Kama kiongozi wa baraza la Mawaziri anayejua fika jinsi magari haya yanavyoongeza kwa kiasi kikubwa gharama za uendeshaji Serikalini, Pinda angweza kusimama kidete na kuzuia ununuzi wa magari hayo ya gharama na badala yake kuwataka Wabunge wakachukue mikopo kutoka mabenki ya biashara ili wajinunulie magari wanayoyataka ili kuwapunguzia walipa kodi mzigo ambao ni mkubwa mno, lakini kwa kulikataa gari na kusema apewe fulani ameonyesha woga na kutojiamini kusimamia maslahi ya Watanzania. Hivi kila waziri akiamua kufanya maamuzi ya pekee yake badala ya maamuzi ya pamoja kama baraza la mawaziri tutafika kweli? Kwa maoni yangu Pinda uongozi umemshinda.
Pinda ni MNAFIKI MKUBWA. Anapenda kucheza na jukwaa ilhali watazamaji wameshamchoka na chenga zake,mara kupiga matobo na kanzu,ambazo zote hazisababishi kupatikana kwa magoli!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.