Polisi VS Majambazi

Mkaa Mweupe

JF-Expert Member
Jun 29, 2007
654
183
Katika siku za karibuni kumekuwa na habari mbalimbali zikiripotiwa kuwa Polisi wamefanikiwa kuyaua Majambazi kadhaa katika matukio ambayo yalisababisha kurushiana risasi.

Jambo linalonishangaza ni kuwa,
"Je, kunakuwa na ni nani hasa anatakiwa kuthibitisha maelezo yanayotolewa na Polisi?"

"Hivi inakuwaje ni Majambazi tu ndio wanauwawa na sio Polisi katika matukio ya kurushiana risasi?"

Nawasilisha.
 
Katika siku za karibuni kumekuwa na habari mbalimbali zikiripotiwa kuwa Polisi wamefanikiwa kuyaua Majambazi kadhaa katika matukio ambayo yalisababisha kurushiana risasi.

Jambo linalonishangaza ni kuwa,
"Je, kunakuwa na ni nani hasa anatakiwa kuthibitisha maelezo yanayotolewa na Polisi?"

"Hivi inakuwaje ni Majambazi tu ndio wanauwawa na sio Polisi katika matukio ya kurushiana risasi?"

Nawasilisha.
Kwahiyo ungependa Polisi wauwawe na majambazi sio?
 
Polisi ni Proffessionals wa kutumia silaha unlike majambazi, ambao mostly hawana hata mahala pa kujaribishia silaha zao, ndio sababu wanashindwa kupambana na polisi. Hakuna jibu zaidi ya hilo.
 
Kwa kuwa polisi wanakuwa wamejiandaa vema kwa tukio inakuwa rahisi kuwakabili majambazi. Wakishtukizwa mbona huwa wanakula kona mbaya?
 
Kwahiyo ungependa Polisi wauwawe na majambazi sio?

Nadhani mshkaji swali lake ni la kimsingi. Ni kwamba in most cases(mara nyingi) unakuta polisi ndo majambazi wenyewe....kwa mfano muulize Zombe na wafanyabiashara wake wa madini alivyowauwa na kuwapora na akashinda kesi kisanii na kifisadi.

Kinachotokea ni kuwa wakishakosa kuleta 10% mara baada ya kupiga issue, au ikitokea wamepiga kwa kigogo kimakosa, au polisi wamelaumiwa sana na vyombo vya habari, hapo ndipo baadhi yao hutolewa muhanga.

Kwa hiyo wanapoandaa kupiga kwa kuwa ni timu ileile, wanazungukana kimtindo, sasa wale wasiokuwa na upolisi halali ndo huwa matatani kwa hiyo wanapigwa shaba kwa mfano wakiwa ndo wanajiandaa pengine Buguruni, unakuta kama watano hivi wanauawa, halafu maiti zinapelekwa Amana Ilala ili kuzuga kuwa wanahitaji matibabu kwa watuhumiwa wa ujambazi ambao wako mahututi. Inakuwa confirmed kuwa wamekufa.

Taarifa ya habari sasa......Watuhumiwa wa Ujambazi watano wameuawa na polisi baada ya kurushiana risasi na polisi huko eneo la kimara baruti. Kamanda wa Polisi kanda maalumu amethibitisha tukio hilo..............

Lakini yako matukio mengine huwa hayatengenezwi na katika haya pande zote mbili huwa zinapata madhara. Majambazi, wengi wao wana mafunzo ya kijeshi kwa hiyo si rahisi watano wakauawa bila madhara hata kidogo kwa askari watatu waliopambana nao...ebo!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Nadhani mshkaji swali lake ni la kimsingi. Ni kwamba in most cases(mara nyingi) unakuta polisi ndo majambazi wenyewe....kwa mfano muulize Zombe na wafanyabiashara wake wa madini alivyowauwa na kuwapora na akashinda kesi kisanii na kifisadi.

Kinachotokea ni kuwa wakishakosa kuleta 10% mara baada ya kupiga issue, au ikitokea wamepiga kwa kigogo kimakosa, au polisi wamelaumiwa sana na vyombo vya habari, hapo ndipo baadhi yao hutolewa muhanga.

