwa kiwango cha juu sana.

Wananchi hawana Amani, tunaambiwa nchi ina amni na utulivu!

Tunafeli kama Taifa kwasababu ya kuwa na viongozi wasiojali. Tunafeli ! tunafeli tunafeli
 
Hizi falsafa zimekufa na Baba Kabwela Julius Nyerere.

Siku hizi Scorpion anakutoboa macho na watu wanaangalia na kujipitia na hamsini zao.
Watu wanahasira na Scorpion huko jela sidhani kama atakuwa salama.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mkuu kuna aliyesema Makonda ni mpiga debe mzuri sana, yeye anasubiri amri ya dereva.
Huyu alikuwa mwenyekiti wa Taifa wa Chipukizi!
Tunajua aliongoza genge lililoleta vurugu katika mkutano halali wa siasa pale Ubungo akiwepo mzee Warioba

Kwasababu ya inexperience yake, leo anapanda miti wananchi wakitweta kwa hofu, vibaka wakitamba mitaani

Kwasiku zote alizokaaa ofisini hakujipanga, leo anatueleza amejipanga! No! waliojipanga ni vibaka na majambazi wanaosumbua wananchi. Watu hawana Amani , akina mkuu wa mkoa wanahubiri kulinda Amani wakiwa wanapanda miti vibaka wanafanyizia watu.

Huku ndiko kufeli tulikosema siku za mwanzo. Tunafeli kwasababu wanaanza kufeli.

Maneno ya kujipanga ni maneo ya kushindwa. Wanafeli , mkoa unafeli nchi inafeli

Tunafeli
 
Kupambana na uhalifu ni jukumu la kila mmoja ukiwemo wewe mtoa bango.Polisi waliopo ni wachache kuliko mahitaji halisi.
Hii hoja ya Polisi wachache ni hoja dhaifu sana na inaeleza mengi kuliko uchache wao

Ni wachache kwa vipi? tuliwaona mitaani na maderaya na kila silaha za kupambana na UKUTA?

Tulisema ni mazoezi dhidi ya wanasiasa , wakasema ni maandalizi ya kupambana na uhalifu.
Leo uhalifu unafanyika tunasikia Polisi ni wachache

UKUTA ni watu wengi sana kuliko magenge ya vibaka na majambazi. Kinachotokea ni viongozi wote kuhamishia fikra zao kuwa upinzani ndio uhalifu kwasababu tu ya masilahi ya kisiasa

Jeshi la Polisi ndilo linapaswa kutueleza kama kuna upungufu wa askari, ili nasi tuulize wale tuliowaona mitaani wakifanya mazoezi makali walitoka wapi?

Tunauliza makonda anapopanda miti hilo ndilo jukumu lake la kwanza mkoani?

Picha kubwa ni kushindwa kwa uongozi mzima na vyombo husika kwasababu tu ya kufikiria kwa mtazamo wa kisiasa na si masilahi ya umma.

Hatuwezi kusema kuna Amani na utulivu huku watu wakisulubiwa, wakilala kwa hofu, akina mama wakishindwa kubeba pochi zao, akina mababa wakicharangwa mapanga n.k.

Amani na utulivu ni lazima uwe kwa wananchi, na si kwa wanasiasa.

Leo mkuu wa mkoa anapanda miti kwa kujua kuna Amani na utulivu, kesho akisikia wapinzani wanafanya mkutano Amani na utulivu hakuna!

Mkuu wa mkoa anpanda miti bila huruma ya wananchi wanaoteswa na vibaka na majambazi, halafu kesho utamsikia akisisitiza Amani na utuliuvu.

Kuna Amani na utulivu gani kwa mtu aliyetobolewa macho? Utawasikia tunajipanga.

Makonda likuwa DC Dar na sasa mkuu wa mkoa, anahitaji kujipanga vipi?

Neno kujipanga ni kauli ya mwisho ya kufunika madhaifu ya kushindwa.

Wanafeli, tunafeli na sisi tunateswa na vibaka.

Wao wanalindwa majumbani mwao, wana Amani na utulivu.

Sisi mitaani hatuna Amani na utulivu na hatupendi waje kuzungumzia maneno hayo mbele yetu. Wanatukejeli, wanatudhalilisha.

Waache kutumia neno Amani na utulivu wakati sisi hatuna Amani.
Wanatung'onga tukidhalilishwa na majambazi.

Wanakusanya kodi zetu na kisha kutukejeli wanajipanga!

Utamwambia mama aliyechanjwa kwa wembe Amani na utulivu gani?

