Pinda na Makinda wampa changamoto Kikwete. Je watajiwajibisha au kuwajibishwa?

Kama ningekua ndie Rais Jakaya Mrisho Kikwete basi nisingesita hata punje kumwajibisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na kuangalia uwezekano wa kumwajibisha Spika Anna Makinda! Ningefanya hivyo kufuatia taarifa iliyotolewa na Ikulu hapo jana! Kwamba, Mheshimiwa Rais hakupandisha posho bali aliwaambia “watumie busara katika suala la kupandisha posho hiyo!”
Hata hivyo, nafahamu fika kwamba hata kama ningekuwa mimi ndie JK nisingekuwa na ubavu wa kuchukua maamuzi hayo hapo juu endapo:
  1. Ikulu kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano imeamua kuudanganya umma kwamba Rais hajapandisha posho isipokuwa amewaagiza wahusika kutumia busara. Hapa maana yake ni kwamba, Rais amebariki upandishwaji wa posho lakini anataka kukana kwamba hajafanya hivyo.
  2. Ikulu kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano pamoja na ushirikiano wao na Spika wa Bunge na Waziri Mkuu, wamefanya hivyo makusudi ili kucheza danadana na akili za Watanzania ili badala ya kujadili suala nyeti la mgomo wa madaktari, hivi sasa tuelekeze akili yetu kwenye suala la posho!
Hivyo basi, ikiwa sababu hasa ndizo hizo mbili nilizozitaja hapo juu basi ni Rais mwenyewe ndie anayepaswa kuwajibika kwa kuudanganya umma unless Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu iwe imetoa taarifa hiyo yenyewe na sio Rais. Na kama taarifa hiyo ni ya Kurugenzi ya Mawasiliano pasi na mkono wa Rais basi Salva Rweymamu anapaswa kuondolewa mara moja. Na kama kilichotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ni kweli na kwamba ndio msimamo wa Rais basi Mheshimiwa Rais hana budi kuwaondoa watu hao mara moja kwavile walichofanya ni hujuma dhidi yake.
Kwanini nasema hivyo?
IKiwa kweli rais aliagiza busara itumike, basi kutangaza upandaji wa posho muda huu ni ukosefu wa busara uliopita mipaka ingawaje yeye aliagiza kutumika kwa busara! Haiwezekani wakati nchi ipo katika hali tete ambapo wananchi wanakufa kutokana na mgomo wa madaktari wanaodai maslahi zaidi; Waziri Mkuu na Spika wanatangaza kuongezeka kwa viwango vya posho kwa Wabunge! Kama ni kweli Rais aliagiza busara kutumika basi iliyofanyika hapa ni HUJUMA dhidi yake kwa sababu hakuna chembe ya busara iliyotumika. Ni hujuma dhidi yake kwa sababu kauli ya Waziri Mkuu na Spika wa Bunge ni dhahiri imeamsha chuki ya wananchi dhidi ya serikali yao hasa ukizingatia imetolewa wakati wananchi wanapoteza maisha kwa kukosa huduma toka kwa madaktari. Hii ni hujuma kwavile inaonesha dhahiri kwamba Waziri Mkuu na Spika wa Bunge wameamua kumfitinisha Rais na wananchi anaowaongoza.
Hivyo, ukiangalia mchanganuo huo hapo juu, utakuta ni lazima ama Rais awajibike, kwa kuudanganya umma! Na kama hajaudanganya umma, kwamba kauli ya Kurugenzi ni ya kweli, basi ni lazima Rais awawajibishe Waziri Mkuu na Spika kwa kumhujumu. Na kama Walichosema Waziri Mkuu na Spika ni sahii na kwamba Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imesema uongo, basi ni lazima Rweymamu ajiuzuru au afukuzwe kazi kwa kutoa kauli inayokinzana na matakwa ya bosi wake ambae ni Rais.
 
Tatizo la viongozi wetu hawa wanaogopana na wana nidhamu ya uwoga kwa kweli.

