BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,011
Eti Waziri Mkuu hajui umaskini wa Watanzania unasababishwa na nini? Halafu anataka ufanywe utafiti ili kugundua chanzo cha umaskini wa Watanzania! Waziri Mkuu wa nchi baada ya miaka 50 ya uhuru hajui umaskini wa Wananchi wake unasabababishwa na nini!
~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*
Pinda asema hajui kwanini Watanzania ni maskini
Wednesday, 30 March 2011
Raymond Kaminyoge
Mwananchi
WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda ameitaka Taasisi ya Utafiti wa Kuondoa Umaskini (Repoa), kufanya utafiti ili kufahamu kwa nini wananchi wa kawaida wanalalamikia hali ngumu ya maisha wakati kitaifa, uchumi unakua.
Pinda alisema hayo Dar es Salaam jana, wakati akifungua mkutano wa 16 wa taasisi hiyo uliowashirikisha watafiti wa masuala ya uchumi.
Alisema tafiti hizo zikifanyika zitaisadia Serikali kuchukua hatua kuboresha maisha ya wananchi wake… "Repoa fanyieni kazi utafiti huu. Watu wanalalamika ugumu wa maisha, hatuwezi kukaa kimya tutafiti inakuwaje uchumi unakua lakini watu wanalalamika maisha ni magumu!" (Toba!) Kwa mujibu wa Pinda Serikali imekuwa ikitumia matokeo ya tafiti za Repoa kutekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo akasisitiza kuwa utafiti kuhusu hali ya umaskini nchini nao ni muhimu.
"Naomba niwapongeze kwa kazi nzuri ambayo mnaifanya, Serikali inajivunia tafiti ambazo zinafanywa na taasisi hii," alisema. Aliitaka taasisi hiyo kujikita zaidi kwenye sekta za kilimo na mifungo kwani hayo ni maeneo ambayo wananchi wanayategemea katika kujiajiri.
"Mkifanya utafiti kwa mfano, katika eneo la ufugaji wa nyuki, matokeo ya utafiti huo yatasaidia wananchi katika kuongeza maarifa na hivyo kujikwamua na umaskini," alisema.
Aliitaka Repoa kufanya utafiti kufahamu ni kwa nini wasomi nchini hawataki kujiajiri kwenye sekta ya kilimo.
"Mtueleze Serikali ifanye nini ili wasomi hawa waweze kuvutiwa na kwenda kujiajiri katika kilimo badala ya kutegemea kuajiriwa kwenye ofisi kubwa mijini," alisema.
Awali, akizungumza katika hafla hiyo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Repoa, Profesa Samwel Wangwe alisema tangu taasisi hiyo ianzishwe mwaka 1995, imeshafanya tafiti 90 (soma hizi ripoti badala ya kukurupuka!)zinazohusu umaskini na kupendekeza njia ya kuondokana nao.
~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*~*
Pinda asema hajui kwanini Watanzania ni maskini
Wednesday, 30 March 2011
Raymond Kaminyoge
Mwananchi
WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda ameitaka Taasisi ya Utafiti wa Kuondoa Umaskini (Repoa), kufanya utafiti ili kufahamu kwa nini wananchi wa kawaida wanalalamikia hali ngumu ya maisha wakati kitaifa, uchumi unakua.
Pinda alisema hayo Dar es Salaam jana, wakati akifungua mkutano wa 16 wa taasisi hiyo uliowashirikisha watafiti wa masuala ya uchumi.
Alisema tafiti hizo zikifanyika zitaisadia Serikali kuchukua hatua kuboresha maisha ya wananchi wake… "Repoa fanyieni kazi utafiti huu. Watu wanalalamika ugumu wa maisha, hatuwezi kukaa kimya tutafiti inakuwaje uchumi unakua lakini watu wanalalamika maisha ni magumu!" (Toba!) Kwa mujibu wa Pinda Serikali imekuwa ikitumia matokeo ya tafiti za Repoa kutekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo akasisitiza kuwa utafiti kuhusu hali ya umaskini nchini nao ni muhimu.
"Naomba niwapongeze kwa kazi nzuri ambayo mnaifanya, Serikali inajivunia tafiti ambazo zinafanywa na taasisi hii," alisema. Aliitaka taasisi hiyo kujikita zaidi kwenye sekta za kilimo na mifungo kwani hayo ni maeneo ambayo wananchi wanayategemea katika kujiajiri.
"Mkifanya utafiti kwa mfano, katika eneo la ufugaji wa nyuki, matokeo ya utafiti huo yatasaidia wananchi katika kuongeza maarifa na hivyo kujikwamua na umaskini," alisema.
Aliitaka Repoa kufanya utafiti kufahamu ni kwa nini wasomi nchini hawataki kujiajiri kwenye sekta ya kilimo.
"Mtueleze Serikali ifanye nini ili wasomi hawa waweze kuvutiwa na kwenda kujiajiri katika kilimo badala ya kutegemea kuajiriwa kwenye ofisi kubwa mijini," alisema.
Awali, akizungumza katika hafla hiyo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Repoa, Profesa Samwel Wangwe alisema tangu taasisi hiyo ianzishwe mwaka 1995, imeshafanya tafiti 90 (soma hizi ripoti badala ya kukurupuka!)zinazohusu umaskini na kupendekeza njia ya kuondokana nao.