Wanafeli, tunafeli kama Taifa.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hili ni la kustaajabisha sana Mkuu kwenye kupambana na viongozi wa vyama vya upinzani hata siku moja hutasikia hili la kuwepo polisi wachache. Kama tulivyowaona hivi karibuni wakitunisha misuli yao kwenye makazi ya raia, lakini tukirudi kwenye kulinda usalama wa raia na mali zao hapo ndiyo utaanza kusikia vigugumizi vya kutokuwepo na polisi wa kutosha na wakati huo huo Watanzania tukiendelea kulipa kodi kubwa ili kupata huduma mbalimbali muhimu ikiwemo hii ya usalama wa raia na mali zao.

usitulazimishe kuwa ni wachache, mbona mazoezi ya kudhibiti wapinzani wanaonekana wengi? wafanye kazi yao wenyewe
 
Mkuu jana tumezungumzia hili suala

Akina Makonda wanapanda miti wakisubiri kupambana na wapinzani, vibaka wanaumiza umma

Polisi walikuwa na mzoezi makali ya kupambana na uhalifu. Damu zinatapakaa mitaani kwa mapanga

Kamanda wa polisi wa operesheni maalumu aliyekuwa mstari wa mbele wakati wa UKUTA, hatumsikii tena

Rais alizundua kampeni ya uhalifu pale kinondoni, hatujui ina matokeo gani

Tukaona IGP akiwa na vijana katika picha, wanakwenda mafunzoni middle east, vibaka wanatamba bila hofu

Huku kama si kufeli ni kitu gani?

MsemajiUkweli
 
Polisi wanakusanya nguvu ya kupambana na UKAWA, hawa wahalifu kwao hawana kipaumbele chochote Mkuu. Subiri wasikie UKAWA wanaandamana, utashangaa jinsi tutakavyowaona walivyo wengi na wakitanua misuli yao kila kona kwenye makazi ya raia.

Mkuu jana tumezungumzia hili suala

Akina Makonda wanapanda miti wakisubiri kupambana na wapinzani, vibaka wanaumiza umma

Polisi walikuwa na mzoezi makali ya kupambana na uhalifu. Damu zinatapakaa mitaani kwa mapanga

Kamanda wa polisi wa operesheni maalumu aliyekuwa mstari wa mbele wakati wa UKUTA, hatumsikii tena

Rais alizundua kampeni ya uhalifu pale kinondoni, hatujui ina matokeo gani

Tukaona IGP akiwa na vijana katika picha, wanakwenda mafunzoni middle east, vibaka wanatamba bila hofu

Huku kama si kufeli ni kitu gani?

MsemajiUkweli
 
Mkuu jana tumezungumzia hili suala

Akina Makonda wanapanda miti wakisubiri kupambana na wapinzani, vibaka wanaumiza umma

Polisi walikuwa na mzoezi makali ya kupambana na uhalifu. Damu zinatapakaa mitaani kwa mapanga

Kamanda wa polisi wa operesheni maalumu aliyekuwa mstari wa mbele wakati wa UKUTA, hatumsikii tena

Rais alizundua kampeni ya uhalifu pale kinondoni, hatujui ina matokeo gani

Tukaona IGP akiwa na vijana katika picha, wanakwenda mafunzoni middle east, vibaka wanatamba bila hofu

Huku kama si kufeli ni kitu gani?

MsemajiUkweli
Mkuu Nguruvi3

Ninakubaliana kwa kiwango fulani katika angalizo lako lakini pia kumbuka ulinzi unaanzia ndani ya familia zetu.

Badala ya kuanza kulaumu polisi, ingefaa kwanza kuangalia kwa upana malezi ya hao watenda maovu.

Kama kuna broken families/society usitegemee polisi wanaweza kumaliza hilo tatizo hata kama wanatenda kile ambacho unakisema kwa sababu broken families/society ni kiwanda cha kuzalisha watoto ambao wanakuwa wezi au majambazi ya kesho.

Ni sawa na kujaribu kuzuia madawa ya kulevya kwa kumatama wauzaji au watumiaji wakati mashamba au viwanda vya kuzalisha vikiwa vinaendelea kuzalisha.

Tatizo ninaloliona hili suala unaliangalia kwa kutumia macho ya matokeo badala ya kutumia macho ya chanzo.

Kama mmonyoko wa maadili utaendelea kuzalishwa kuanzia kwenye familia tusitegemee polisi wanaweza kumaliza hili tatizo la vijana kujiingiza kwenye kazi za wizi au ujambazi.
 
Mkuu Nguruvi3

Ninakubaliana kwa kiwango fulani katika angalizo lako lakini pia kumbuka ulinzi unaanzia ndani ya familia zetu.

Badala ya kuanza kulaumu polisi, ingefaa kwanza kuangalia kwa upana malezi ya hao watenda maovu.

Kama kuna broken families/society usitegemee polisi wanaweza kumaliza hilo tatizo hata kama wanatenda kile ambacho unakisema kwa sababu broken families/society ni kiwanda cha kuzalisha watoto ambao wanakuwa wezi au majambazi ya kesho.

Ni sawa na kujaribu kuzuia madawa ya kulevya kwa kumatama wauzaji au watumiaji wakati mashamba au viwanda vya kuzalisha vikiwa vinaendelea kuzalisha.

Tatizo ninaloliona hili suala unaliangalia kwa kutumia macho ya matokeo badala ya kutumia macho ya chanzo.

