The secretary
JF-Expert Member
- Jan 14, 2012
- 4,149
- 2,536
naomba kujua dalili na visababishi na first aid kabla ya kufika hospital
hilo sio tatizo la dharula maana huanza taratibu na matokeo yake huonekana kikubwa nikwenda hospital unapoona dalili zake
naomba kujua dalili na visababishi na first aid kabla ya kufika hospital
Pneumonia ni ugonjwa unaotokana na maambukizi ktk mapafu(yanaweza kuwa yote au moja).Husabishwa na bacteria,virusi au hata fangasi.Dalili zinahusisha kukohozi chenye makoozi,mafua,homa,kupumulia ndani(breathing in) ambayo huambatana na sauti zisizo za kawaida kufuani n.k.Hili sio tatizo la dharura nenda hospitali watachukua makohozi(sputum culture) au kitu kinaitwa pleural effusion,ikithibitika matibabu yataanza.
Ngahekapahi naona umefika mbali saana....Pneumonia ni ugonjwa unaowapata both watoto na watu wazima, sina hakika unaongelea kwa group gani sasa, maana baadhi ya dalili zaweza tofautiana.
Naomba niongelee kwa watoto (mimi ni mdau mkubwa wa afya za watoto). Pneumonia kwa watoto ni ugonjwa simple sana (lakini unaongoza kwa kuua) ambao wala hauhitaji ujuzi mwingi na test sophisticated kuugundua na kutoa matibabu husika. Dalili kubwa kwa watoto ni kikohozi, na/au mafua, na/au homa, na kupumua kwa shida na/au haraka. Daktari atamchunguza kwa kuhesabu idadi yake ya pumzi kwa dakika, kama imevuka kiwango cha kawaida basi ni Pneumonia. Daktari pia anaweza msikiliza mtoto kifua kwa stethoscope na kusikia crepitations.
Udharura wa Pneumonia unakuja kama ni Pneumonia kali (kuna vigezo vya kusema hivyo)...mara nyingi hakuna first aid unayoweza kutoa nyumbani zaidi ya kumuwaisha mtoto hospitali akapate huduma husika. Pneumonia sasa hivi inaua watoto wengi zaidi hata ya Malaria.
NB:
Sputum Culture ni kipimo ambacho unatoa makohozi ili kutambua ni vijidudu gani (microbacteria) wamesababisha hiyo Pneumonia, mara nyingi hufanyika kwa Pneumonia Sugu na/au Tuberculosis.
Pleural Effusion ni complication ya Pneumonia pale inapoendelea kiasi cha mapafu kujaa maji kwenye pleural cavity...hii ni complication late sana ya Pneumonia sugu au Tuberculosis, na hayo maji maji yanaweza kutolewa kwa sindano ili kupima kujua ni vijidudu gani vinasababisha.