Na nyie mmezidi bwana, hakuna zuri kwenu? Mlitaka awaache hata kama wamekosea? Ni vizuri pia mjue kwamba Pinda siyo Rais, ni Rais pekee mwenye mamlaka ya kumtimua yeyote katika nafasi yoyote. Lakini si waziri mkuu anayeweza kumfukuza Ndulu. Ya kupongeza tupongeze, na ya kuponda tuponde. sasa nyie yote mnaponda tu, kwani nyie wapinzani?
Watu hawaoni tena uzuri wowote kwa waziri mkuu wao na serikali yake kwa kua watu wameshaona viongozi wao na serikali kwa ujumla haiwathamini na inazidi kuwafanyia mzaha na usanii. Dalili ya kuchoshwa, sio lazima ni wapinzani bali ni watu wanapenda nchi yao.