measkron
JF-Expert Member
- Apr 11, 2011
- 3,782
- 2,406
Wadau Leo nikiwa ndani ya bus kuelekea Dar es salaam, ndani ya bus kulikuwa na wazungu wapatao 8, ikiwa 6 walikuwa viti vya mbele na 2 walikuwa viti vya nyuma. Kufika maeneo ya Mombo Polisi walisimamisha gari na wakapanda ndani ya Gari mmoja akiwa na uniform na mwingine mwanadada amevalia nguo za kiraia. Wakasalimia abiria na mara aliyevaa nguo za kiraia moja kwa moja aliwafata abiria Wa kizungu na kuomba kuona hati zao za kusafiria, kulikuwa na wakenya 3, waganda 2 lakini kwa kuwa hawakuweza kujulikana kama ni raia Wa kigeni hawakuulizwa lolote. Askari aliyekuwa na uniform alikuwa akishika shika mifuko kwenye carrier..... Hivi kwa Ukaguzi huu wazungu tu ndio wanaoweza kuwa wahamiaji haramu?