Polisi waanza uchunguzi mauaji m/kiti CHADEMA Usa river

PISTO LERO

JF-Expert Member
Mar 8, 2011
2,819
1,454

UCHUNGUZI wa kifo cha Mwenyekiti wa Chadema, Kata ya Usa River, Msafiri Mwambo (32) umefanyika jana kwa kushirikisha, maofisa polisi na ndugu na jamaa wa marehemu , akiwapo Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki, Joshua Nassari.

Akizungumza na Mwananchi jana baada ya uchunguzi huo, Nassari alisema walitarajia taarifa ya kitaalamu ya chanzo cha kifo hicho ingetolewa jioni ili waanze taratibu za mazishi.

"Tupo hapa Mount Meru Hospitali, uchunguzi wa kifo cha Mwenyekiti wetu unaendelea na tunaimani tutapewa taarifa za kitaaluma kuhusu chanzo cha kifo chake,"alisema Nassari.

Nassari alisema wameamua uchunguzi wa kitaalamu ufanyike na taratibu za kisheria zifuatwe licha ya Mwambo kuonekana kwamba alikuwa amechinjwa kabla ya kufariki dunia.

Alisema baada ya uchunguzi huo ,walitarajia jana jioni kufanya kikao na wanafamilia ili kupanga taratibu za mazishi.

"Tutakuwa na kikao jioni na wanafamilia ili kupanga taratibu za mazishi leo (jana), nadhani baada ya hapo tutakuwa na maelezo zaidi,"alisema Nassari.

Katika hatua nyingine, aliyekuwa Meneja Mwenza wa Kampeni katika jimbo hilo, wakati wa uchaguzi, uliofanyika April Mosi, mwaka huu Vicent Nyerere na Mbunge wa Jimbo la Musoma Mjini amewasili jana mjini hapa kwa ajili ya taratibu za mazishi ya marehemu huyo.


Akizungumza na gazeti hili, Nyerere alisema ameamua kurejea Arumeru kuungana na wakazi wa jimbo hilo katika msiba huo kwa kuwa aliahidi katika kampeni kwamba watakuwa pamoja na wakazi wa jimbo hilo katika shida na raha.

"Muda huu naelekea msibani, kifo hiki kimetusikitisha sana"alisema Nyerere.

Mwenyekiti huyo, aliuawa juzi usiku kwa kuchinjwa na watu wasiojulikana baada ya kumpigia simu akiwa katika eneo la Mji Mwema akitazama taarifa ya habari.

Lakini muda mfupi baadaye alikutwa jirani na Shule ya Mukidoma akiwa amefariki dunia hata hivyo, wauwaji hao, waliondoka na simu yake pekee na kuiacha pikipiki aliyokuwa akiiendesha.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali (IGP), Said Mwema ameunda kikosi maalumu kinachoongozwa na Naibu Kamishina wa polisi, Isaya Mngulu kuchunguza kasi ya mashamba ya wawekezaji kuvamiwa na wananchi.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Arusha jana, Mngulu ambaye tayari timu yake imeanza kazi alisema pamoja na mambo mengine, watachunguza kiini cha matatizo ya uvamizi wa mashamba.

“Hivi tuanavyozungumza tayari maofisa wa vitengo mbalimbali kutoka makao makuu wako Arumeru kukusanya taarifa za kiintelijensia zitakazo saidia kutatua tatizo hili,” alisema Naibu Kamishina huyo.

Aliwataka wananchi wenye tatizo la ardhi kutumia njia sahihi kudai mashamba kutoka kwa viongozi na serikalini badala ya kuvamia mashamba yanayomilokiwa kihalali na wawekezaji.

KWA HISANI YA MWANANCHI

 

UCHUNGUZI wa kifo cha Mwenyekiti wa Chadema, Kata ya Usa River, Msafiri Mwambo (32) umefanyika jana kwa kushirikisha, maofisa polisi na ndugu na jamaa wa marehemu , akiwapo Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki, Joshua Nassari.