Kwa hiyo wanapoandaa kupiga kwa kuwa ni timu ileile, wanazungukana kimtindo, sasa wale wasiokuwa na upolisi halali ndo huwa matatani kwa hiyo wanapigwa shaba kwa mfano wakiwa ndo wanajiandaa pengine Buguruni, unakuta kama watano hivi wanauawa, halafu maiti zinapelekwa Amana Ilala ili kuzuga kuwa wanahitaji matibabu kwa watuhumiwa wa ujambazi ambao wako mahututi. Inakuwa confirmed kuwa wamekufa.

Taarifa ya habari sasa......Watuhumiwa wa Ujambazi watano wameuawa na polisi baada ya kurushiana risasi na polisi huko eneo la kimara baruti. Kamanda wa Polisi kanda maalumu amethibitisha tukio hilo..............

Lakini yako matukio mengine huwa hayatengenezwi na katika haya pande zote mbili huwa zinapata madhara. Majambazi, wengi wao wana mafunzo ya kijeshi kwa hiyo si rahisi watano wakauawa bila madhara hata kidogo kwa askari watatu waliopambana nao...ebo!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Duh! Mbona naona maruweruwe. Naomba urudie hii kwa Lugha rahisi.
 
Katika siku za karibuni kumekuwa na habari mbalimbali zikiripotiwa kuwa Polisi wamefanikiwa kuyaua Majambazi kadhaa katika matukio ambayo yalisababisha kurushiana risasi.

Jambo linalonishangaza ni kuwa,
"Je, kunakuwa na ni nani hasa anatakiwa kuthibitisha maelezo yanayotolewa na Polisi?"

"Hivi inakuwaje ni Majambazi tu ndio wanauwawa na sio Polisi katika matukio ya kurushiana risasi?"

Nawasilisha.

sasa ulitaka police wauawe? au nawewe ni ja....i? am sory
 
Hili suala hata mimi linanipa wasiwasi,majambazi wanafanya vibaya kuua watu,lakini polisi wasijisifie kuyaua majambazi kwani wanahalalisha sheria mkononi. Kama kuna uwezekano wa kuyakamata yakamatwe.
 
Hili suala hata mimi linanipa wasiwasi,majambazi wanafanya vibaya kuua watu,lakini polisi wasijisifie kuyaua majambazi kwani wanahalalisha sheria mkononi. Kama kuna uwezekano wa kuyakamata yakamatwe.

Jambazi ambaye kuna uhakika pasi shaka kuwa ni jambazi akikutwa kwenye tukio auawe tu, hakuna sababu ya kutupotezea muda wa wanasheria wetu kubishana bure mahakamani na jambo lililoko wazi. Shida ya hizi sheria ni kuwa hazitoi ile haki halisi, zinatoa hukumu kulingana na mabishano ya wanasheria, ambapo wakati mwingine jambazi huonekana hana hatia na kuachiwa huru, ilhali anayebambikiziwa kesi ya ubakaji hufungwa kifungo cha maisha!
 
polisi hawana haki ya kuua mtu wanayendhania ni majambazi , naomba tuelewe hili. Polisi wana uhakika gani 100% kuwa wanaowauwa ni majambazi? Kuuwa iwe ni in very exceptional cases isiwe ni kawaida na kama inatokea polisi inbidi wasikitikie kitendo hicho na sio kushangilia jamani.

Na kama watauwa basi wajisubmit wenyewe kwenye inquest ili ionekane kuwa polisi walikuwa justified kufanya hivyo na sio vinginevyo.
 
well the answer is simple, mapolisi most of the time wana wa outnumber majambazi na kama majambazi wakiwa wengi kuliko polisi, polisi hua hawa wa engage ktk fire fight, pili mapolisi wanakua wamejiposition vizuri kuliko majambazi na majambazi wanakua anxious kwani jinsi mda unavyoenda chance za wao kukamatwa zinaongezeka so wanamake ridicoulous move then they end up dead!
 
polisi hawana haki ya kuua mtu wanayendhania ni majambazi , naomba tuelewe hili. Polisi wana uhakika gani 100% kuwa wanaowauwa ni majambazi? Kuuwa iwe ni in very exceptional cases isiwe ni kawaida na kama inatokea polisi inbidi wasikitikie kitendo hicho na sio kushangilia jamani.

Na kama watauwa basi wajisubmit wenyewe kwenye inquest ili ionekane kuwa polisi walikuwa justified kufanya hivyo na sio vinginevyo.

