Pinda, Muungano, na Hatima ya Zanzibar

Vuia Ndo waziri kiongozi! yeye ameshatumia hekima ktk kujibu!

Wacha hao mawaziri wadogo waendelee kutumia jazba!
 
Kama wanaona hawapo huru si wadai na ikishindika si warudie mapinduzi!
 
Vuia Ndo waziri kiongozi! yeye ameshatumia hekima ktk kujibu!

Wacha hao mawaziri wadogo waendelee kutumia jazba!

Sawa kwa kumsifia Vuai. lakini mbona hushauri kuwa Pinda naye afuate nyayo za Vuai. Kwa nafasi yake aliyonayo matamshi yake yasiyo na busara (yaliyojaa ubabe) ni karaha -hayo matamshi si awaachie akina Mh. Seleli na wenzake wale wa back-bench.. Pinda mambo yanamzonga Bwana!!!!
 
Waungwanae; mimi mwenyewe naona ni vizuri mazanzibaaaaariiiiiiii! WAJITOE TU. Kwani naona wanaleta vitisho visivyokuwa na msingi. Siku muungano ukivunjika,wao ndio watakao umia zaidi kuliko Tanganyika. Ukifanya utafiti mdogo tu sasa hivi, utagundua kuwa biashara ya zanzibar inategemea sana bara: kama haitoshi, kama muungano ukivunjika,lazima wapemba watalia kwani biashara ya pilipili na mbogamboga inayowaweka mujini daresalamaaaaa! itakufa. Muungano uendelee.
 
Kauli ya Pinda ni za Uhani- Hamza


Na Mwantanga Ame



SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema kauli ya Waziri Mkuu Mizengo Peter Pinda kutaka muundo wa Muungano wa serikali moja ni Uhaini kwa kuwa inadhamiria kufuta Serikali ya Mapinduzi Zanzibar iliyopo kihalali. Hata hivyo, Waziri wa Nchi, Afisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Hassan Juma alisema kuwa matamshi hayo ni mawazo Pinda binasfi.



Kauli ya Waziri Hamza imekuja baada ya Waziri Mkuu huyo kuliambia Bunge kuwa matatizo yanayojitokeza katika kero za Muungano yatamalizika kwa kuwa na nchi moja yenye serikali moja. Pinda alitoa kauli hiyo alipomjibu Mbunge wa Ziwani Ali Said Salim(CUF) aliyetaka kujua mambo ambayo sio ya Muungano yanaongozwa kupitia serikali gani wakati mambo ya Zanzibar yanasimamiwa na serikali ya Zanzibar. Pinda aliliambia Bunge kwamba suluhu ya matatizo hayo ni nchi moja na serikali moja na kelele zote zitamalizika.



Hivi karibuni Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi walipinga kauli ya Pinda aliyoitoa baada ya SMZ kutangaza msimamo wa BLM wa kuliondoa suala la uchimbaji mafuta na gesi asilia katika mambo ya Muungano. Waziri Mkuu huyo alipingwa na Viongozi wa SMZ na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi baada ya kutoa majibu kwa Mbunge wa Nzega, Mheshimiwa Lukas Selelii, alietaka kujua sababu za viongozi wakuu kukaa kimya kuhusu matamshi ya viongozi waandamizi kutoka Zanzibar kuhusu suala la mafuta huku akidai kuwa yanauweka Muungano katika hali tete na kuitishia SMZ.



Hamza alisema Kauli ya hivi karibuni ya Waziri Mkuu huyo ni sawa na Uhaini kwani ina lenga kuiondoa madarakani Serikali ya Zanzibar na ipo kwa Katiba. Alisema kauli hiyo haitaweza kuifuta Serikali ya Zanzibar kama alivyoelezea Waziri Mkuu huyo kwa vile imewekwa na wananchi wa Zanzibar ambao ndio wenye uwezo wa kuiondoa.
Alisema ni vyema Waziri Mkuu anapotoa kauli kuhusu serikali ya Zanzibar kuwa makini kwani zimekuwa zikiashiria kuleta migongano kwa pande mbili za Muungano.