Akizungumza na Mwananchi jana baada ya uchunguzi huo, Nassari alisema walitarajia taarifa ya kitaalamu ya chanzo cha kifo hicho ingetolewa jioni ili waanze taratibu za mazishi.

"Tupo hapa Mount Meru Hospitali, uchunguzi wa kifo cha Mwenyekiti wetu unaendelea na tunaimani tutapewa taarifa za kitaaluma kuhusu chanzo cha kifo chake,"alisema Nassari.

Nassari alisema wameamua uchunguzi wa kitaalamu ufanyike na taratibu za kisheria zifuatwe licha ya Mwambo kuonekana kwamba alikuwa amechinjwa kabla ya kufariki dunia.

Alisema baada ya uchunguzi huo ,walitarajia jana jioni kufanya kikao na wanafamilia ili kupanga taratibu za mazishi.

"Tutakuwa na kikao jioni na wanafamilia ili kupanga taratibu za mazishi leo (jana), nadhani baada ya hapo tutakuwa na maelezo zaidi,"alisema Nassari.

Katika hatua nyingine, aliyekuwa Meneja Mwenza wa Kampeni katika jimbo hilo, wakati wa uchaguzi, uliofanyika April Mosi, mwaka huu Vicent Nyerere na Mbunge wa Jimbo la Musoma Mjini amewasili jana mjini hapa kwa ajili ya taratibu za mazishi ya marehemu huyo.


Akizungumza na gazeti hili, Nyerere alisema ameamua kurejea Arumeru kuungana na wakazi wa jimbo hilo katika msiba huo kwa kuwa aliahidi katika kampeni kwamba watakuwa pamoja na wakazi wa jimbo hilo katika shida na raha.

"Muda huu naelekea msibani, kifo hiki kimetusikitisha sana"alisema Nyerere.

Mwenyekiti huyo, aliuawa juzi usiku kwa kuchinjwa na watu wasiojulikana baada ya kumpigia simu akiwa katika eneo la Mji Mwema akitazama taarifa ya habari.

Lakini muda mfupi baadaye alikutwa jirani na Shule ya Mukidoma akiwa amefariki dunia hata hivyo, wauwaji hao, waliondoka na simu yake pekee na kuiacha pikipiki aliyokuwa akiiendesha.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Inspekta Jenerali (IGP), Said Mwema ameunda kikosi maalumu kinachoongozwa na Naibu Kamishina wa polisi, Isaya Mngulu kuchunguza kasi ya mashamba ya wawekezaji kuvamiwa na wananchi.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Arusha jana, Mngulu ambaye tayari timu yake imeanza kazi alisema pamoja na mambo mengine, watachunguza kiini cha matatizo ya uvamizi wa mashamba.

"Hivi tuanavyozungumza tayari maofisa wa vitengo mbalimbali kutoka makao makuu wako Arumeru kukusanya taarifa za kiintelijensia zitakazo saidia kutatua tatizo hili," alisema Naibu Kamishina huyo.

Aliwataka wananchi wenye tatizo la ardhi kutumia njia sahihi kudai mashamba kutoka kwa viongozi na serikalini badala ya kuvamia mashamba yanayomilokiwa kihalali na wawekezaji.

KWA HISANI YA MWANANCHI
Mwema na Intellijensia. Mashamba kuvamiwa ni muhimu kuliko kifo hiki!!GRRRRRRRRRRRRRRRRRRR!!!! tutaamka tu kufanya umma uchukue hatua wewe endeleza UMAGAMBA tu ya Mwanza hayajaisha bado unatuletea U@@S@$%e katika maisha ya ndugu zetu!!
 
Polisi wetu huwa wanahitimisha kwanza halafu ndo wanaanza uchunguzi kuthibitisha walichohitimisha awali. Mara baada ya tukio hili kutokea polisi walisema halihusiani na mambo ya kisiasa. Sijui walijuaje hata kabla hawajaanza uchunguzi. Nakumbuka hata ile issue ya songea ambapo watu walikuwa wakiuwawa polisi walitoa conclusion hata kabla uchunguzi haujafanywa. Huenda hii ndo style ya polisi wa TZ.
 
