Pinda: Pamoja na matatizo ya umeme lakini uchumi wetu haujatetereka

Ndibalema

JF-Expert Member
Apr 26, 2008
10,956
4,648
Nimeshangazwa na kauli ya Waziri mkuu Mizengo Pinda kuwa "pamoja na matatizo ya umeme nchini lakini uchumi wa Tanzania haujatetereka hata kidogo...na ndio maana hata viongozi hawatetemeki kuelezea uimara huo wa uchumi.."

Mimi simwelewi Waziri mkuu wangu.
nashindwa kumwelewa jamani, naomba wanaJF mnisaidie huu uchumi ulio imara ni uchumi upi?
Au miye sijui mambo ya uchumi kwa sababu sio fani yangu?
 
Umemsahau yule waziri wa habari wa iliyokuwa serikali ya Iraq WAKATI ULE?......Wakati wamarekani wanamwaga mabomu kama mvua mitaa ya Baghadad, jamaa anaripoti kuwa.."we havent spotted any American Soldier in Baghdad, and any who will approach, his grave will be right here in Baghdad..."..Hizo ni Propaganda za wanasiasa, ambazo kawaida huwa ni kinyume na ukweli....Kiwanda chochote kikisimama abnormally kwa masaa 6 tu, tayari ni hasara kubwa!...Kama viwanda vinaripoti hasara kila siku, uchumi huo wa taifa unaopanda unahesabiwa kutokana na nini?...si ni aggregate ya production za viwanda anuwai?...achana na MWONGO MKUU HUYO!
 
Umemsahau yule waziri wa habari wa iliyokuwa serikali ya Iraq WAKATI ULE?......Wakati wamarekani wanamwaga mabomu kama mvua mitaa ya Baghadad, jamaa anaripoti kuwa.."we havent spotted any American Soldier in Baghdad, and any who will approach, his grave will be right here in Baghdad..."..Hizo ni Propaganda za wanasiasa, ambazo kawaida huwa ni kinyume na ukweli....Kiwanda chochote kikisimama abnormally kwa masaa 6 tu, tayari ni hasara kubwa!...Kama viwanda vinaripoti hasara kila siku, uchumi huo wa taifa unaopanda unahesabiwa kutokana na nini?...si ni aggregate ya production za viwanda anuwai?...achana na MWONGO MKUU HUYO!

Umenikumbusha mbali sana.! Kweli watawala wetu wa leo wako kama Mohamed al Sahaf wa Iraq. N-way, dhamiri zao zinawasuta! Hawasemi kama industrial products zetu zimeongezeka au la! Je exports zetu katika kipindi hiki cha mgao wa umeme na ukame zina status ipi? Very sad!
 
Nimeshangazwa na kauli ya Waziri mkuu Mizengo Pinda kuwa "pamoja na matatizo ya umeme nchini lakini uchumi wa Tanzania haujatetereka hata kidogo...na ndio maana hata viongozi hawatetemeki kuelezea uimara huo wa uchumi.."

Mimi simwelewi Waziri mkuu wangu.
nashindwa kumwelewa jamani, naomba wanaJF mnisaidie huu uchumi ulio imara ni uchumi upi?
Au miye sijui mambo ya uchumi kwa sababu sio fani yangu?


Kama alidanganya bunge utegemee nini zaidi. Nina mfano halisi: Mwezi wa 12 nilinunua betri ya national Special kwa Tzs.350/= Lakini mwezi huu nimenunua kwa Tzs.700/=. Kama cost of sales ni kubwa namna hiyo how can u compete with other products from other states. Uchumi kuimalika tuna export zaidi ya importation? Jina hili ni baya "PINDA".
 
:A S 13::A S 13:Wamelewa madaraka na huduma za bure kila saa.....mwenzetu hajui hata bei ya sukari wala chumvi,gari halipii mafuta wala nini,atajuaje shida zetu??? Dr Slaa akisema wanamuona mchochezi na mwenye nia ya kuharibu usalama.....hawatuelewi jamani....tuchukue hatua....mwenzake Lowassa juzi kasema iundwe tume ya kushughulikia mfumuko wa bei na matatizo ya kiuchumi yeye haoni lolote.......
 
