Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,467
- 113,570
Wanabodi,
Kila nipatapo fursa, sipendi kabisa kukosa kipindi cha Maswali na Majibu ya Papo kwa Papo kwa Waziri Mkuu Bungeni, ambapo Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo, Kayanza, Peter Pinda, hujibu maswali ya papo kwa papo, ile leo nilikikosa kipindi hiki.
Lakini kupitia taarifa za habari, nimemsikia Mhe. Pinda, akisema kuwa ni jukumu la wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya kuhakikisha CCM inashinda chaguzi zote ili CCM iendelee kutawala milele!.
Naombeni wajuzi wa masuala ya utawala, mnirekebishe if I'm wrong!, kuanzia kwa rais JK na wanasiasa wengine wote ambao japo wamechaguliwa kwa tiketi tuu za vyama vyao vya siasa, lakini walio wachagua sio wanachama wa vyama vyao tuu, bali wamechaguliwa na umma wa Watanzania wote kwa ujumla wetu, rais, mbunge, diwani au wenyeviti wa mitaa, ukiishaguliwa, japo unabaki kuwa mwanachama wa chama chako lakini unageuka ni mtumishi wa umma, paid by taxpayers money, jukumu lako kuu sasa ni kuutumikia umma ambao chama chako ni sehemu ya umma huo na sio kukitumikia chama chako!.
Hii inamaanisha rais JK, japo ameshinda kwa tiketi ya CCM, kuongoza serikali ya JMT, kwa kutumia ilani ya uchaguzi ya CCM, ambapo kwa wakati huo huo yeye ndiye Mwenyekiti wa CCM, hakuchaguliwa na wana CCM pekee, amechaguliwa na Watanzania wote kwa ujumla wetu kuiongoza Tanzania na Watanzania na sio amechaguliwa na wana CCM, kuongoza serikali ya CCM kwa ajili ya wana CCM pekee!, hapana!, JK na serikali yake, japo ni CCM, lakini amechaguliwa kuongoza serikali ya Tanzania kwa niaba ya Watanzania wote na kwa manufaa ya Watanzania wote, wakiwemo watu wa vyama vingine vyote vilivyopo kisheria kwa mujibu wa katiba na sio kwa manufaa ya wana CCM!. (Of the people, by the people and for the people), hivyo hili la viongozi wa umma kutakiwa kuhakikisha CCM inatawala milele, kusema ukweli, mimi linanitatiza!.
JK ndiye rais wa Chadema, ndiye rais wa CUF na ndiye rais wa wote wenye vyama na wasio na vyama. Yeye ndiye rais wa Dr. Slaa, yeye ndiye rais wa Prof. Lipumba, yeye ndiye rais wetu sisi wote kama Watanzania, ni rais wa waliomchagua na pia rais wa wasiomchagua, anatakiwa kufanya kazi kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa kwanza na sio maslahi ya chama chake cha CCM!.
Kauli ya Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda bungeni leo kuwa Wakuu wa wilaya na mikoa, wako pale kuhakikisha CCM inashinda chaguzi zote ili itawale milele, haiwezi kupita bila kupingwa!. Hi inamaanisha kuwa viongozi hawa, wako kwa ajili ya kuilinda na kuitetea status quo ya CCM ili iendelee kutawala milele!. Kwa maoni yangu, this is very wrong kwa tafsiri sahihi ya Public Servants!. Kwa kauli hii ya Pinda, it goes without saying kuwa wakuu wa majeshi yetu, Polisi wetu, mahakama zetu na wakuu na vyombo vya dola, na vyombo vya kiserikali, wanateuliwa ili wahakikishe CCM haishindwi na inaendelea kutawala milele!.
Public Servant, ni mtumishi wa umma, ma RC na ma DC ni viongozi wa serikali, kwa maana hiyo ni viongozi wa umma, na watatimiza majukumu yao kwa maslahi ya umma na sio kwa maslahi ya CCM. Ndio maana Mhe. Tundu lissu aliwakataa hawa wasihusishwe ile tume ya katiba na juzi akasisitizwa hawapaswi kuwamo bungeni!.
Hata wabunge wa kuchaguliwa, ni watumishi wa umma, japo wanateuliwa kwa tiketi za vyama vya siasa, wanachaguliwa na wananchi na sio na vyama vyao, hivyo wakishashinda ubunge, wanakuwa ni watumishi wa watu na sio watumishi wa vyama vyao, hivyo wanapaswa kutekeleza majukumu yao ya kibunge kwa maslahi ya wananchi na sio kwa maslahi ya vyama vyao!. Kama ni kweli, majukumu ya ma RC na ma DC ni kuhakikisha CCM haishindwi, hii ina maana kubwa zaidi katika mustakabali wa mabadiliko halali ya serikali!.
