BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,005
Pinda awaonya vigogo
Mwandishi Maalumu, Zanzibar
Daily News; Wednesday,January 14, 2009 @20:20
Mwandishi Maalumu, Zanzibar
Daily News; Wednesday,January 14, 2009 @20:20
Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema viongozi serikalini hawana budi ‘kujinyonga' kama kweli wanataka kumsaidia mkulima wa kawaida.Alitoa kauli hiyo jana mchana wakati akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Cheju mara baada ya kukagua mradi wa kilimo cha mpunga katika Bonde la Cheju, Wilaya ya Kati, Kusini Unguja.
"Ninaposema kujinyonga nina maana tubadilike, tuache maneno maneno na tudhamirie yale tunayosema, la sivyo kilimo hakitaweza kuwa uti wa mgongo wa Taifa hili," alisema.
Akifafanua, Waziri Mkuu alisisitiza kauli yake ya kuacha kununua magari ya serikali kama kweli viongozi wamedhamiria kuwasaidia wananchi. Alisema yeye anaposafiri na magari matatu ni sawa na kushika Sh milioni 300 na kwamba anaamini kama zingetumika kununua matrekta, yangepatikana mengi zaidi kuliko hayo magari matatu.
"Ninasisitiza kwamba yote tuyafanyayo, changamoto iko kwetu sisi viongozi … bado hali ya kujipenda ni kubwa sana na wakati mwingine inatufanya tuzibe masikio … na ndiyo maana nikasema semina kwa sasa basi, ili tuonekama tutaokoa fedha hizo," alisema. Alisema: "Katika mwaka huu wa fedha, fedha zilizotengwa na wizara mbalimbali kwa ajili ya semina peke yake zimefikia Sh bilioni 33.
Nilijiuliza nikikataza semina na fedha hiyo tukanunulia matrekta madogo, tutapata mangapi? Kwangu mimi kilimo cha jembe la mkono ni tatizo na bila kulibadili hatutaweza kusonga mbele." Akijibu risala ya wanakijiji hao, alisema serikali kwa sasa inakabiliwa na mtihani mkubwa wa jinsi gani itamsaidia mkulima azalishe kwa wingi zaidi kuliko alivyokuwa akifanya hapo nyuma.
"Gharama ya kisima kimoja ni Sh milioni 12, kama Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja ataacha kununua gari, katika bajeti ijayo mtaweza kukamilisha visima vitano ambavyo mmesema mnavihitaji ili kusaidia kilimo cha umwagiliaji maji katika bonde hili … ninajua hili linawezekana lakini ni lazima viongozi tusimame kidete," alifafanua. Katika risala yao, wakazi wa Cheju waliomba serikali iwasaidie kutengeneza barabara ya kuingia katika bonde hilo ambayo gharama ya kuweka kifusi ni Sh milioni 34.
Pia walisema visima vitatu kati ya vitano havifanyi kazi sababu ya kukosa umeme ambavyo gharama yake ni Sh. milioni 65.WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amesema viongozi serikalini hawana budi ‘kujinyonga' kama kweli wanataka kumsaidia mkulima wa kawaida.
Alitoa kauli hiyo jana mchana wakati akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Cheju mara baada ya kukagua mradi wa kilimo cha mpunga katika Bonde la Cheju, Wilaya ya Kati, Kusini Unguja. "Ninaposema kujinyonga nina maana tubadilike, tuache maneno maneno na tudhamirie yale tunayosema,la sivyo kilimo hakitaweza kuwa uti wa mgongo wa Taifa hili," alisema.
Akifafanua, Waziri Mkuu alisisitiza kauli yake ya kuacha kununua magari ya serikali kama kweli viongozi wamedhamiria kuwasaidia wananchi. Alisema yeye anaposafiri na magari matatu ni sawa na kushika Sh milioni 300 na kwamba anaamini kama zingetumika kununua matrekta, yangepatikana mengi zaidi kuliko hayo magari matatu.
"Ninasisitiza kwamba yote tuyafanyayo, changamoto iko kwetu sisi viongozi … bado hali ya kujipenda ni kubwa sana na wakati mwingine inatufanya tuzibe masikio … na ndiyo maana nikasema semina kwa sasa basi.