Haja ainisha uchumi upi ana zungumzia. Kama ni uchumi wa Tanzania au la. Ingefaa aulizwe. Yawezekana ana ongelea uchumi wa baadhi ya watu maana hata Marekani kuna baadhi ya Wall Street companies zili tajirika kwa kubet against the economy. Kwa hiyo hata hapa nchini kwetu kuna uchumi wa baadhi ya watu una tegemea uchumi wa jumla wa taifa kuwa mbovu.
 
Nimeshangazwa na kauli ya Waziri mkuu Mizengo Pinda kuwa "pamoja na matatizo ya umeme nchini lakini uchumi wa Tanzania haujatetereka hata kidogo...na ndio maana hata viongozi hawatetemeki kuelezea uimara huo wa uchumi.."

Mimi simwelewi Waziri mkuu wangu.
nashindwa kumwelewa jamani, naomba wanaJF mnisaidie huu uchumi ulio imara ni uchumi upi?
Au miye sijui mambo ya uchumi kwa sababu sio fani yangu?

Siyo lazima kaka uwe MCHUMI kujua uchumi... tena WA NCHI UNAYOISHI , uko imara au magumashi. Pinda naye kesha haribikiwa.
 
:A S 13::A S 13:Wamelewa madaraka na huduma za bure kila saa.....mwenzetu hajui hata bei ya sukari wala chumvi,gari halipii mafuta wala nini,atajuaje shida zetu??? Dr Slaa akisema wanamuona mchochezi na mwenye nia ya kuharibu usalama.....hawatuelewi jamani....tuchukue hatua....mwenzake Lowassa juzi kasema iundwe tume ya kushughulikia mfumuko wa bei na matatizo ya kiuchumi yeye haoni lolote.......

Hapo kwenye nyekundu Michelle naona umepotoka na unashindwa kuona alama za ukutani... Kwa kipindi hiki cha 2010-2015 LOWASA NI WA KUPUUZWA KWA KILA KITU AISEE.
 
mwenye shida hajui mwenye njaa! haya ndio ya mfalme yule wa ufaransa enzi izo aliyepinduliwa na kuuawa mitaani na wanachi wenye hasira kali na njaa wakati wanaandamana wako nje ya palace lake juu gorofani yeye yuko juu wanawashangaa alipouliza walinzi na watumishi wake kua wanashida gani akajibiwa eti wanaandamana hawana mikate ya kula mkewe akawatuma watumishi eti kama mikate hamna si wale keki!
 
Anakuwa mtoto wa mkulima hata kichwani!!! Hii balaaa. Kama kwa hali hii inayokumba sasa wananchi bado uchumi haujatetereka, basi inabidi nirudi darasani kujifunza tena maana ya neno uchumi.
 
Ni vizuri wanaJF wakamjulisha Mhe. Pinda, Waziri Mkuu wetu kuwa uchumi wetu kwa vyovyote ni lazima unaathirika na kutetereka, kutokana na kutopatikana kwa nishati muhimu kama umeme. Mgao wa umeme unaoendelea sasa matokeo yake ni viwanda kadhaa vinafungwa. Kutozalisha bidhaa wakati huo sio tu mwenye kiwanda hapati pato, bali wafanyakazi wanakosa ajira.

Kupunguka kwa bidhaa sokoni sio tu kutalazimisha bei kupanda, bali watumiaji na walaji wengine watazikosa na kuathirika. Mfumko wa bei ndiyo matokeo: yaani uchumi utatetereka.

Kama hospitali imekatiwa umeme kutokana na mgao, huduma ya upasuaji haiwezi kutolewa na wagonjwa wanaathirika. Wagonjwa wakiongezeka uchumi utatetereka.

Chuoni kusipokuwa na umeme, wanafunzi na wahadhiri wao hawawezi kusoma! Hata kama wazazi wamekwisha lipia ada watoto wao, itakuwa mafunzo hayaendi inavyotakikana.

Huku nyumbani kwetu tunapokosa umeme, mapishi hayaendi vizuri na inakuwa ni lazima kuni au mkaa utumike. Vitu viaendelea shagala bagala. Matumizi ya mkaa na kuni badala ya umeme yanapunguza uoto asilia kwa miti kukwatwa, na mazingira kuathirika. In the long term, uchumi unatetereka.

Ofisini kwa wakubwa wenye kukaa maghorofani, kama mawaziri wanaomsaidia Waziri Mkuu na Rais, lifti hazifanyi kazi. Wanaathirika na wanachelewesha kutekeleza majukumu yao. Uchumi unaathirika.

