Anyisile Obheli
JF-Expert Member
- Dec 13, 2009
- 3,398
- 319
Pole shekh Yahya,
Uso kuwa na haya,
Na utabiri mbaya,
Ulojaa mabaya.
Umejiweka mtukufu,
Na huna utakatifu,
Una mawazo mafu,
Tena toka kwa wafu.
Unatuletea ya kuzimu,
Tuso abudu mizimu,
Umetufanya wazimu,
Na wenye fikra adimu.
Elimu yako ya kijini,
Waitangaza nchini,
Kuturudisha chini,
Na mambo ya kifirauni.
Ole tena ole,
Mungu atoa ole,
Usipoiogopa ole,
Hutaipata pole.
Na dini hayafanani,
Uletayo hadharani,
Maamuma wafundisheni,
Usituletee wanazuoni.
Uso kuwa na haya,
Na utabiri mbaya,
Ulojaa mabaya.
Umejiweka mtukufu,
Na huna utakatifu,
Una mawazo mafu,
Tena toka kwa wafu.
Unatuletea ya kuzimu,
Tuso abudu mizimu,
Umetufanya wazimu,
Na wenye fikra adimu.
Elimu yako ya kijini,
Waitangaza nchini,
Kuturudisha chini,
Na mambo ya kifirauni.
Ole tena ole,
Mungu atoa ole,
Usipoiogopa ole,
Hutaipata pole.
Na dini hayafanani,
Uletayo hadharani,
Maamuma wafundisheni,
Usituletee wanazuoni.