mtamanyali
JF-Expert Member
- Dec 6, 2011
- 1,161
- 613
kwa sasa sina waziri wala raisi, nitawachagua 2015.
jibu hili litamkost sana Pinda na ccm kwa ujumla,Na nampongeza sana F.Mbowe kwa kuulizj swali hili
bullet nimesikia katika taarifa ya habari kuwa Mh jaji Walioba kawapiga marufuku RC Na DC kuhudhuria vikao vya maoni ya katiba inawezekana walishaanza kutumia uwezo wao wakuhakikisha ccm inatawala mileleHivi hawa ma RC na DC si ndio Anna Kilalgo aliwatetea kuwa wawemo katika uratibu wa katiba mpya? Fikiria sasa ni upendeleo kiasi gani kwa CCM watakao uonyesha! Vyeo hivi vifutwe kabisa ndani ya katiba
Sio Wenje aliyeuliza?
Kwa kauli ya Pinda ina maana kwamba kuanzia usalama wa taifa, polisi, jeshi, mahakama vipo kuhukikisha ccm inatawala milele huku wakitumia pesa ya watanzania?, huo ni upumbavu uliopita kiasi.
juzi tu kwenye semina ya wakuu wa wilaya na mkoa jk alisema hivi '' ninyi wakuu wa wilaya na miko ni wafanya kazi wa serikali fanyeni kazi na acheni kufanya siasa'' wakati anasema hayo pinda nae alikuwa yupo ....leo hii pinda anaropoka kivyake....
Pasco mimi sikukiona, ila sishangai, mimi ni mwanachama haswa wa CCM, na hili ndilo tatizo kubwa la hawa viongozi wa "Serikali" wanaoingia madarakani kwa tiketi ya CCM, na CCM inaonekana kituko kwa tabia hii sijui kama wanasoma alama za nyakati.
Watu ni waelewa kupita maelezo, na hasa kundi hili kubwa mno la vijana wanaoelimishwa na darasa la ulimwengu kupitia media ambayo kila mtu anai-access.Kauli hizo zilifaa kipindi kile tunaingia kwenye vyama vingi.
Kutoa agizo la kuhakikisha wanashinda bila kutoa muongozo na kusisitiza misingi itakayowafanya washinde itapelekea muendelezo wa mbinu chafu za kijinga zinazokiletea chama aibu kila siku.
Hawa wanatugawa sijui kama wanajitambua, kwakuwa wanadhani wao ni CCM na wengine si wao wakati madaraka waliyonayo yanapaswa kuwa ya kuwatumikia watu wote bila ubaguzi wowote na hata kauli zao zisimame katka misingi hiyo.
Kauli kama hiyo alitakiwa atoe katibu Wilson au Nape kwa wadhifa wake. Mnakitia doa chama, na ndiyo mnakipeleka pabaya, hebu rejeeni misingi ya CCM mwanzo kabisa mwa katiba, yaani hiyo peke yake mkiihubiri, kwa vitendo, ni vigumu chama kingine kuwayumbisha. Mh Pinda, please!
Pinda ametuthibitishia kuwa nchi yetu ina tatizo.
DC/RC wana mamlaka juu ya mahakimu wa wilaya mikoa kwa mujibu sheria iliyotungwa mwaka jana iliyolalamikiwa sana na Lissu
DC/RC ni wenyevitii wa kamati ya ulinzi na usalama inayompa mamlaka ya kuagiza polisi kufanya jambo lolote ikiwepo kumkamata mtu ye yote.
DC/RC ni msemaji wa mwisho wilayani hata msimamizi wa uchaguzi wa wilayani (mkurugenzi) yuko chini yake. Japo wana majukumu tofauti. je, haki itatendeka?
Sasa mkanganyiko huu + kauli ya Pinda unapata nini kama siyo vurugu.
bullet nimesikia katika taarifa ya habari kuwa Mh jaji Walioba kawapiga marufuku RC Na DC kuhudhuria vikao vya maoni ya katiba inawezekana walishaanza kutumia uwezo wao wakuhakikisha ccm inatawala milele