Alifahamisha kwamba msimamo wa Serikali ya Zanzibar utabakia kuwa ni wa serikali mbili na hakuna atakayeweza kuifuta Zanzibar. Alisema ingawa Waziri Mkuu katoa kauli hiyo kutokana na wadhifa wake, lakini bado inaashiria hatari kwani pindipo litapojitokeza jambo la aina yoyote linaweza kumgeukia yeye binafsi."Watu wenye kazi zao wapo; litakapotokea jambo basi kauli kama hii ijulikane kuwa hakuna mdogo wala mkubwa atakayeachwa kushughulikiwa ipasavyo. Na serikali ya Zanzibar itakuwepo na itaendelea" alisema. Alifahamisha kuwa serikali ya Zanzibar itaendelea kuwepo na wananchi wasiingiwe na hofu kwa matamshi hayo.



Waziri Hamza alitoa matamshi hayo ndani ya Baraza la Wawakilishi ambapo wajumbe kadhaa wa Baraza hilo waliyaunga mkono mbele ya Spika wa Baraza, Mheshimiwa Pandu Ameir Kificho, kabla ya kikao hicho kuakhirishwa.
 
huyu PM mi nilishasema huko nyuma anatoa kauli za kukurupuka mno.akibanwa anaanza kulia
 
PM pengine bado anajifikiria kuwa akiwemo Bungeni mle yumo kama wakati ule alivyokuwa TAMISEMI au yumo kama akina Mheshimiwa Seleli. Anasahau kuwa ni Waziri Mkuu tena wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na busara zake zinahitajika sana katika matamshi.
 
Tatizo Pinda anachuki binafsi na Zanzibar na Wazanzibar, we tazama navyo-collabo na waziri wake Masha kuchochea machafuko ktk uchaguzi mkuu ujao, maelfu ya askari wanini zanzibar, si wangeishinikiza serikali yao ya kimamluki kukubali kufanya uchaguzi huru na wa haki, kusinge hitaji kupelekwa hata mgambo ingekuw shwari kabisa lakini kwa kuwa hana haja na usalama wa raia na mali zao zanzibar ndo anachochea vurugu makusudi.
 
Mkuu Ndivyo Ilivyo nakuunga mkono kabisa.hivi kweli PM unasimama unazungumza kwa niaba ya serikali unasema kama mnataka muungano uvunjike jaribuni muone!!!!!ni hatari sana kuwa na PM wa namna hii..majibu yake yamekaa kimipashomipasho sana
 
MIAFRIKA NDIVYO TULIVYO..

Ndugu zangu nadhani umefika muda nami niandike kitabu changu kuhusu Miafrika Ndivyo Tulivyo kisha nimlipe Nyani Ngabu fidia ya jina hili..
Hivi kusema kweli Ugonvi kati ya Zanzibar na bara, kitu gani haswa!.. Yaani kesho tukisema Zanzibar ni nchi, kitaongezeka kitu gani kwao zaidi ya PRIDE..kuwa sasa hivi zanzibar inajulikana kama nchi..Tangayika haipo na wala haijulikani hilo tatizo lao wenyewe wamependa iwe hivyo.. so what comes with this recognition! maanake kama ni serikali ya Zanzibar (SMZ) ipo na wana viongozi wao, bunge lao, utawala wao..na mfumo uliopo sasa hivi kama sikosei kwa wazanzibar ni Changu Changu, Chako Changu!..

Mapato yote ya Zanzibar ni ya Wazanzibar isipokuwa wanachogombea ni mkato zaidi toka serikali ya Muungano. sasa ikiwa chenu hakiwatoshi na sababu kubwa ya kuvunja muungano ni kile kinachotoka bara ktk serikali ya muungano mnagawiwa kama mkoa kinawauma, Mkijikata mtapata kipi zaidi na toka wapi? au hii kitu mafuta ndio inawatoeni roho!..What if mafuta hayo yapo kati ya Bara ya Zanzibar (offshore) nani mwenye mali hiyo na kipimo gani cha mipaka kimewekwa baina ya bara na Zanzibar ndani ya maji!..
Tanganyika imeua jina la nchi yake na kuwajulikana kwa mikoa tu, leo imekuwa sababu ya zanzibar kudai nchi ambayo tayari wanayo isipokuwa jina tu ndio halitumiki..Hii kitu gani jamani?..

