Kachocho T.K
Member
- Feb 1, 2011
- 25
- 3
Pamoja na kuwepo watu kiduchu waliohudhuria mkutano wa waziri mkuu uliofanyika wiki iliyopita kwenye viwanja vya uhuru platform mjini Bukoba, maarufu kama mayunga, Bwana pinda alishindwa kutoa tamko la serikali kuhusu bei halisi ya sukari. Wananchi wakiwa wapweke na kuonekana kama wako sehemu ya ibada wakati yeye akihutubia mkutano wa hadhara, walibadilika na kushangilia pale pinda alipogusia suala la sukari kupanda bei mjini abukoba na maeneo mengine wakati kiwanda cha sukari kipo km 70 tu kutoka mjini Bukoba. Aliishia kusema haiingii akilini kuona kiwanda kipo km 70 kutoka hapa halafu wananchi wanunue sukari kwa sh 2,000 hadi elfu 2,200 wakati wakazi wa Dar. wanapata sukari kwa sh1,800 kwa sukari hiyo inayotoka kagera. Aliwavunja watu mbavu na kurudia hali ya kusononeka pale aliposema nimemwagiza mkuu wa mkoa kubaini wasambazaji wa sukari mkoani humu kisha wakae chini na kuangalia sababu za kupanda kwa bei ya sukari na kutafuta njia mbadala.
Hivi kweli kulikuwa na haja ya pinda kupanda jukwaani na kuwaambia wananchi maongezi yake na mkuu wa mkoa? Wananchi walitarajia serikali makini ingekuja na suruhisho la bei halisi wanayopashwa kutoa si maongezi yake na mkuu wa mkoa.
Hivi kweli kulikuwa na haja ya pinda kupanda jukwaani na kuwaambia wananchi maongezi yake na mkuu wa mkoa? Wananchi walitarajia serikali makini ingekuja na suruhisho la bei halisi wanayopashwa kutoa si maongezi yake na mkuu wa mkoa.