Nadhani Waziri Mkuu wetu alighafilika kidogo alipotamka eti uchumi haujatetereka. Tumwonee huruma. Kijana wa mkulima, amezidiwa mzigo.
 
Jinga kabisa, sasa tumwamini nani sasa, bosi wake juzi anasema uchumi wetu unaathiriwa kiurahisi sana na matatizo madogo madogo wewe unatuambia pamoja na hayo bado uchumi uko bomba, pambaf
 
Masikini, wameshamchakachua baba wa watu kisiasa..!!! Yaani anaanza kuwa kama kina M....ambao alipokuwa waziri wa fedha aliwahi kuongea hadharani kuwa mgao wa umeme na ukame havijaathiri uchumi..!! Hawa viongozi waache kukurupuka, wawe wanatumia wataalamu ambao hawajachakachuliwa na wanasiasa, ili wawape facts na sio propaganda.

Kuna vitu mtu unapaswa kuvifikira hata kama huna utaalamu, wewe mgao wa umeme unasema haujateteresha uchumi; wanajua maana ya kutetereka kwa uchumi..?? Muuza kuku au perishables anakula hasara kila siku kwa kutupa bidhaa kisa zimeharibika baada ya kukosa umeme..!!! Anafikiria multiplier effect ya simple problem kama hii ya huyu mfanyabiashara...?? Wafanyabiashara wanatumia nishati mbadala kuzalisha bidhaa zao badala ya umeme wa Tanesco, then anategemea cost of living iwe the same..?? Au anafikiri uchumi kutetereka ni kwa wao kukosa per-diem au sitting allowances..?? Uchumi una aspects au parameters nyingi more than one can think..!!

Kuna kiongozi mwenzake naye nasikia aliwahi kusema kuwa uchumi wa Tz umekua kwa kuangalia foleni barabarani na kudai kuwa wananchi wengi wana magari siku hz..!! Hajiulizi kuwa uchumi unatetereka kwa kukosa miundo mbinu bora (barabara) ambazo zinarandana na kuongezeka kwa mahitaji ya kijamii ambapo siku hizi gari limegeuka kuwa basic need kutokana na uozo kwenye sekta ya public transport....??? Hajiulizi kati ya hayo ni magari mangapi ni ya makampuni..? Hajiulizi income gap inayoitesa Tz ambapo kuna watu hata nauli ya commuter bus kwa trip moja inawapa shida..!!

Nafikiri viongozi wetu waanze kupewa shule ya uchumi na public speech..!! Wawe wanajua kuwa wenzetu, viongozi wao huwa wanaongea kitu baada ya vichwa kadhaa katika sekta husika kukaa na kumshauri. Na hivyo vichwa vikigundulika vimem-mislead kiongozi wa serikali hasa Rais, then vinaipata joto ya jiwe. Hapa kwetu; nina mashaka kidogo..!! Si ajabu kuna watu wanawadanganya hawa viongozi kwa kiwango cha juu baada ya kugundua kuwa viongozi wenyewe wanawaamini sana na pia hawana muda wa kuchuja wanayopewa..!!
 
Haijalishi kama ni waziri mkuu au la mwingine yeyote kusema uchumi wetu haujatetereka! Mtu anayetoa kauli hiyo ni mpumbavu kuliko tunavyodhani, ww pinda una uhakika wa mshahara wako na marupurupu umeme ukikatika wanakuwashia jenereta on the spot, mimi ninategemea umeme lets say ni kinyozi au nina machine zangu za kusaga na kukoboa, umeme unapokuwa wa mgao bado sijatetereka? Lets say nilichukua credit kupata machines zangu, at the end napopeleka marejesho nikiwaambia nashindwa kurejesha ipasavyo maana umeme wa mgao watanielewa? Nashindwa kuelewa umekaa madarakani zaidi ya miongo mitatu lakini mpaka leo unatoa kauli za kipumbavu, maskini tz! Ungekuwa nchi za watu makini ungeshafukuzwa kazi mda mrefu mf albino issue, umesema uongo bungeni! Na sasa unatudanganya hadharani! Bora yako umezaliwa tz na si ulaya (au nchi zilizoendelea) kweli tz tuna viongozi useless!
 
Ifike mahali tuanze kutembea na mawe mifukoni... kiongozi akitoa upupu wa hivyo anafurumushwa kwa mawe.. Yaani viwanda 50+ vimesitisha uzalishaji, hatujagusa biashara na shughuli nyingine zinazotegemea umeme, yeye bado hajui kama kuna effects mbaya mno kwenye uchumi???
 