Ama kweli naamini maneno ya CIA mmoja aliyejiuzuru alipohojiwa jinsi wanavyofanikiwa kuzigombanisha nchi maskini.. na akasema tefauti na matumizi ya FEAR kwa nchi za Ulaya, mwafrika mgombanishe kwa PRIDE..
alifafanua na kusema, Waafrika watauana wao kwa wao kwa sababu ndogo sana ya pride. Watagombea kipande cha ardhi ktk shamba kubwa hata iwe futi moja utafikiri kipoande hicho kina maana kubwa sana kwao, lakini ajabu siku ya mavuno utawakuta hao hao wagonvi waki share mavuno zaidi ya kipande kile cha ardhi..Ndio hayo ya kina Raila na huyo Morgan ambao wamesababisha maelfu kuliwa, walipopewa cheo tu wamesahau kabisa kile walichokuwa wakigombania..wanakula sahani moja na shetani.

Ukielewa jinsi Pride kuwa ndio kiini cha umaskini na magonvi yote ya mtu mweusi basi hili swala la Muungano halina tofauti kabisa, na hakika - Miafrika NDIVYO TULIVYO..
 
Last edited:
Tatizo la viongozi wa ZNZ ni UELEWA wao una hitilafu kidooogo,Manake haiwezekani kila linalozungumzwa upande wa pili lionekane ni balaa,PM siku ile alichokisema ni kwamba,ANGEOMBEA siku moja katika maisha yake angeiona serikali moja tu ya TANZANIA ndio mambo haya yangekwisha,which is true,kwani zogo loote hili linasababishwa na nini????ukweli ni kua huwezi kuwa na nyumba moja yenye watu wenye nguvu sawa,hapo lazima zogo litokee tu.Lakini utashangaa waziri mkubwa kabisa katika ofis ya waziri kiongozi(Mh HAMZA) anakurupuka na kuzusha jipya tena zito as if PM alisema kwamba SMZ iwe dissolved kesho hivi,nina wasiwasi huenda ikawa wanayatumia magazeti zaidi kujibu hoja,kuliko kuuona ukweli moja kwa moja wao wenyewe.MAnake mimi siku hio nimeona kwa macho yangu PM akijibu swali,na hakusema kwamba wanakusudia kuifuta SMZ,kesho yake magazeti yakatoa headlines kubwakubwa,tena za kutisha,na muheshimiwa huyu katika SMZ anaijibu kama alivyoisoma kwenye Mwananchi,au Tanzania DAima hivi.
 
Last edited:
Nakushukuru sana King wa Kwetu kwa bandiko lako. Kumbe sasa hata na mimi naliona tatizo liko wapi. Ni vyombo vya habari vichonganishi vinavyoendeshwa na watumishi (vihiyo, wasiojali taaluma zao na pengine labda ni mamluki). Kama PM alisema kama hivyo ulivyosema wewe- sasa ana kosa gani? Si amelizungumza hilo kwa lugha njema tu yenye busara. Nafikiri ni kweli vyombo vya habari vyengine vianatuyumbisha na hasa hao waandidhi wake (na Wahariri) makanjanja.
 
Huyu mzee mchemfumu tu, sijawahi ona mtawala anayeropoka kama huyu, he dont deserve to be called PM
 
MIAFRIKA NDIVYO TULIVYO..

Ndugu zangu nadhani umefika muda nami niandike kitabu changu kuhusu Miafrika Ndivyo Tulivyo kisha nimlipe Nyani Ngabu fidia ya jina hili..
Hivi kusema kweli Ugonvi kati ya Zanzibar na bara, kitu gani haswa!.. Yaani kesho tukisema Zanzibar ni nchi, kitaongezeka kitu gani kwao zaidi ya PRIDE..kuwa sasa hivi zanzibar inajulikana kama nchi..Tangayika haipo na wala haijulikani hilo tatizo lao wenyewe wamependa iwe hivyo.. so what comes with this recognition! maanake kama ni serikali ya Zanzibar (SMZ) ipo na wana viongozi wao, bunge lao, utawala wao..na mfumo uliopo sasa hivi kama sikosei kwa wazanzibar ni Changu Changu, Chako Changu!..