Polisi ni Wanafiki andekuwa balozi wa CCM hata Mbunge Nasari angekuwa Ndani, au kashahojiwa kama mara tatu hivi.... Lakini kwa kuwa ni CDM basi wanajivuta.

Polisi badilikeni, hali imeshabadilika maana hata mawaziri wanaotemeshwa kazi ni kutokana na nguvu ya Umma.
 
polic acheni kujidhalilisha kamateni wauaji hawa hata kama ni uvccm au nani akamatwe, siyo kuanza mazingaombwe yenu ya kirumba mwanza mnakose et mnaowakamata wandai hawakuhusika na ivo mnawaachia,...
 
poleni wancdm na familia yake kwa ujumla Mungu aiweke roho ya marehemu amina mahali pema peponi
 
Namba ya simu ya marehemu inajulikana kwanini hao wana wa intelijensi wasiichunguze kupitia kampuni ya simu aliyokuwa akitumia kujua ni nani aliyeongea na marehemu kwa wakati huo ili aweze kuisadia intelijensi kufanya kazi yake? badala ya kuja na jibu kuwa ni issue ya mashamba.
 
Namba ya simu ya marehemu inajulikana kwanini hao wana wa intelijensi wasiichunguze kupitia kampuni ya simu aliyokuwa akitumia kujua ni nani aliyeongea na marehemu kwa wakati huo ili aweze kuisadia intelijensi kufanya kazi yake? badala ya kuja na jibu kuwa ni issue ya mashamba.

Ikifika kesho bila mtu yoyote kukamatwa basi ujue polisi wanacheza. Walitakiwa hadi sasa wawe wamewahoji watu wote waliompigia simu marehemu dakika za mwisho. TCRA wangeweza kutoa number. Lakini siku ya 3 sasa wanapiga porojo hawa polisi.
 
Ni kweli inaweza kuangaliwa simu iliyompigia marehemu na polisi wakaweza kujua ni nani aliyempigia simu mara ya mwisho
 
Si kwamba hawa polisi hawajui ni wapi pa kuanzia uchunguzi wao ni kwa kuwa wanatimiza amri ya mwajiri wao mkuu (si raia)
 
Sasa naona polisi wanataka kualalisha mauaji kwa baadhi ya watu....hata syria kulianza hivi hivi
 
Inauma sana,siisahau tarehe 5 January ktk mauaji yaliyofanywa na polisi kwa makusudi.Ktk taarifa Yao walisema hao waliouwawa walikuwa wanavamia kituo cha polisi,wakaumbuka raia mmoja kati ya waliouwawa ni raia Wa Kenya na alikuwa ktk shughuli zake za kawaida na aliuwawa eneo la jogoo house mbali kabisa na kituo cha polisi.Ndio maana Lema aliposema waziri mkuu ni muongo Serikali ilipotezea hili jambo na hatujaona muendelezo wake.Nnasema polisi wanatumika vibaya kupoteza haki za raia,polisi wamekuwa mstari wa mbele kuvuruga utaratibu(uvunjifu Wa amani)bila kuwajibishwa na yeyote yule.Mfano mwingine ni kwa wabunge Wa Chadema kujeruhiwa vibaya kwa kukatwa na mapanga,ni nini polisi wamefanya zaidi ya kukutupuka mara tutamkamata Dkt Slaa na mengine Kama hayo.Polisi wamekuwa ni watu wa kukumbushwa majukumu yao kweli?Walijifunza nini ccp?Rushwa zimelijaa jeshi la polisi mwanzo mwisho.Tunaliomba jeshi la polisi litende haki sawa kwa raia yeyote bila kubagua.
 
