Ahsante sana P,
Huyu mama anasema ameishi miaka yote hiyo na hajawahi kumsimulia mtu yeyote mambo yake hadi alipoamua kunisimulia mimi baada ya kukutana kwenye net. Amejitahidi sana na anasema anampenda mume wako. Hata akisafiri lazima atamfuatilia kwe sms nzuri na kumpigia simu. Ila mume akipiga basi kuna shida au kuna kitu anataka kuuliza. Na anasema sms kutoka kwa mume wake ziko dry sana zaidi ya amri ya afande!
ka ushauri kangu kadogo kwako mtu mzima,usije ukaanza 'yale mambo yetu' na huyu mama(maana kaumizwa na hujui kwanini of all the people ka-open up kwako tu)hata kama ni mtandaoni.mzee usije ukapatwa huruma ukaona umpe bi mkubwa faraja ukijua ni kwenye net tu.ya watu kuchinjwa na strangers huanza hivihivi.Au pia inawezekana ukawa ni mtego mama chanja wako baadae akakuchombeza(kimtego)mzee ukafumaniwa mtandaoni.ni hayo tu mkubwa.