Binafsi yangu, nimesikitishwa na kauli hiyo, and to be honest, nilikuwa na very high hopes kuhusu Pinda, kuelekea 2015! lakini sasa nimeamini Pinda pia ni wale wale!. Kwa vile CCM ni chama tawala, hivyo public servants wana jukumu la kuhakikisha CCM inashinda na kutawala milele!.
Hii inamaanisha hata kama 2015, Watanzania wataamua kuivote out CCM kupitia njia halali ya ballot box, hao public servants wenye jukumu la kuitumikia serikali mpya ya chama kitakachoshinda, tayari wako kwenye mind set ya chama kimoja kuhakikisha lazima CCM inashinda!, na jee ikitokea CCM ikashindwa kweli, jee watakabidhi madaraka kwa mshindi halali?!, jee majukumu yao yatabadilika or what does Pinda exactly meant?!.
Hii maana yake, hata ikitokea wapinzani wakashinda kwenye ballot box, lakini ushindi wa jumla ni CCM!.
Kusema ukweli, civic education kuhusu multipartism Tanzania, inatakiwa kuanzia juu ndipo ishuke chini kwa wananchi wa kawaida!.
Sasa ndio nimeanza kuelewa, no wonder kwa nini jina la Pinda, halitajwi kabisa kabisa katika presidential materials!. Maliza tuu term yako kwa amani, ukaiendeleza ile kampuni yako ya P & P, nami nitakutangazia sana ile asali yako, ila nakuomba Tanzania yetu utuachie kwa amani, hii sio Tanzania ya CCM, CHADEMA au CUF!. Tanzania ni ya Watanzania wote!.
Kiukweli, mabadiliko yakija, hizi nafasi za ma DC na ma RC ndizo ziwe za kwanza kufutiliwa mbali!.
I'm Very Disapointed!.
Paskali.
NB. Paskali ni Mtanzania mzalendo, Mwandishi wa habari wa kujitegemea ambaye ni mwanachama wa chama cha siasa, lakini sio mfuasi au mshabiki wa chama chochote cha siasa!. Ni mkereketwa wa maendeleo, mzalendo kwa kutanguliza mbele Utanzania kwa maslahi ya Taifa.
Kila nipatapo fursa, sipendi kabisa kukosa kipindi cha Maswali na Majibu ya Papo kwa Papo kwa Waziri Mkuu Bungeni, ambapo Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo, Kayanza, Peter Pinda, hujibu maswali ya papo kwa papo, ile leo nilikikosa kipindi hiki.
Lakini kupitia taarifa za habari, nimemsikia Mhe. Pinda, akisema kuwa ni jukumu la wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya kuhakikisha CCM inashinda chaguzi zote ili CCM iendelee kutawala milele!.
Naombeni wajuzi wa masuala ya utawala, mnirekebishe if I'm wrong!, kuanzia kwa rais JK na wanasiasa wengine wote ambao japo wamechaguliwa kwa tiketi tuu za vyama vyao vya siasa, lakini walio wachagua sio wanachama wa vyama vyao tuu, bali wamechaguliwa na umma wa Watanzania wote kwa ujumla wetu, rais, mbunge, diwani au wenyeviti wa mitaa, ukiishaguliwa, japo unabaki kuwa mwanachama wa chama chako lakini unageuka ni mtumishi wa umma, paid by taxpayers money, jukumu lako kuu sasa ni kuutumikia umma ambao chama chako ni sehemu ya umma huo na sio kukitumikia chama chako!.
Hii inamaanisha rais JK, japo ameshinda kwa tiketi ya CCM, kuongoza serikali ya JMT, kwa kutumia ilani ya uchaguzi ya CCM, ambapo kwa wakati huo huo yeye ndiye Mwenyekiti wa CCM, hakuchaguliwa na wana CCM pekee, amechaguliwa na Watanzania wote kwa ujumla wetu kuiongoza Tanzania na Watanzania na sio amechaguliwa na wana CCM, kuongoza serikali ya CCM kwa ajili ya wana CCM pekee!, hapana!, JK na serikali yake, japo ni CCM, lakini amechaguliwa kuongoza serikali ya Tanzania kwa niaba ya Watanzania wote na kwa manufaa ya Watanzania wote, wakiwemo watu wa vyama vingine vyote vilivyopo kisheria kwa mujibu wa katiba na sio kwa manufaa ya wana CCM!. (Of the people, by the people and for the people), hivyo hili la viongozi wa umma kutakiwa kuhakikisha CCM inatawala milele, kusema ukweli, mimi linanitatiza!.