Hivi Polisi wana wajibu wa kuchunguza au mpaka washanikizwe? Nilisikia kauli fulani hapo awali kuwa Polisi walidai hayakuwa mauaji ya kisiasa sasa kama ni hivyo walisubiri nini muda kuthibitisha hizo hisia/propaganda zao?

Miaka ile ya 90 tulisikia kwamba ni ccm tu ndio wanaoweza kuamua iwapo Tz ibaki na amani au la. Inawezekana ni kweli.
 
Polisi mkoani Arusha yaahidi kutoa sh m 10 kwa mtu atakayefanikisha kukamatwa kwa watu waliomuua m/kiti wa CDM; Msafiri Mwambo ktk kata ya USA River.
"Kifo hiki sio tu kimetustua, bali kimetugusa Polisi kwa sababu moja ya majukumu yetu ni kulinda mali na usalama wa wananchi. Tutafanya kila liwezekanalo kuwasaka na kuwatia mbaroni wote waliohusika na tukio hili la kinyama na tunaahidi kutoa sh M 10 kwa atakayesaidia wauaji kupatikana" Alisema Kamanda Andengenye.
Viongozi CDM wasisitiza Uharaka wa uchunguzi
 
KAMANDA wa Polisi Mkoa wa
Arusha, RPC Thobias Andengenye
ametoa ahadi ya jumla ya shilingi
za kitanzania milioni 10 kwa
mwananchi atakaewezesha
kupatikana kwa waliohusika na
mauaji ya kikatili kwa aliekuwa
Mwenyekiti wa CHADEMA Kata ya
Usa-River aliauwawa juzi Ijumaa.
Andengenye ameyasema hayo
wakati alipopewa nafasi ya
kuzungumza na wafiwa,
viongozi na wananchi wengine
katika sherehe za kuaga mwili
wa marehemu huyo zilizofanyika
katika uwanja wa Ngusero, Usa-
River kuanzia saa sita mchana
leo.
Akizungumza kwa niaba ya Jeshi
la Polisi, Kamanda Andengenye
alisema kuwa Jeshi lake lina
wajibu wa kulinda maisha na
mali za wananchi na hivyo
litafanya kila linalowezekana
kuhakikisha watuhumiwa wote
wanatiwa nguvuni.
Alitoa rai kwa wananchi wema
kutoa ushirikiano kwa Jeshi hilo
ili kuweza kufanikisha
kupatikana kwa wahalifu hao.
Kamanda Andengenye
aliambatana na viongozi
wengine wa Polisi akiwemo OCD
wa Wilaya ya Arumeru, OCD John.
Viongozi wengine wakubwa
waliopata nafasi kuzungumza
katika shughuli hiyo ya kutoa
heshima za mwisho walikuwa ni
Mkuu wa Wilaya ya Arumeu Mh
Mercy Silla, Mbunge wa Arumeru
Mashariki, Mh Joshua Nassari, na
Mbunge wa Musoma Mjini Mh
Vicent Nyerere.
Wengine ni mwakilishi wa
Kamati Kuu ya CHADEMA na
Mbunge wa Zamani Jimbo la
Arusha Mjini, Mh Godbless Lema,
Mbunge mpya wa CHADEMA viti
maalumu, Mh Cecilia Paresso
pamoja na mwakilishi wa chama
hicho Mkoa wa Kilimanjaro Mh
Basil Lema.
***
 
kwa hili Jeshi linaonyesha lipo serious na halipendi uhuni huu wanafahamu watoe taarifa tafadhari
 
kwa hili Jeshi linaonyesha lipo serious na halipendi uhuni huu wanafahamu watoe taarifa tafadhari

Lakini bado wataalamu wa intelejensia wanasema njia ni fupi tu kuwakamata wauaji hao 7bu kabla kabla hawajafanya unyama huo walimpigia cm kabla.
 
Na kuhusu kiwia na machemli watatoa sh ngapi kumjua aliowakata mapanga?
 
Back
Top Bottom