Masikini, wameshamchakachua baba wa watu kisiasa..!!! Yaani anaanza kuwa kama kina M....ambao alipokuwa waziri wa fedha aliwahi kuongea hadharani kuwa mgao wa umeme na ukame havijaathiri uchumi..!! Hawa viongozi waache kukurupuka, wawe wanatumia wataalamu ambao hawajachakachuliwa na wanasiasa, ili wawape facts na sio propaganda.

Kuna vitu mtu unapaswa kuvifikira hata kama huna utaalamu, wewe mgao wa umeme unasema haujateteresha uchumi; wanajua maana ya kutetereka kwa uchumi..?? Muuza kuku au perishables anakula hasara kila siku kwa kutupa bidhaa kisa zimeharibika baada ya kukosa umeme..!!! Anafikiria multiplier effect ya simple problem kama hii ya huyu mfanyabiashara...?? Wafanyabiashara wanatumia nishati mbadala kuzalisha bidhaa zao badala ya umeme wa Tanesco, then anategemea cost of living iwe the same..?? Au anafikiri uchumi kutetereka ni kwa wao kukosa per-diem au sitting allowances..?? Uchumi una aspects au parameters nyingi more than one can think..!!

Kuna kiongozi mwenzake naye nasikia aliwahi kusema kuwa uchumi wa Tz umekua kwa kuangalia foleni barabarani na kudai kuwa wananchi wengi wana magari siku hz..!! Hajiulizi kuwa uchumi unatetereka kwa kukosa miundo mbinu bora (barabara) ambazo zinarandana na kuongezeka kwa mahitaji ya kijamii ambapo siku hizi gari limegeuka kuwa basic need kutokana na uozo kwenye sekta ya public transport....??? Hajiulizi kati ya hayo ni magari mangapi ni ya makampuni..? Hajiulizi income gap inayoitesa Tz ambapo kuna watu hata nauli ya commuter bus kwa trip moja inawapa shida..!!

Nafikiri viongozi wetu waanze kupewa shule ya uchumi na public speech..!! Wawe wanajua kuwa wenzetu, viongozi wao huwa wanaongea kitu baada ya vichwa kadhaa katika sekta husika kukaa na kumshauri. Na hivyo vichwa vikigundulika vimem-mislead kiongozi wa serikali hasa Rais, then vinaipata joto ya jiwe. Hapa kwetu; nina mashaka kidogo..!! Si ajabu kuna watu wanawadanganya hawa viongozi kwa kiwango cha juu baada ya kugundua kuwa viongozi wenyewe wanawaamini sana na pia hawana muda wa kuchuja wanayopewa..!!
Kwa hapa kwetu, kiongozi akishasiba tu anaweza kuongea kitu chochote kwani ni tumbo ndilo linalomwongoza kusema na si kichwa. Kina Pinda wakishatoka majumbani kwao wmeshiba wanadhani wanajua kila kitu. Uchumi kwangu unakuwa imara pale bidhaa za chakula zinapoweza kufikika kwa unafuu kwa kila mtu na wala si kwa sababu kikundi cha watawala wacache kinakula na kuanza kutuonesha matumbo
 
Nimeshangazwa na kauli ya Waziri mkuu Mizengo Pinda kuwa "pamoja na matatizo ya umeme nchini lakini uchumi wa Tanzania haujatetereka hata kidogo...na ndio maana hata viongozi hawatetemeki kuelezea uimara huo wa uchumi.."

Mimi simwelewi Waziri mkuu wangu.
nashindwa kumwelewa jamani, naomba wanaJF mnisaidie huu uchumi ulio imara ni uchumi upi?
Au miye sijui mambo ya uchumi kwa sababu sio fani yangu?
Watanzania tunalishwa uongo kila leo na tunaridhika, hakuna mtu wa kuuliza huo uchumi haukutetereka kwa kiasi gani???????? Kwa data zipi zinazo onyesha kukua au kutokutetereka kwa uchumi!!! Economical indicators zipi maana vyanzo vyote vya mapato viko effected kwa ukosefu wa umeme, sasa wewe waziri mkuu unasema uchumi uko stable haujawa effected unafikiria kweli au kivipi???????? Hao ndio viongozi wetu wa SISIEM.
 
Back
Top Bottom