Mapato yote ya Zanzibar ni ya Wazanzibar isipokuwa wanachogombea ni mkato zaidi toka serikali ya Muungano. sasa ikiwa chenu hakiwatoshi na sababu kubwa ya kuvunja muungano ni kile kinachotoka bara ktk serikali ya muungano mnagawiwa kama mkoa kinawauma, Mkijikata mtapata kipi zaidi na toka wapi? au hii kitu mafuta ndio inawatoeni roho!..What if mafuta hayo yapo kati ya Bara ya Zanzibar (offshore) nani mwenye mali hiyo na kipimo gani cha mipaka kimewekwa baina ya bara na Zanzibar ndani ya maji!..
Tanganyika imeua jina la nchi yake na kuwajulikana kwa mikoa tu, leo imekuwa sababu ya zanzibar kudai nchi ambayo tayari wanayo isipokuwa jina tu ndio halitumiki..Hii kitu gani jamani?..

Ama kweli naamini maneno ya CIA mmoja aliyejiuzuru alipohojiwa jinsi wanavyofanikiwa kuzigombanisha nchi maskini.. na akasema tefauti na matumizi ya FEAR kwa nchi za Ulaya, mwafrika mgombanishe kwa PRIDE..
alifafanua na kusema, Waafrika watauana wao kwa wao kwa sababu ndogo sana ya pride. Watagombea kipande cha ardhi ktk shamba kubwa hata iwe futi moja utafikiri kipoande hicho kina maana kubwa sana kwao, lakini ajabu siku ya mavuno utawakuta hao hao wagonvi waki share mavuno zaidi ya kipande kile cha ardhi..Ndio hayo ya kina Raila na huyo Morgan ambao wamesababisha maelfu kuliwa, walipopewa cheo tu wamesahau kabisa kile walichokuwa wakigombania..wanakula sahani moja na shetani.

Ukielewa jinsi Pride kuwa ndio kiini cha umaskini na magonvi yote ya mtu mweusi basi hili swala la Muungano halina tofauti kabisa, na hakika - Miafrika NDIVYO TULIVYO..


Kwanini huwi muungwana na kukubali Wazanzibari watumie kilicho chao?
Hii kauli ya "Changu changu ... Chao changu " mbona unaigeuza?
Kwani Zanzibar ilishadai kitu gani kutoka bara kuwa ni chao? Kwa sasa bara wana madini, mapori na maziwa makubwa, jee ulisikia zanzibar ikidai ipatiwe mgao? Jee umesikia lini pato a inayoitwa Serikali ya Muungano likakasimiwa na kutiwa kwenye Bajeti ya Zanzibar? Ukisikia asilimia 4.5 ni kwa mapato ya misaada inayokuja kwa jina la Tanzania. Sasa wapi inapply hiyo chenu changu? Umeme zanzibar wanaadhiriwa kila siku kwa kuchelewa kulipa.
Naona hivi Muungwana huwa hanganganii ujinga wa mtu na kwa vile Wazanzibari ni wajinga kwa kungangania mafuta yasiopo basi nyie mlio sio wajinga ni bora mkawachia na ujinga wao na hapo mtakaspothibitisha ujinga wao itakuwa wakati mzuri wa kuwacheka lakini kwea sasa Wazanzibari wanataka chao na ni haki kupewa basi!
 
Ngekewa.