Ukiwa polisi kwenye doria ukapata habari kuna ujambazi unatendeka, na ukifika kwenye tukio unakutana na watu wenye bunduki wanapambana na wewe, unahitaji uhakika gani tena kuwa hawa ni majambazi? Au benki inavamiwa majambazi wanaonekana kabisa wakirusha risasi hovyo kusambaratisha watu, unataka polisi watafute uhakika gani kwenye hali kama hii? Jambazi yuko mbele yako na SMG mtutu unatema kama mvua unataka polisi akamkamate, atamkamataje? Unacheza wewe! Jambazi auawe tu, hakuna kubembelezana. Watu wenye mawazo kama haya ya kwako mi nawaona mdebwedo tu.
 
This question is not easy as other people think.

No one is safe! I repeat kama hamjui polisi wanatakiwa kufanya nini msishabikie haya mambo. better know what polisi are supposed to be

unaweza kuzushiwa mwizi any time, unaweza ukapaki gari mtu akatilia mashaka na kuita polisi. hivi mnawajua polisi wanavyofanya kazi

I hate majambazi, lakini kuna sababu ya polisi kuji-equip their solution iswe kuua tu. some of them are innocent!

majamabazi wanaweza kumteka tax driver wakavamia sehemu polisi wanavyokuja tax driver naye anauawa!

wanachojitetea wao ni kuwa zana hafifu za kazi!

naona kuna majibu mapesi hapa kwa swali gumu
 
nadhani ni mambo ya timing ..
Tukio lililopita tuliona police mmoja aliumizwa vibaya kichwa chake na ilisadikika imeingia zaidi kwenye ubongo
 
This question is not easy as other people think.

No one is safe! I repeat kama hamjui polisi wanatakiwa kufanya nini msishabikie haya mambo. better know what polisi are supposed to be

unaweza kuzushiwa mwizi any time, unaweza ukapaki gari mtu akatilia mashaka na kuita polisi. hivi mnawajua polisi wanavyofanya kazi

I hate majambazi, lakini kuna sababu ya polisi kuji-equip their solution iswe kuua tu. some of them are innocent!

majamabazi wanaweza kumteka tax driver wakavamia sehemu polisi wanavyokuja tax driver naye anauawa!

wanachojitetea wao ni kuwa zana hafifu za kazi!

naona kuna majibu mapesi hapa kwa swali gumu

Naomba niongeze kidogo hapo. Kila mara utasikia makamanda kuwa 'Polisi walikuwa wakiwafuatilia majambazi na majambazi walipojua kuwa wanafuatiliwa walianza kutupa risasi na polisi wakajibu na katika mapambano hayo majambazi deshi deshi waliuawa"

/tujiulize, taarifa hii tumeishaisikia mara ngapi?

/inawezekana 'sinema' hii iwe inajirudia vile vile kila mara idadi kubwa ya majambazi inapouawa?

/ile kanuni ya askari kumpiga risasi mhalifu miguuni imeishia wapi?

/ina maana kuwa majambazi wetu sasa ni majasiri sana kiasi kwamba kila wanapogundua wanafuatiliwa na Polisi wanaamua kuanzisha mapambano ya risasi badala ya kutimua mbio na kuwaachia askari kazi ya kuwafukuza na kuwakamata kama ilivyokuwa zamani?

/katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita zaidi ya majambazi 25 wameawa kwa staili hii hii ya "walipogundua wanafuatwa na Polisi waliamua kuwatupia risasi Polisi ambao nao walijibu mapigo na katika mapambano hayo Polisi walifaulu kuua majambazi deshi deshi"

Hawa wanaouawa sio Viumbe wa ajabu waliotoka sayari ya Mars ama Pluto kuja kufanya uhalifu Tanzania. Ni ndugu zetu, jamaa zetu, marafiki zetu, wadogo zetu, waume wa watu, wababa wa watoto na kadhalika. Tunapaswa kujiuliza na kutafuta dawa ya kuzuia wao kupinda kushoto wakati jamii nzima inawenda kulia. Kamwe kutupiana risasi hakuwezi kuwa jawabu. Ni sawa na wale wanaosema adhabu ya mtu aliyeuwa ni kunyongwa.

