Kiranja Mkuu
JF-Expert Member
- Feb 18, 2010
- 4,066
- 4,085
Nikiwa naenda kazini kwa kutumia daladala, mara akapanda askari polisi, gari ilikuwa na nafasi kadhaa za kukaa, na miongoni mwa nafasi hizo ni nafasi iliyokuwepo jirani na nilipokaa.
Baada ya kituo kimoja tokea alipopandia, akatoa kipisi cha sigara kutoka kwenye mfuko wake wa shati, akakiwasha na kuanza kukivuta.
Abiria na wqahudumu wa daladala tulimsihi azime kwa kuwa anahatarisha afya zetu, akagoma na akawa akiporomosha matusi kwa sauti ya ulevi.
Nimekereka kwelikweli, na nimeamua kuteremka kwenye hilo gari kabla sijafika kule niendako.
Kweli Tanzania hamna polisi, ila yunifomu za polisi
Baada ya kituo kimoja tokea alipopandia, akatoa kipisi cha sigara kutoka kwenye mfuko wake wa shati, akakiwasha na kuanza kukivuta.
Abiria na wqahudumu wa daladala tulimsihi azime kwa kuwa anahatarisha afya zetu, akagoma na akawa akiporomosha matusi kwa sauti ya ulevi.
Nimekereka kwelikweli, na nimeamua kuteremka kwenye hilo gari kabla sijafika kule niendako.
Kweli Tanzania hamna polisi, ila yunifomu za polisi