Sijasikia Zanzibar kuwa wana jeshi lao. Sijasikia kuwa Zanzibar wana polisi wao.Sijasikia kuwa Zanzibar wana balozi zao. Sijasikia kuwa wabunge kutoka Zanzibar wanalipiwa na SMZ. Sijasikia kuwa wazanzibari wakitibiwa Muhimbili wanalipa tofauti. Sijasikia kuwa wazanzibari wakisoma katika shule na vyuo vilivyoko bara wanalipishwa tofauti. Mambo yote haya yanagharamiwa na SMT ambayo mapato yake ni kutokana na hayo madini, mapori n.k. yaliyopo bara.Zanzibar walikuwa wanauziwa umeme kwa bei ya chini kuliko bara. Hiyo tofauti ilikuwa inalipwa na nani? Mnaposema Zanzibar haifaidiki na rasilmali zilizokuwepo bara mna mana gani? Mlitaka mfaidike vipi? Mfanyiwe kama Alaska, kila mzanzibari apewe mgao wa Tanzanite ndiyo mridhike?
Mkandara hakukosea.

Amandla........
 
Kwanini huwi muungwana na kukubali Wazanzibari watumie kilicho chao?
Hii kauli ya "Changu changu ... Chao changu " mbona unaigeuza?
Kwani Zanzibar ilishadai kitu gani kutoka bara kuwa ni chao? Kwa sasa bara wana madini, mapori na maziwa makubwa, jee ulisikia zanzibar ikidai ipatiwe mgao? Jee umesikia lini pato a inayoitwa Serikali ya Muungano likakasimiwa na kutiwa kwenye Bajeti ya Zanzibar? Ukisikia asilimia 4.5 ni kwa mapato ya misaada inayokuja kwa jina la Tanzania. Sasa wapi inapply hiyo chenu changu? Umeme zanzibar wanaadhiriwa kila siku kwa kuchelewa kulipa.
Naona hivi Muungwana huwa hanganganii ujinga wa mtu na kwa vile Wazanzibari ni wajinga kwa kungangania mafuta yasiopo basi nyie mlio sio wajinga ni bora mkawachia na ujinga wao na hapo mtakaspothibitisha ujinga wao itakuwa wakati mzuri wa kuwacheka lakini kwea sasa Wazanzibari wanataka chao na ni haki kupewa basi!
Mkuu wangu pengine wewe huelewi bajeti ya serikali mbili zilizoungana inakwenda vipi.. Na hii ndiyo tofauti ya kuelewa kwenu.
Nitajaribu kukufahamusha naposema Changu Changu, Chako Changu wala sii kinyume...nitakubali tu kupata elimu (somo) toka kwako ikiwa kinachofanyika ni kinyume na kuelewa kwangu..
Mkuu kwanza hii ni lugha inayotumiwa kila siku na lazima uifahamu vizuri mtililiko wake laa sivyo utaona maji hayafuati mkondo - maluweluwe!
Serikali ya Zanzibar haiwezi kudai wala kuwa na bajeti inayotegemea bara ktk bunge lake kwa sababu hii ni serikali nzima inayoingia ktk muungano wetu..hili gumu nalo mkuu wangu kuhafamu, labda pitia na utazame site ya bunge lake upate kuelewa kuwa hakuna mwakilishi wa bara hata mmoja.. site hii Hapa.

Hivyo kile kinachopatikana Zanzibar pato la makusanyo ya kodi zao ndicho kinachounda bajeti ya Zanzibar, wanachagua mawaziri wao na viongozi wao bila kumshirikisha Mbara yeyote wala bara hawakatiwi kitu toka bunge hilo maanake sii mali yao..ndio naposema Changu Changu..Yaani kinachochumwa Zanzibar kinabakia Zanzibar.

Sasa ukija tazama upande wa bara, hawa hawana serikali kama ya Zanzibar ama utaratibu unaofanana na huo wa visiwani.. Seikali yao (Tanganyika) imekwisha kufa siku nyingi pamoja na kwamba nyie mnahofia kifo cha serikali ya Zanzibar au hilo jina la Zanzibar na sijui kutoitwa Zanzibar ni nchi..Tanganyika sii serikali, sii nchi wala hakuna jina Tanganyika ktk ramani wala fikra za watu miaka 45..Na hakuna hata haja ya kumwambia mtu kuwa Tanganyika sio NCHI kwani haipo kweli.