Nakuunga mkono Waberoya. Tuumize vichwa vyetu kujiuliza badala ya kutafuta majibu mepesi kwa maswali mazito.
 
wakati mwingine majambazi nayo huwaga yanawaoteaga mapolisi...!
experience from songea , mwanza, ukerewe nk
 
Hili suala hata mimi linanipa wasiwasi,majambazi wanafanya vibaya kuua watu,lakini polisi wasijisifie kuyaua majambazi kwani wanahalalisha sheria mkononi. Kama kuna uwezekano wa kuyakamata yakamatwe.
nyie wote mnaowalaumu polisi kwa kuua majambazi mimi nashindwa kuwaelewa kabisa,au nyie mnaona raha mijambazi inavyoua watu kikatili bila hata huruma ukerewe yamefanyika mauaji ya kutisha na kila siku raia wema wasio na hatia wanauawa na mijambazi nyie mnaona raha,nahisi hamjawahi kukutana na ukatili wa majambazi na iko siku mungu atawapambanisha na majambazi ndio mtajua kama muwatetee au vinginevyo,hawa washenzi ni wakatili sana hongera saaaaaaaana jeshi la polisi mkilipata jambazi na mkadhibitisha kama ni jambazi hata kama mmelikamata likiwa hai pigeni risasi uwa kabisa washenzi hawa wasio na hata chembe ya ubinadamu,ila polisi wawe makini wasiingize ubinafsi na chuki katika mapambano haya,bravo jeshi la polis ueni kila jambazi mnalopambana nalo mkithibitisha kama ni jambazi fumua kichwa washenzi hawa wanataka kuifanya nchi hii kama haina serikali.
 
Hivi kuua ni rahisi kuzungumzia?tunazidi kudidimia kwenye unyama wa porini ama tunastaarabika?tukiruhusu jambazi liuwawe tunajenga precedence ya ajabu kuwa mtu akifumaniwa na mume/mke wa mtu atalambwa risasi mtaambiwa alirushiana risasi na polisi.land valuer wa arusha manispaa aliuliwa akisingiziwa jambazi huko moshi kwenye bar ya kwa rozi k.i.a. 2003/2004 ninyi acheni tu polisi ni wezi na wezi ni polisi na wanafahamiana vilivyo-this is a dark continent wajameni.take care of zombe and others
 
nyie wote mnaowalaumu polisi kwa kuua majambazi mimi nashindwa kuwaelewa kabisa,au nyie mnaona raha mijambazi inavyoua watu kikatili bila hata huruma ukerewe yamefanyika mauaji ya kutisha na kila siku raia wema wasio na hatia wanauawa na mijambazi nyie mnaona raha,nahisi hamjawahi kukutana na ukatili wa majambazi na iko siku mungu atawapambanisha na majambazi ndio mtajua kama muwatetee au vinginevyo,hawa washenzi ni wakatili sana hongera saaaaaaaana jeshi la polisi mkilipata jambazi na mkadhibitisha kama ni jambazi hata kama mmelikamata likiwa hai pigeni risasi uwa kabisa washenzi hawa wasio na hata chembe ya ubinadamu,ila polisi wawe makini wasiingize ubinafsi na chuki katika mapambano haya,bravo jeshi la polis ueni kila jambazi mnalopambana nalo mkithibitisha kama ni jambazi fumua kichwa washenzi hawa wanataka kuifanya nchi hii kama haina serikali.

...Mkuu, ndio maana tukasema tusitafute majibu mepesi kwa maswali mazito. Hakuna sentensi yoyote inayowalaumu Polisi kwa kuua Majambazi, lakini tunapaswa kuumiza vichwa kujiuliza kwamba je, hii ndio dawa??

Wewe unasema kuwa tusubiri siku tuingiliwe na majambazi ndipo tutakapojua uchungu wa Kuwatetea lakini Ongeza pia na kwamba na wewe subiri siku ndugu yako anapita mahali na katika kelele za mwizi! Mwizi! akakosewa na kutwangwa risasi ya kichwa kwa makosa!

Lakini pia tujiulize, mbona ujasiri huu wa kuwatwanga risasi za vichwa unakuja kwa majambazi ambayo mengine yanashukiwa tu na kuuawa hata kabla ya kufanya ujambazi wenyewe lakini Ujasiri huu hauonekani kwenye kuyatwanga risasi mijambazi iliyokubugu ambayo inaiba mabilioni na ambayo kila siku ushahidi wa Ujambazi wao unaanikwa sehemu kadhaa ikiwemo humu JF lakini hakuna anayechukua hatua bali kusuburi mwizi wa Kuku na kuondolea hasira zake hapo??

Tusitafute majibu mepesi kwa maswali magumu.
 
Back
Top Bottom