Wakuu,
Nimeshangazwa na kitendo cha askari mmoja jijini Mwanza mwenye cheo cha Konstebo kuwapa wanafunzi bunduki kisha kupiga picha wakiwa wamebeba silaha hiyo kwa kupokezana huku wengine wakiwa wameishika mithili ya askari walioko kwenye mafunzo ya kulenga shabaha.
Kitendo hicho kilitokea juzi kwenye shule ya msingi Tambukareli iliyoko kata ya Butimba jijini Mwanza mara baada ya wanafunzi hao kumaliza mitihani yao ya darasa la saba.
Binafsi nimeziona picha hizo huku askari huyo akiwa amesimama pembeni huku akiwa amelegeza macho hali ambayo kwa haraka haraka unaweza kusema huenda alikuwa ametumia sigara kubwa. Ninavyofahamu mimi, askari haruhusiwi kutoa silaha kwa mtu awaye yote.
Wakuu, kumekuwapo matukio mengi ya Polisi kutumia silaha ovyo na kusababisha mauaji ya raia wasio na hatia. Je, kitendo cha askari kutoa silaha kwa wanafunzi na kupiga nayo picha, yaweza kuwa moja ya uthibitisho kuwa baadhi yao wanatumia sigara kubwa na kuna umuhimu wa kupimwa akili kabla ya kuajiriwa kwenye vyombo vyetu vya ulinzi na usalama? Tujadiri kwa hoja.
Nimeshangazwa na kitendo cha askari mmoja jijini Mwanza mwenye cheo cha Konstebo kuwapa wanafunzi bunduki kisha kupiga picha wakiwa wamebeba silaha hiyo kwa kupokezana huku wengine wakiwa wameishika mithili ya askari walioko kwenye mafunzo ya kulenga shabaha.
Kitendo hicho kilitokea juzi kwenye shule ya msingi Tambukareli iliyoko kata ya Butimba jijini Mwanza mara baada ya wanafunzi hao kumaliza mitihani yao ya darasa la saba.
Binafsi nimeziona picha hizo huku askari huyo akiwa amesimama pembeni huku akiwa amelegeza macho hali ambayo kwa haraka haraka unaweza kusema huenda alikuwa ametumia sigara kubwa. Ninavyofahamu mimi, askari haruhusiwi kutoa silaha kwa mtu awaye yote.
Wakuu, kumekuwapo matukio mengi ya Polisi kutumia silaha ovyo na kusababisha mauaji ya raia wasio na hatia. Je, kitendo cha askari kutoa silaha kwa wanafunzi na kupiga nayo picha, yaweza kuwa moja ya uthibitisho kuwa baadhi yao wanatumia sigara kubwa na kuna umuhimu wa kupimwa akili kabla ya kuajiriwa kwenye vyombo vyetu vya ulinzi na usalama? Tujadiri kwa hoja.