Kite Munganga
Platinum Member
- Nov 19, 2006
- 1,773
- 952
Tarehe 15 usiku palitokea ujambazi wa kiaina katika kumbi mbili Igunga ambazo zina Guest House na wateja wakaibiwa fedha nyingi tu na mali zingenezo, sasa mazingaombwe yalianza kesho yake tarehe 16/11/08 ambapo mwaathirika wa ujambazi huo alipomtambua na kutoa taarifa kuwa kati ya majambazi yale mmoja alikuwa ni askari Polisi wa hapo hapo Igunga anayeitwa "Mwaka" ndiye aliyekuwa ameshika Bunduki kwenye tukio siku hiyo, OCS akishirikiana na askari wa upelelezi Manda kwa harakaharaka wakatuma Askari kuanzisha kamatakamata mjini hasa ikilenga wazururaji na wageni na kuwaunganisha na kesi ya ujambazi huo huku wakimwacha askari wao bila kumfungulia mashtaka au kufanya upelelezi kama kweli alihusika au la, Kwa wenyeji wa Igunga wanadai kuwa wanahisi kuwa ujambazi huo ulipangwa na Polisi kwani sio kawaida kabisa Polisi kukosa kufanya doria sehemu hizo siku za week-end na inazidi kutia mashaka kwa hao wazurulaji kupelekwa mahakamani kesho yake tarehe 17 wakidaiwa kuwa ndio waliotenda kosa hilo huku Polisi aliyetajwa akiachwa huru huria mtaani lakini akiwa kasimamishwa kazi, kinachofanywa ni wale vijana wabebe kesi na Polisi isihusishwe kabisa na matukio ya siku hiyo ili kuficha uchafu ulio ndani ya Polisi wetu wa Igunga, mwisho napenda mtu mwenye namba za IGP Mwema au RPC wa Tabora ili nikomae nao, pia si vibaya nikipata namba za wakili yeyote aliyeko Tabora