Hivi JK kama rais hawezi kusema sitaki hizo posho za wabunge ziongezwe?
 
wanaogopa kauli ya 'leo kwako kesho kwangu' kuwa wanalindana kwa nyadhifa zao ati inaweza fika wakati mwingine akipata cheo anaweza lipa kisasi.
 
It is obvious kuwa Serikali is in a BIG MESS! The President has to fire the whole Government and a new one formed. All leaders linked, even remotely, to the scandals of the past five years [doctors strike; Dowans; Jairo Bribes; Richmond; Wildlife; Gongo La Mboto and Mbagala explosions; EPAs; vote rigging etc etc] should be purged from the system and new ones appointed. This purge should include senior civil servants and leaders of public agencies who have been implicated in these scandals. Particular attention should be paid to the untouchables who have plundered the nation with impunity.

The President should form a new Government drafting into the Cabinet the main opposition leaders. A Special Prosecutor [SP]and a Special Court {SC}should be created to handle expeditiously the corruption crimes of the past five years. The SP and SC should be given 2 years to complete their task with a special jail built in say Mpanda for the mafisadis and other corrupt citizens found guilty. Particular attention should be paid to accomplices of the Mafisadis who are/were not in direct empolyment of Government - the business leaders etc.
 
Kama ningekua ndie Rais Jakaya Mrisho Kikwete basi nisingesita hata punje kumwajibisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na kuangalia uwezekano wa kumwajibisha Spika Anna Makinda! Ningefanya hivyo kufuatia taarifa iliyotolewa na Ikulu hapo jana! Kwamba, Mheshimiwa Rais hakupandisha posho bali aliwaambia "watumie busara katika suala la kupandisha posho hiyo!"
Hata hivyo, nafahamu fika kwamba hata kama ningekuwa mimi ndie JK nisingekuwa na ubavu wa kuchukua maamuzi hayo hapo juu endapo:

  1. Ikulu kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano imeamua kuudanganya umma kwamba Rais hajapandisha posho isipokuwa amewaagiza wahusika kutumia busara. Hapa maana yake ni kwamba, Rais amebariki upandishwaji wa posho lakini anataka kukana kwamba hajafanya hivyo.
  2. Ikulu kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano pamoja na ushirikiano wao na Spika wa Bunge na Waziri Mkuu, wamefanya hivyo makusudi ili kucheza danadana na akili za Watanzania ili badala ya kujadili suala nyeti la mgomo wa madaktari, hivi sasa tuelekeze akili yetu kwenye suala la posho!
Hivyo basi, ikiwa sababu hasa ndizo hizo mbili nilizozitaja hapo juu basi ni Rais mwenyewe ndie anayepaswa kuwajibika kwa kuudanganya umma unless Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu iwe imetoa taarifa hiyo yenyewe na sio Rais. Na kama taarifa hiyo ni ya Kurugenzi ya Mawasiliano pasi na mkono wa Rais basi Salva Rweymamu anapaswa kuondolewa mara moja. Na kama kilichotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ni kweli na kwamba ndio msimamo wa Rais basi Mheshimiwa Rais hana budi kuwaondoa watu hao mara moja kwavile walichofanya ni hujuma dhidi yake.
Kwanini nasema hivyo?
IKiwa kweli rais aliagiza busara itumike, basi kutangaza upandaji wa posho muda huu ni ukosefu wa busara uliopita mipaka ingawaje yeye aliagiza kutumika kwa busara! Haiwezekani wakati nchi ipo katika hali tete ambapo wananchi wanakufa kutokana na mgomo wa madaktari wanaodai maslahi zaidi; Waziri Mkuu na Spika wanatangaza kuongezeka kwa viwango vya posho kwa Wabunge! Kama ni kweli Rais aliagiza busara kutumika basi iliyofanyika hapa ni HUJUMA dhidi yake kwa sababu hakuna chembe ya busara iliyotumika. Ni hujuma dhidi yake kwa sababu kauli ya Waziri Mkuu na Spika wa Bunge ni dhahiri imeamsha chuki ya wananchi dhidi ya serikali yao hasa ukizingatia imetolewa wakati wananchi wanapoteza maisha kwa kukosa huduma toka kwa madaktari. Hii ni hujuma kwavile inaonesha dhahiri kwamba Waziri Mkuu na Spika wa Bunge wameamua kumfitinisha Rais na wananchi anaowaongoza.
Hivyo, ukiangalia mchanganuo huo hapo juu, utakuta ni lazima ama Rais awajibike, kwa kuudanganya umma! Na kama hajaudanganya umma, kwamba kauli ya Kurugenzi ni ya kweli, basi ni lazima Rais awawajibishe Waziri Mkuu na Spika kwa kumhujumu. Na kama Walichosema Waziri Mkuu na Spika ni sahii na kwamba Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imesema uongo, basi ni lazima Rweymamu ajiuzuru au afukuzwe kazi kwa kutoa kauli inayokinzana na matakwa ya bosi wake ambae ni Rais.

