Msema hovyo
Senior Member
- Jul 3, 2011
- 195
- 86
Hawa akina mama wanatumia zaidi ya masaa matatu hadi manne kuchanja kuni huko maporini, na wanajiweka katika hatari ya kuumwa na nyoka. Lakini zaidi ya yote, wanakata miti iliyo kwenye chanzo cha maji jambo ambalo linachangia sana kuharibu mazingira na kusababisha ukosefu wa maji kwenye mabwawa ya kuzalishia umeme. Wakati hawa akina mama wakikata kuni, wababa upande wa pili wanachoma mkaa, kuzidisha athari ya uharibifu wa mazingira.
Lakini tukumbuke kwamba gesi inazalishwa pale Mtwara, nchini tanzania, si ya kununua kutoka nje. Kama tungesambaza gesi nchi nzima na kwa bei rahisi, hakuna mtu angekata kuni wala kuchoma mkaa. Kwa kufanya hivyo tungetunza mazingira, tungeokoa muda unaotumika na hawa kina mama kuchanja kuni, tungewaokoa na hatari ya kujikata au kuumwa na nyoka, na zaidi sana tungepunguza gharama ya maisha kwa watanzania walio wengi ambao wanategemea sana mkaa na mafuta kwa ajili ya kupikia. Lakini kwa kuwa watanzania na hasa hawa akina mama maskini, ndiyo waliochagua CCM, basi hawana budi kula jeuri yao. Poleni sana kina mama, next time msiipe kura CCM.