Jambo ambalo linanishinda kuelewa sijawahi kuwasikia Wazanzibar wakilalamika na uonevu huo kwa Tanganyika, na kuuliza kwa nini muungano uliua nchi iitwayo Tanganyika, ikiwa kweli nyie ni Waungwana wenye mapenzi na haki maanake haki haiwezi kusimama tu kwa mahitaji yenu isipokuwa kwa kila atakaye tendewa kinyume cha haki..itokee nchi yoyote, mahala popote duniani nilitegemea kwamba wananchi na viongiozi wa zanzibar wataipinga mfumo unaovunja jina na kupora haki ya watu kuwa na NCHI yao..
Maajabu ya mwafrika imewatokea usoni mwao lakini hawakuona ubaya wowote Tanganyika kupoteza serikali, nchi na jina lake ila itauma tu ikiwa Zanzibar itapoteza vitu hivyo.. (mkuki kwa nguruwe)

Pili, napozungumzia Chako Changu ni kwamba mapato yote ya madini, maziwa maji na kadhalika ni mapato ambayo yanatengeneza Bunge la muungano ambapo pato lake linalotengeneza bajeti haligawiki kwa madini au maziwa ila makusanyo ya kodi zote. Hivyo Barricks wanapolipa kodi huingia ktk mfuko wa Taifa, samaki wa Kanda ya ziwa wanapouzwa Ulaya nchi za EU pato lake (kodi zake) huingia ktk mfuko wa Taifa.. Hivyo kila kitu kilichopatikana toka mfuko wa Taifa kwa jumla ya kodi zote ndio hutengeneza bajeti ya serikali ya Muungano ambayo Zanzibar pia imo na ina wawakilishi wake tofauti na ile ya Zanzibar..

Kumbuka tu ktk pato hilo la mfuko wa Taifa, Zanzibar haikuingiza hata chapa, lakini bajeti ikisomwa huambatanisha matumizi kwa visiwa vya Pemba na Unguja. Ukitaka pia pitia site ya Bunge la muungano utaona wawakilishi kibao na hata bajeti zinazohusu matumizi ya visiwani..site hii Hapa.

Hivyo visiwa hivi hupata pango lake toka bajeti yao wenyewe na kisha toka bunge la muungano. Bara wanachotegemea ni toka Bunge la Taifa tu ambako kila mkoa na wilaya zake hukatiwa ktk fungu moja na mikoa ya visiwani pamoja na kwamba pato zima limetoka bara..
 
Ngekewa.

Sijasikia Zanzibar kuwa wana jeshi lao. Sijasikia kuwa Zanzibar wana polisi wao.Sijasikia kuwa Zanzibar wana balozi zao. Sijasikia kuwa wabunge kutoka Zanzibar wanalipiwa na SMZ. Sijasikia kuwa wazanzibari wakitibiwa Muhimbili wanalipa tofauti. Sijasikia kuwa wazanzibari wakisoma katika shule na vyuo vilivyoko bara wanalipishwa tofauti. Mambo yote haya yanagharamiwa na SMT ambayo mapato yake ni kutokana na hayo madini, mapori n.k. yaliyopo bara.Zanzibar walikuwa wanauziwa umeme kwa bei ya chini kuliko bara. Hiyo tofauti ilikuwa inalipwa na nani? Mnaposema Zanzibar haifaidiki na rasilmali zilizokuwepo bara mna mana gani? Mlitaka mfaidike vipi? Mfanyiwe kama Alaska, kila mzanzibari apewe mgao wa Tanzanite ndiyo mridhike? Mkandara hakukosea.

Amandla........

,,,,,,eeh bana eeh,, na Mikopo ya Elimu ya Juu,hili fuko jipya la JIMBO nalo,Ofisi za Wabunge katika kila JIMBO na hata ile tower ya BoT branch pale KINAZINI haifanani kabisa na BRANCHES nyengine za BoT huko Tanganyika(sijui ndio katika kutupamba tuu),,,,,,,mmmh ni mengi mwanangu NGEKEWA lakini ndio vile tena hatuelewi ha haaaaaa!!!!!!!,,ipo kazi hapa.
 
