Mwanajamii
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 7,063
- 68
[h=3]NEC Yamsafisha Siyoi: Pingamizi La Chadema Latupwa Nje[/h]
NEC yamsafisha Sioi (Tanzania Daima)
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imemsafisha mgombea wa CCM katika uchaguzi mdogo wa Arumeru Mashariki, Sioi Sumari, kutokana na tuhuma za utata wa uraia wake zilizokuwa zimewasilishwa katika rufaa na mgombea wa CHADEMA, Joshua Nassari.
Uamuzi huo wa NEC uliotangazwa jana mbele ya waandishi wa habari na Mkurugenzi wa tume, Julius Mallaba, akisema kuwa kutokana na sababu kadhaa zilizoonyeshwa na jopo la wataalamu wa tume waliokaa kupitia vifungu vya sheria za uhamiaji za Kenya na Tanzania, rufaa hiyo imeonekana haina msingi.
Kwa mujibu wa maelezo na vielelezo vilivyowasilishwa pamoja na rufaa ya mrufani na kwa kuzingatia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977, Katiba ya zamani ya Kenya, Sheria ya Uraia ya Tanzania, Na. 6 ya mwaka 1995, Tume inakubaliana na uamuzi wa msimamizi wa uchaguzi wa kukataa pingamizi la mrufani kwa sababu zifuatazo.
Katika maelezo ya mrufani na vielelezo alivyowasilisha tume, hakuna popote ilipothibitishwa kuwa Sioi alipata uraia wa Kenya. Kwa kuwa mrufani ndiye aliyetoa madai kuwa mgombea alipata uraia wa Kenya kwa kuzaliwa kwake Kenya, basi alipaswa kuthibitisha madai yake kwa mujibu wa kanuni, alisema.
NEC yamsafisha Sioi (Tanzania Daima)
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imemsafisha mgombea wa CCM katika uchaguzi mdogo wa Arumeru Mashariki, Sioi Sumari, kutokana na tuhuma za utata wa uraia wake zilizokuwa zimewasilishwa katika rufaa na mgombea wa CHADEMA, Joshua Nassari.
Uamuzi huo wa NEC uliotangazwa jana mbele ya waandishi wa habari na Mkurugenzi wa tume, Julius Mallaba, akisema kuwa kutokana na sababu kadhaa zilizoonyeshwa na jopo la wataalamu wa tume waliokaa kupitia vifungu vya sheria za uhamiaji za Kenya na Tanzania, rufaa hiyo imeonekana haina msingi.
Kwa mujibu wa maelezo na vielelezo vilivyowasilishwa pamoja na rufaa ya mrufani na kwa kuzingatia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977, Katiba ya zamani ya Kenya, Sheria ya Uraia ya Tanzania, Na. 6 ya mwaka 1995, Tume inakubaliana na uamuzi wa msimamizi wa uchaguzi wa kukataa pingamizi la mrufani kwa sababu zifuatazo.
Katika maelezo ya mrufani na vielelezo alivyowasilisha tume, hakuna popote ilipothibitishwa kuwa Sioi alipata uraia wa Kenya. Kwa kuwa mrufani ndiye aliyetoa madai kuwa mgombea alipata uraia wa Kenya kwa kuzaliwa kwake Kenya, basi alipaswa kuthibitisha madai yake kwa mujibu wa kanuni, alisema.