Dr Matola PhD
JF-Expert Member
- Oct 18, 2010
- 56,492
- 92,965
Ndugu wanajamvi,
Mimi huwa sina kawaida ya kuandika porojo hapa jamvini, jana kuna rafiki anaefanya kazi idara nyeti alinifata ili twend tukapate moja moto moja baridi,
Sasa kutokana na hali halisi ya jinsi tulivyopigika akanishauri twende FFU mase ukonga, ili tunywe laga za buku buku (extreme ) ndipo baada ya bia ya tatu vikaanza kupigwa ving'ora vikiwataka askari wote wa zamu na wale standby wakaripoti juu mara moja, juu maana yake ni kule base kwenye kulenga shabaha, huwezi kuamini mezani kwani nilikuwa na FFU watano ambao walikuwa standby lakini wote walikimbia na kutuomba tuhame kwenye Bar ya jeshi twende uraiani, basi tulivokuwa uraiani maongezi yao ilibidi nishtuke nakuanza kujiuliza sasa wale FFU wanaopigaga watu wanatokea nchi gani! mbona leo nipo kambini kwao lakini wengi hawakubaliani na amri za hovyo hovyo? na nilipowauliza kwamba hamtowajibishwa kwakutokuwepo base wakasema wao hawana nyumba za jeshi kwa hiyo wanakaa uraiani hivyo kuwa standby sio lazima wapatikane muda huo labda kama wangekuwa wanakaa kambini.
Baadae ndio tukapigiwa simu kumbe walikuwa wanakwenda kuwatuliza Chadema central polisi, basi askari wakasema hafadhari tulivyokimbia maana sisi wenyewe ni Chadema damu.
Mimi huwa sina kawaida ya kuandika porojo hapa jamvini, jana kuna rafiki anaefanya kazi idara nyeti alinifata ili twend tukapate moja moto moja baridi,
Sasa kutokana na hali halisi ya jinsi tulivyopigika akanishauri twende FFU mase ukonga, ili tunywe laga za buku buku (extreme ) ndipo baada ya bia ya tatu vikaanza kupigwa ving'ora vikiwataka askari wote wa zamu na wale standby wakaripoti juu mara moja, juu maana yake ni kule base kwenye kulenga shabaha, huwezi kuamini mezani kwani nilikuwa na FFU watano ambao walikuwa standby lakini wote walikimbia na kutuomba tuhame kwenye Bar ya jeshi twende uraiani, basi tulivokuwa uraiani maongezi yao ilibidi nishtuke nakuanza kujiuliza sasa wale FFU wanaopigaga watu wanatokea nchi gani! mbona leo nipo kambini kwao lakini wengi hawakubaliani na amri za hovyo hovyo? na nilipowauliza kwamba hamtowajibishwa kwakutokuwepo base wakasema wao hawana nyumba za jeshi kwa hiyo wanakaa uraiani hivyo kuwa standby sio lazima wapatikane muda huo labda kama wangekuwa wanakaa kambini.
Baadae ndio tukapigiwa simu kumbe walikuwa wanakwenda kuwatuliza Chadema central polisi, basi askari wakasema hafadhari tulivyokimbia maana sisi wenyewe ni Chadema damu.