Ngekewa.

Sijasikia Zanzibar kuwa wana jeshi lao. Sijasikia kuwa Zanzibar wana polisi wao.Sijasikia kuwa Zanzibar wana balozi zao. Sijasikia kuwa wabunge kutoka Zanzibar wanalipiwa na SMZ. Sijasikia kuwa wazanzibari wakitibiwa Muhimbili wanalipa tofauti. Sijasikia kuwa wazanzibari wakisoma katika shule na vyuo vilivyoko bara wanalipishwa tofauti. Mambo yote haya yanagharamiwa na SMT ambayo mapato yake ni kutokana na hayo madini, mapori n.k. yaliyopo bara.Zanzibar walikuwa wanauziwa umeme kwa bei ya chini kuliko bara. Hiyo tofauti ilikuwa inalipwa na nani? Mnaposema Zanzibar haifaidiki na rasilmali zilizokuwepo bara mna mana gani? Mlitaka mfaidike vipi? Mfanyiwe kama Alaska, kila mzanzibari apewe mgao wa Tanzanite ndiyo mridhike? Mkandara hakukosea.

Amandla........

La Zanzibar wana vikosi vya ulinzi vyenye idadi kubwa kuliko hao olisi na hao hulipwa na SMZ (Hii ni kuonyesha kuwa hakuna ulazima wa kuwepo kwa hao Polisi wa Muungano, huko kunakofanywa ni kufuja fedha zenu bure. Nini sababu ya hili ? ni kujidai kuwa Muungano unahudumia Zanzibar)
Wabungw wa Zanzibar wana faida gani kuwepo katika Bunge ambalo linashughulikia MAMBO YA BARA TU? Ni ile ile, kupoteza gharama ili tu kuwepo ushahidi kuwa kuna huduma zinatolewa kwa Zanzibar.
Wazanzibari watakuwa na Balozi zao vipi ikiwa LWENGO la muungano ni kuona kuwa Zanzibar haina mahusiano ya moja kwa moja na mataifa mengine kwani kwa kufanya hivyo itakuwa rahisi kwa Zanzibar kuendelea na kuwapita kimaendeleo wenzao.
Suala la matibabu Muhimbili si suala la kuzungumza kwani hakuna mgonjwa kutoka Zanzibar anayepewa rufaa kwenda Muhimbili na ukimuona anakwenda basi anakwenda kwa gharama yake mwenyew na sio kuwa anafuata huduma ya Muungano.

Kuhusu Elimu kwani si mkopo? Na hata hivyo ni nyie mnalazimisha kuwa Wazanzibar wasome vyuo vyenu kwa kuweka vikwazo chungu nzima kwa kuanzishwa Taasisi za elimu kule Zanzibar na halafu kwa kujifanya kuwa nyie ndie wa kupanga, kuchagua na kutathmini mfumo wa elimu kwa nchi mbili tofauti.


Suala la umeme na bei rahisi sio kweli hata kidogo ingawa msaada wa kutengenezea gridi za umeme huwa zinaombwa kwa jina la Tanzania. Kama Zanzibar haihusiki ni kazi ndogo tu , waruhusuni wawe na mawasiliano moja kwa moja katika kuomba misaada yao.

Tunaposema kuwa hatufaidiki na rasilimali za Bara tuna maana faida ya moja kwa moja inayokwenda kwa mwananchi na sio pesa mnazowapa watu fulani tu hiyo aidha ni ujira wao kwa kukutumikieni katika kuitawala Zanzibar au ni hongo ili wawe watumishi wa matakwa yenu.
Hayo iliyoyafikiri wewe kuwa ni kufaidika kwa Zanzibar si chengine bali ni KERO kwa Wazanzibari kwani kwa ubabe wenu mnalazimisha kuifanya Zanzibar ionekane inawategemea wakati ambapo hamkuwa na haja ya kufanya hivyo kwani HAKUNA UMUHIMU wa gharama mnazojitia.
 
Back
Top Bottom