Polisi singida wateka, watishia bunduki na kutaka kumlawiti mfanyabiashara

MADORO

Senior Member
Nov 12, 2011
198
117



SAKATA la ushuru wa kuku limeendelea kuchukua sura mpya,baada ya mfanyabiashara wa kuku 'kutekwa' na askari polisi sita na kupelekwa kwenye vichaka vilivyopo kando kando ya bwawa la Kindai nje kidogo ya mji wa Singida na kutishiwa kuawa kwa kupigwa risasi.

Mfanyabiashara huyo Ayubu Yussuph (28)amedai kuwa baada ya kufikisshwa kwenye eneo hilo la vichaka,aliteremshwa kutoka kwenye gari na kisha alikandamizwa na mdomo wa bunduki shingoni na kuamriwa kuvua shati na suruali.

Mfanyabiashara huyo ,Ayubu alisema siku ya tukio desemba mbili saa 4.00 asubuhi alikamatwa na askari hao akiwa nje ya mahakama ya Utemini walikokswenda kuwawekea dhamana wafanyabiashara wenzao.

Alisema akiwa na kaka yake mahakamani hapo.askari trafiki kwa jina anaitwa Eliudi alimwendea na kumwambia kuwa,jana yake alishiriki kumpiga na kumchania shati.

"Basi baada ya kunitupia lawama za uwongo, alinichukua na kuniambia kuwa ananipeleka kituo cha kati cha polisi kwa ajili ya kunifungulia mashitaka.Trafiki huyo akiwa na polisi wengine watano, walinipandisha kwenye gari lao na badala ya kunipeleka kituoni,walielekeza gari lao barabara ya kuelekea bwawa la Kindai",alisema.

Ayubu alisema walipofika Kindai,walimteremsha chini na kisha kumwingiza kwenye kichaka na kumkandamiza shingoni kwa mdomo wa bunduki. Polisi mwingine naye alimkandamiza kwa bundiki kwenye makalio yake, jirani na sehemu ya kutolea haja kubwa.

Mfanyabiashara huyo wa kuku za kienyeji,alisema kipindi chote hicho,alipambana nao vikali baada ya kubaini kuwa walitaka kumwingilia kimwili kinyume na maumbile kabla ya kumuuwa.

"Baada ya kuhangaishana nao kwa muda mrefu,askari hao walienda kuchota maji bwawani na kisha kunimwagia mwilini mwangu na wakaniambia eti tukifika kituoni,nieleze kuwa nimekamatwa ndani ya bwawa la Kindai baada ya kuwatoroka",

Tunaendelea kumtafuta RPC au RCO ili aeleze kinagaubaga suala hili tutawajuza wana JF kila kinachojiri. Hili ndio Jeshi la Usalama wa raia na mali zao.
 
hata ile kesi ya kumbambikia mfugaji na kumtoa upepo wa mil 9 haijesha wamezua nyingine.duh!
 
Jamani inasikitisha sana.Hawa policcm wamezidi ubabe na roho chafu.nimesoma hii story mpaka machozi yamenilenga
 
Baada ya kuhangaishana nao kwa muda mrefu,askari hao walienda kuchota maji bwawani na kisha kunimwagia mwilini mwangu na wakaniambia eti tukifika kituoni,nieleze kuwa nimekamatwa ndani ya bwawa la Kindai baada ya kuwatoroka",[/FONT][/COLOR][FONT="][/FONT]


hiri jeshi huwa narikubari sana
 
Kigoma walitesa mpaka wakaua na hawa tena. usalama gani wanalinda?
 
ndo faida ya kuwapa utawala wanamitindo(jk),hivi toka lini mzazi humwambia mwanae maneno yasofaa (mimba vihelehele,kula hadi uliwe, kasi zaidi, maisha bora tz,mwenye Richmond hamjui huku usivunje mkataba etc).Tuache ushabiki mfu tumwombe Rab atuonee huruma atujalie kupata viongozi sio watawala kama ilivyo sasa tz.Amina.
 



SAKATA la ushuru wa kuku limeendelea kuchukua sura mpya,baada ya mfanyabiashara wa kuku 'kutekwa' na askari polisi sita na kupelekwa kwenye vichaka vilivyopo kando kando ya bwawa la Kindai nje kidogo ya mji wa Singida na kutishiwa kuawa kwa kupigwa risasi.