Pinda once again anathibitisha ni kilaza wa hali ya juu; na yule bibi spika ni bendera ifatayo upepo ..yani yupo yupo tu. Her thinking is completely controlled by the events.
 
Suala sio nani anawadanganya watanzania.. ni je wewe na mimi kama watanzania tumechukua hatua gani kwa hili na mambo lukuki yakijinga/kipumbavu yanayoendelea nchi hii

Tutabaki kuumiza keyboard zetu tu.. lets Act
 
Tunajadili hii mada kama vile hizi posho hazijalipwa, kiukweli hizi posho zilianza kulipwa tangu bunge lililopita. Cha maana tuangalie nani aliruhusu huo ulipaji kama rais alikuwa hajasaini? Mkaguzi mkuu wa serikali, takukuru na vyombo vya kinidhamu vinatakiwa vitupe taarifa ya huu mkanganyo. Ni wakati sasa na bunge liundiwe tume itakayoshughukia huu upimbavu na ikiwezekana hiyo ripoti isomwe kwa mbwembwe kama ambavyo ripoti nyingine zimesomwa. Na napendekeza mwenyekiti wa hiyo kamati awe Zitto au Januari.

Na sie watanzania ni wakati muafaka wa kuuliza huu uzembe umefanyikaje na ifike wakati tudai wazembe wawajibishwe.


Yani hili nalo tuliundie tume?:nono: mbona kila kitu kiko wazi? hiyo hela wanalipana na walishaanza siku nyingi

Kukaa humu JF na kulalamika haitobadili chochote! hawa jamaa walishatuona watanzania kama matutusa
 
Maelezo ya JK yalikuwa na utata posho zimeshaanza kulipwa kama spika alivyosema. JK atakuwa ameruhusu ila anataka awadhalilishe wenzake kama alivyofanya kwenye suala la Jairo. Ningekuwa mimi Pinda ningeshaachia ngazi zamani. This is the most divided government. Hata ile ya Mugabe na Tsvangrai, au ya Kibaki na Raila zina afadhali
 
Sasa sina mashaka tumefika mwisho wa ukuta ambapo haitavumilika tena. Mgongano wa ongozeko ya posho ya wabunge, umefikia mahali sasa tunaona kwa wazi kuwa tunadanganywa. Waziri Mkuu anasema vyake, Spika makinda anAsema vyake na Rais anakanusha kwa kuWapinga viongozi wakuu wenzake.

Ukweli ni kuwa kuna mkanganyiko mkubwa ambao ni wa makusudi. Hawa watu wametudharau sana tena sana. Yaani wametufanya Watanzania wote MAZEZETA ambao tunaweza kudanganyika kirahisi hivyo. Huu mkanganyiko na mgongano sio mdogo, na pengine MEDIA ingapaswa kushikia bango jambo hili mpaka waombe radhi. Hii dharau kubwa kuwahi kufanywa na serikali kwa watu wake. Pum$$$@@@333 zao!

JAMANI TUMETUKANWA, TUSI KUBWA TUMEITWA MABWEGE NA MAZEZETA.

