OMUSILANGA
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 384
- 227
Ndiyo wakuu! Katika hali ya kuendelea kutapatapa kwa serikali ya ccm wakati miti yote inateleza , imejitokeza tena leo ktk wila ya ya Rorya baada ya polisccm kuzuia mkutano wa hadhara wa cdm ktk kata ya Nyathorongo kwa kisingizio cha mgomo wa walimu. Mikutano hii ni operation inayo endelea jimboni Rorya ktk kuendeleza harakati na kutoa elimu ya uraia kwa wananchi chini ya uratibu wa Kamanda Odelo Odelo pamoja na wapiganaji wengine. Kutapatapa huku mara ohoo! Suala liko mahakamani, kufunga magazeti (mwanahalis) pamoja na vitisho kamwe si suluhu kuelekea Tanzania tuitakayo. Waungwana wanasema "SIKU MJINGA AKIJITAMBUA, MWEREVU YUPO MATATANI ". Pamoja sana makamanda,mpaka kieleweke.