Mfanyabiashara huyo Ayubu Yussuph (28)amedai kuwa baada ya kufikisshwa kwenye eneo hilo la vichaka,aliteremshwa kutoka kwenye gari na kisha alikandamizwa na mdomo wa bunduki shingoni na kuamriwa kuvua shati na suruali.

Mfanyabiashara huyo ,Ayubu alisema siku ya tukio desemba mbili saa 4.00 asubuhi alikamatwa na askari hao akiwa nje ya mahakama ya Utemini walikokswenda kuwawekea dhamana wafanyabiashara wenzao.

Alisema akiwa na kaka yake mahakamani hapo.askari trafiki kwa jina anaitwa Eliudi alimwendea na kumwambia kuwa,jana yake alishiriki kumpiga na kumchania shati.

"Basi baada ya kunitupia lawama za uwongo, alinichukua na kuniambia kuwa ananipeleka kituo cha kati cha polisi kwa ajili ya kunifungulia mashitaka.Trafiki huyo akiwa na polisi wengine watano, walinipandisha kwenye gari lao na badala ya kunipeleka kituoni,walielekeza gari lao barabara ya kuelekea bwawa la Kindai",alisema.

Ayubu alisema walipofika Kindai,walimteremsha chini na kisha kumwingiza kwenye kichaka na kumkandamiza shingoni kwa mdomo wa bunduki. Polisi mwingine naye alimkandamiza kwa bundiki kwenye makalio yake, jirani na sehemu ya kutolea haja kubwa.

Mfanyabiashara huyo wa kuku za kienyeji,alisema kipindi chote hicho,alipambana nao vikali baada ya kubaini kuwa walitaka kumwingilia kimwili kinyume na maumbile kabla ya kumuuwa.

"Baada ya kuhangaishana nao kwa muda mrefu,askari hao walienda kuchota maji bwawani na kisha kunimwagia mwilini mwangu na wakaniambia eti tukifika kituoni,nieleze kuwa nimekamatwa ndani ya bwawa la Kindai baada ya kuwatoroka",

Tunaendelea kumtafuta RPC au RCO ili aeleze kinagaubaga suala hili tutawajuza wana JF kila kinachojiri. Hili ndio Jeshi la Usalama wa raia na mali zao.

Mo Dewji mbunge wenu mme mkonsati?Hope hii incident iko jimboni kwake maana kwa Lisu hawawezi kufanya huu upuuzi hao policcm
 
Polisi Singida toeni maelezo mazuri, toka Mahakamani ya Utemini mpaka kituo cha polisi ni Kilometa mbili, tuambieni ilikuwaje mtuhumiwa huyu alifikishwa amelowana, hakukuwepo mvua siku hiyo, mlimchukua mahakamani mbele ya watu wengi, mlimfikisha kituoni amelowana, mlimpeleka Kindai kufanya nini? Kwanini mnataka kulawiti hamjaoa? IGP fuatilia sakata hili, linachukiza.
 
Ushuru wa kuku???
serikali ya kikwete inakusanya ushuru wa kuku???? kweliiii!!!!
 
Hii habari haipo kwenye jukwaa husika! Inatuchafulia jukwaa letu la siasa.
 
Tunakoelekea uaminifu kwa Polic utaisha kabisa nakuja kubaki kila mtu na maamuzi yake peke yake na baadae yale ya rwanda yatufikie kwani mateso raia wanayopata watavumilia na mwisho wake uvumilivu utaisha na ukiisha kila aina ya baya litatokea. My take serikali mmwe waangalifu sana ktk kuwawajibisha hawa polic wanaofanya haya mambo kwani haya mambo yakiendelea yatakoma na mwisho wake itajakuwa ngumu kukabiliana nayo
 