SERIKALI IMEFANYA MAUAJI YA KIMBARI - IMESHINDWA KUWASIKILIZA MADAKTARI KWA WAKATI PALE WALIPOLETA MADAI YAO, WAKAFANYA DHIHAKA NA LEO WATU WANAKUFA HOSPITALI KWA SABABU YA MGOMO WA MADAKTARI - DAMU HII NA IWE JUU YENU SERIKALI YA CCM AMBAYO SASA IKO WAZI KUWA NI SERIKALI YA NGUVU YA GIZA.

Matusi haya yatawarudia (WANA JF HESABUNI SIKU SABA - 7 KUANZIA LEO) MUONE MATUSI HAYA YATAKAPOIRUDIA SERIKALI HII KWA KISHINDO CHA KULITIKISA TAIFA, MAANA MACHOZI YA WATANZANIA YAMEFIKA KWA MUNGU.
 
Wewe mtoa hii mada ndo unamatatizo makubwa sana. We utatamanije kuwa JK bana!!?? Huyu JK hivi unamjua vizuri wewe?????
 
Acha matusi mkuu. Kwa kauli zilizokwisha tolewa na viongozi hao, hakuna udangayifu wowote, bali wamekuwa wakitolea ufafanuzi upotoshwaji juu ya suala zima za posho za Wabunge. Hata kama wangekuwa wamepitisha nani mwenye kosa hapo wabunge waliopendekeza posho hizo au Rais, Waziri Mkuu au Spika. Tujaribu kutafakari sana kabla ya kulaumu. Nakumbuka wabunge wengi tu walikubaliana kupandishiwa posho wakiwemo wa upinzani. HAPA NANI ANAWADANGANYA WATANZANIA? Rais, Waziri Mkuu na Spika au WAbunge. Mimi naona ni Wabunge. Tujaribuni kwenda na facts badala ya hisia binafsi.

wapinzani wapi hao??shibuda nae unamuita mpinzani?? au wale ccm b nao ni wapinzani.acha hizo ndugu.
 
Wewe mtoa hii mada ndo unamatatizo makubwa sana. We utatamanije kuwa JK bana!!?? Huyu JK hivi unamjua vizuri wewe?????

Hizi ni ndoto za mchana.... labda useme kwamba ungekuwa Rais kitu ambacho ukitia nia unaweza kuupata.... lakini unaposema ungekuwa JK sikuelewi!
 
  • as far as I know ni kwamba Rais anatudanganya kwasababu wabunge walishaanza kulipwa tangu kikao kilichopita na zilianzaje kutolewa kama hazikubarikiwa na Rais? Rais hana msimamo.......
 
Kama kweli wewe naye unajiita great thinker, basi humu JF tumeishiwa. Kama baba yako aliyekuzaa akikutukana huwezi kujisikia vizuri ukimtukana wewe yeye atajisikiaje. Kama Initials za majina ya watu zingekuwa zinamaanisha Matusi sijui ingekuaje, hebu tupe initials za jina lako na wewe tukutafutie tusi lako. Kiongozi yeyote ambaye ni RIGID ndugu yangu siyo kiongozi huyo. Kiongozi anayejali Demokrasia na utawala bora lazima awe Flexible, ndiyo maana Viongozi wa CDM (SLAA na MBOWE ) wanapeleka chama wanavyojua simply because they are Rigid. Hakuna anayethubutu kuwakosoa na kuwashauri. Angalia mahusiano ya ZITTO na viongozi wakuu wa CDM na mahusiano na watu kama LEMA na SUGU na viongozi hao ni tofauti kabisa kwa sababu ZITTO hawanyeyekei na pale wanapokwenda kinume anatofautiana nao( mfano ni walipotoka nje ya ukumbi wa bunge wakati President anahutubia, ZITTO alibaki). Lema na Sugu wanakubalika kwa viongozi hao kwa sababu wanafuata nyao zao kama vile kuanzisha vurugu na n.k
kwa mtazamo wangu JK siyo kigeugeu bali ni Kiongozi anayekubali ushauri, madilko na hali halisi kulinagana na mazingira ya wakati huo.

wewe ni muongo siku hiyo zito hakuwepo kabisa ndani ya bunge umbea tu
 
Back
Top Bottom