Kama mmonyoko wa maadili utaendelea kuzalishwa kuanzia kwenye familia tusitegemee polisi wanaweza kumaliza hili tatizo la vijana kujiingiza kwenye kazi za wizi au ujambazi.
Mkuu yale mazoezi ya askari mitaani, pikipiki, maderaya n.k. yalilenga nini ?

Pili, malezi ni suala moja, usimamizi ni suala jingine. Yuko wapi Makonda wa UKUTA? Yuko wapi kamishna wa operesheni maalum za Polisi? Yuko wapi kamanda wa kanda maalumu? Yuko wapi IGP?
Yuko wapi waziri wa mambo ya ndani? Yuko wapi Rais?

Mbona walikuwepo wakati wa UKUTA wakitumia kila resources?

Leo inageukaje suala la malezi?

Mkuu wa mkoa anapopanda miti , watu wakicharangwa mapanga ina picha gani?

Mkuu wa mkoa anaposema wanajipanga, walikuwa wapi siku zote?

Mkuu tatizo si malezi, hayo ni sehemu tu ya jamii.

Tatizo ni viongozi kujishughulisha na mambo trivial na kuacha majukumu yao.

Hakuna mtu aliyekufa katika mikutano ya siasa mwaka huu mzima.

Ni wangapi wamekufa kwa ujambazi? Ni wangapi wamekufa kwa ajali?

Haya yanaeleza kufeli na lazima tukubali kusimama pamoja na kuwaambia, wanafeli na tuna feli kama Taifa

Tuwaambie wazi, mikutano ya jangwani si tatizo, tatizo ni mapanga , visu wanavyopambana navyo wananchi kule mitaani.

Ni akina hofu waliyo nayo akina mama kule mitaani. Hata kutembea na pochi katika nchi wanayolipa kodi sasa ni 'privilege' .

Leo askari wetu yupo Lugalo si kwasababu nyingine bali vibaka wa nchi yetu. Inauma sana. Tunafeli hatukubali

Wanafeli, tunafeli kama Taifa, inasikitisha sana!

Tukubali kuwa tunafeli , tukae pamoja kuangalia kwanini tuna feli. Lakini ukweli kuwa yunafeli hatuwezi kuukwepa!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Polisi wanakusanya nguvu ya kupambana na UKAWA, hawa wahalifu kwao hawana kipaumbele chochote Mkuu. Subiri wasikie UKAWA wanaandamana, utashangaa jinsi tutakavyowaona walivyo wengi na wakitanua misuli yao kila kona kwenye makazi ya raia.
Ni aibu kwa nchi hii vibaka kucharanga mapanga watu kana kwamba hatuna 'law and order'

Polisi na mazoezi yao imefikia wapi?

Mkuu wa Mkoa anapanda miti, wananchi wanateseka. Real kwamba tatizo la Dar ni miti!

Ingalikuwa siasa, leo ungeona serikali nzima ikijipanga kwa matamako na vitisho

Kwa hili la vibaka eti wanajipanga.Walipoteuliwa na Rais hawakuwa na muda wa kujipanga

Wanajipanga wakati vibaka wanatoboa macho watu, wanapiga mapanga, akina mama sasa hata kushika pochi ni kama 'zawadi' na si haki yao. Roho za akina mama juu

Akina baba wakiamka asubuhi hawajui watafika kazini salama na kurudi makwao.

Tunaambiwa Amani na utulivu wakati wa mikutano ya siasa.

Hivi kwa sasa kuna Amani gani kwa mtu aliyelela hospitali baada ya kucharangwa mapanga na visu?

Wanatumia Amani na utulivu kwa wanasiasa, huku mitaani ni shida tu. Kweli!

Wote hakuna anyetoa tamko. Hili lingekuwa la NCCR au CUF ungeiona serikali nzima ikivuma , matamko n.k. La vibaka kila mmoja amejificha

Afadhali mkuu wa mkoa aliyesema wanajipanga maana walikuwa hawajajipanga.

Waziri wa mambo ya ndani haonekani, wale wakuu wa Polisi hatuwaoni.
Tunaona vibaka tu wakitamba, wakicharanga mapanga ! hawana hofu

Wanafeli jamani, tuwaambie wazi wanafeli na tunafeli kama Taifa

Vibaka wanapotishia Taifa, kuna tatizo, tumefeli! inasikitisha sana, tumefeli sana
 
  • Thanks
Reactions: BAK
..hata hapo mataa ya kamata nyerere road kuna vibaka mno....hapo relini....usiombe upate break down ya gari hapo usiku...lazima wakulize.....kuna wakati dada mmoja hapo kwenye mataa asubuhi sana akiwa garini alishangaa kupigwa bonge la jiwe usoni baada ya taa za kijani kuwaka akiwa kwenye mwendo...akakimbia na gari hivyo kwa panic midamu tele ikimtiririka usoni akaenda kusimama hapo mbele ya reli....hilo likawa kosa maana walikuwa wanamsubiri hapo vibaka...aliposimama tu kwa panic wakamvamia na kumsanua kila kitu garini....tumemkuta hapo akiwa hoi...inauma...
 
Back
Top Bottom