Polisi wa Usalama wa barabarani na ushuru wa kuku vina uhusiano gani? Bahati mbaya Askari hawa walikata gari wakalipeleka kwenye ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa. Je Huko ndio Kituo cha Polisi? Polisi (TRAFIC) wameanza lini kukamata magari na kuyahifadhi kwa wakurugenzi wa Manispaa. Singida mjini jutieni uamuzi wenu wa kuchagua mbunge ambaye hajui matatizo yenu, mlikimbilia elfu kumi za Dewji, sasa mnatozwa ushuru wa vibanda kinyume cha utaratibu, ardhi inauzwa na Mkuu wa Mkoa, anajichukulia tenda zote hata kama hana sifa, na Polisi wameamua kujitafutia ulaji kwa njia ya kukusanya ushuru wa kuku. Singida mjini shamba la Bibi kila mmoja anakula anavyoweza kuwahi. Ila polisi wamefanya vibaya sana kutaka kumlawiti mfanyabiashara huyu. Ukatili wa polisi hawa jamani...Mhhhh
 
Mo Dewji mbunge wenu mme mkonsati?Hope hii incident iko jimboni kwake maana kwa Lisu hawawezi kufanya huu upuuzi hao policcm

hawa askari washenzi kweli mpaka kubaka sasa mi nadhani ni wakati wawa na nchi kuchukua hatua mkononi huu ni ushenzi na ubakaji.
 



SAKATA la ushuru wa kuku limeendelea kuchukua sura mpya,baada ya mfanyabiashara wa kuku 'kutekwa' na askari polisi sita na kupelekwa kwenye vichaka vilivyopo kando kando ya bwawa la Kindai nje kidogo ya mji wa Singida na kutishiwa kuawa kwa kupigwa risasi.

Mfanyabiashara huyo Ayubu Yussuph (28)amedai kuwa baada ya kufikisshwa kwenye eneo hilo la vichaka,aliteremshwa kutoka kwenye gari na kisha alikandamizwa na mdomo wa bunduki shingoni na kuamriwa kuvua shati na suruali.

Mfanyabiashara huyo ,Ayubu alisema siku ya tukio desemba mbili saa 4.00 asubuhi alikamatwa na askari hao akiwa nje ya mahakama ya Utemini walikokswenda kuwawekea dhamana wafanyabiashara wenzao.

Alisema akiwa na kaka yake mahakamani hapo.askari trafiki kwa jina anaitwa Eliudi alimwendea na kumwambia kuwa,jana yake alishiriki kumpiga na kumchania shati.

"Basi baada ya kunitupia lawama za uwongo, alinichukua na kuniambia kuwa ananipeleka kituo cha kati cha polisi kwa ajili ya kunifungulia mashitaka.Trafiki huyo akiwa na polisi wengine watano, walinipandisha kwenye gari lao na badala ya kunipeleka kituoni,walielekeza gari lao barabara ya kuelekea bwawa la Kindai",alisema.

Ayubu alisema walipofika Kindai,walimteremsha chini na kisha kumwingiza kwenye kichaka na kumkandamiza shingoni kwa mdomo wa bunduki. Polisi mwingine naye alimkandamiza kwa bundiki kwenye makalio yake, jirani na sehemu ya kutolea haja kubwa.

Mfanyabiashara huyo wa kuku za kienyeji,alisema kipindi chote hicho,alipambana nao vikali baada ya kubaini kuwa walitaka kumwingilia kimwili kinyume na maumbile kabla ya kumuuwa.

"Baada ya kuhangaishana nao kwa muda mrefu,askari hao walienda kuchota maji bwawani na kisha kunimwagia mwilini mwangu na wakaniambia eti tukifika kituoni,nieleze kuwa nimekamatwa ndani ya bwawa la Kindai baada ya kuwatoroka",

Tunaendelea kumtafuta RPC au RCO ili aeleze kinagaubaga suala hili tutawajuza wana JF kila kinachojiri. Hili ndio Jeshi la Usalama wa raia na mali zao.
Haingii akilini, askari 6 wakiwa na silaha na nia ya kumfanyia mtu mmoja kitu mbaya halafu utuambie eti jamaa alikukuruka mpaka askari wakashindwa kumfanyia kitu! Hadithi hii inaonyesha kuna kitu kimefichwa nyuma ya pazia au ni moja kati simulizi tu. Paukwa pakawa eeenh?. Au mna bifu na baadhi ya askari? Tupe ukweli.
 
kweli hii ndiyo sura halisi ya jeshi letu la polisi! Tunaomba sheria ichukue mkondo wake.
 
Back
Top Bottom