JK ndiye rais wa Chadema, ndiye rais wa CUF na ndiye rais wa wote wenye vyama na wasio na vyama. Yeye ndiye rais wa Dr. Slaa, yeye ndiye rais wa Prof. Lipumba, yeye ndiye rais wetu sisi wote kama Watanzania, ni rais wa waliomchagua na pia rais wa wasiomchagua, anatakiwa kufanya kazi kwa kutanguliza mbele maslahi ya taifa kwanza na sio maslahi ya chama chake cha CCM!.
Kauli ya Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda bungeni leo kuwa Wakuu wa wilaya na mikoa, wako pale kuhakikisha CCM inashinda chaguzi zote ili itawale milele, haiwezi kupita bila kupingwa!. Hi inamaanisha kuwa viongozi hawa, wako kwa ajili ya kuilinda na kuitetea status quo ya CCM ili iendelee kutawala milele!. Kwa maoni yangu, this is very wrong kwa tafsiri sahihi ya Public Servants!. Kwa kauli hii ya Pinda, it goes without saying kuwa wakuu wa majeshi yetu, Polisi wetu, mahakama zetu na wakuu na vyombo vya dola, na vyombo vya kiserikali, wanateuliwa ili wahakikishe CCM haishindwi na inaendelea kutawala milele!.
Public Servant, ni mtumishi wa umma, ma RC na ma DC ni viongozi wa serikali, kwa maana hiyo ni viongozi wa umma, na watatimiza majukumu yao kwa maslahi ya umma na sio kwa maslahi ya CCM. Ndio maana Mhe. Tundu lissu aliwakataa hawa wasihusishwe ile tume ya katiba na juzi akasisitizwa hawapaswi kuwamo bungeni!.
Hata wabunge wa kuchaguliwa, ni watumishi wa umma, japo wanateuliwa kwa tiketi za vyama vya siasa, wanachaguliwa na wananchi na sio na vyama vyao, hivyo wakishashinda ubunge, wanakuwa ni watumishi wa watu na sio watumishi wa vyama vyao, hivyo wanapaswa kutekeleza majukumu yao ya kibunge kwa maslahi ya wananchi na sio kwa maslahi ya vyama vyao!. Kama ni kweli, majukumu ya ma RC na ma DC ni kuhakikisha CCM haishindwi, hii ina maana kubwa zaidi katika mustakabali wa mabadiliko halali ya serikali!.
Binafsi yangu, nimesikitishwa na kauli hiyo, and to be honest, nilikuwa na very high hopes kuhusu Pinda, kuelekea 2015! lakini sasa nimeamini Pinda pia ni wale wale!. Kwa vile CCM ni chama tawala, hivyo public servants wana jukumu la kuhakikisha CCM inashinda na kutawala milele!.
Hii inamaanisha hata kama 2015, Watanzania wataamua kuivote out CCM kupitia njia halali ya ballot box, hao public servants wenye jukumu la kuitumikia serikali mpya ya chama kitakachoshinda, tayari wako kwenye mind set ya chama kimoja kuhakikisha lazima CCM inashinda!, na jee ikitokea CCM ikashindwa kweli, jee watakabidhi madaraka kwa mshindi halali?!, jee majukumu yao yatabadilika or what does Pinda exactly meant?!.
Hii maana yake, hata ikitokea wapinzani wakashinda kwenye ballot box, lakini ushindi wa jumla ni CCM!.
Kusema ukweli, civic education kuhusu multipartism Tanzania, inatakiwa kuanzia juu ndipo ishuke chini kwa wananchi wa kawaida!.
Sasa ndio nimeanza kuelewa, no wonder kwa nini jina la Pinda, halitajwi kabisa kabisa katika presidential materials!. Maliza tuu term yako kwa amani, ukaiendeleza ile kampuni yako ya P & P, nami nitakutangazia sana ile asali yako, ila nakuomba Tanzania yetu utuachie kwa amani, hii sio Tanzania ya CCM, CHADEMA au CUF!. Tanzania ni ya Watanzania wote!.
Kiukweli, mabadiliko yakija, hizi nafasi za ma DC na ma RC ndizo ziwe za kwanza kufutiliwa mbali!.
I'm Very Disapointed!.
Paskali.
NB. Paskali ni Mtanzania mzalendo, Mwandishi wa habari wa kujitegemea ambaye ni mwanachama wa chama cha siasa, lakini sio mfuasi au mshabiki wa chama chochote cha siasa!. Ni mkereketwa wa maendeleo, mzalendo kwa kutanguliza mbele Utanzania kwa maslahi ya Taifa.