Waziri Mkuu Pinda asitisha utekelezaji wa agizo la Magufuli la Bomoa bomoa

Sasa nimekubali kwamba Mungu alipelekewa habari za ufisadi mkuu unaoendelea ndani ya ccm kisha akashuka Tz kuona kama habari hizi alizoziskia zina ukweli.
Na atakuwa ameshukia Dodoma bungeni na kile alichokikuta kule ni harakati za kuchakachua sauti ya wanyonge kupitia spika wa kuchongwa na mafisadi wakishirikiana na wasaliti wachache wa kambi ya wanyonge.
Alichoamua Mungu ni kuwachafulia lugha serikali ya mafisadi ili wasielewane. Kila waziri sasa la lwake, Jk hivi... pinda vile mpaka sasa hata ukiwauliza kauli yao ya mwisho kuhusu Dowans hawakumbuki maana wametoa nyingi zinazotofautiana.
SittaHivi, Mwakyembe hivi... Ngeleja vile...
Chiligati hivi.. Lowasa vile..
Selina na Werema hivi...mkulu vile...
Makamba hivi... pius vile... Yaani vurugu vurugu tu lugha imeshachafuka mnara wa maendeleo haujengeki tena.
Walahi kwa jinsi Mungu alivyoihofisha hii serikali ya Jk, hata mtu ukiisukuma na ubua inaanguka!!!
.
 
Sitaki kuamini bila kusikia wengine walioipata moja kwa moja hiyo habari! Ila kama ni kweli basi magufuli aendelee kuchapa kazi mpaka afukuzwe kwa kutotii agizo la pinda lililopinda! Kujiuzulu ndicho wanachotaka, so, atawafurahisha!
 

Waziri wa ujenzi John Magufuli ameanza kupunguzwa kasi na serikali katika kusimamia zoezi la bomoa bomoa kwenye hifadhi ya barabara baada ya kuagizwa kusimamisha zoezi hilo mpaka itakapoamuliwa vinginevyo na baraza la Mawaziri.
Hatua hiyo ilitangazwa na Waziri mkuu Mizengo Pinda leo wakati akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara mjini Chato ambapo alimwagia Waziri huyo sifa lukuki katika kutekeleza majukumu yake.
Pinda alisema kasi aliyoanza nayo Magufuli katika wizara yake mpya imeitisha serikali na kuwa ameagizwa kusimamisha zoezi hilo mpaka litakapojadiliwa na baraza la mawaziri.
“Rais aliona kwenye bara bara panale lega na kumrudishaMagufuli kwenye wizara hiyo,huyu serikalini tunamwita ‘buldoza’ hata hiyo ameanza kwa speed kubwa na tumwemwagiza asimamishe zoezi hilo mpaka litakapojadiliwa na baraza la Mawaziri”alisema Pinda
Akisema baraza hilo litakaa na kuangalia upya maeneo yaliyopangwa kwa ajili ya bomoa bomoa na kusema kuwa kabla ya kuruhusu zoezi hilo kuendrlea lazima wakubaliane kwanza kwenye baraza la mawaziri.
Akiwahutubia maelfu ya wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara katika shule ya msingi Chato jana jioni Waziri mkuu Pinda alisema inabidi pia itolewe elimu kwanza akidai maeneo mengine bomoa bomoa sio lazima.
Aidha alisema zoezi hilo ambalo lilizua malalamiko nia ya kulisimamisha ni kujipanga upya huku akisisitiza kuwa serikali inamwamini Waziri Magufuli kama kiongozi mwenye uwezo na ilimpa ofisi hiyo ili pia aweze kuwabana makandarasi wazembe.
Pia katika mkutano huo ambao awali waziri Magufuli aliutumia kujifagilia kwa kukiponda chama cha Chadema kilichofanya maandamano ya amani hivi karibuni wilaya kwake,Pinda alisema waziri huyo amekuwa akitumiwa kunyosha mambo kwenye wizara zinazolega lega.
Kasi ya Magufuli ambayo pia inaonekana katika jimbo lake kwa nyumba nyingi zilizo katika hifadhi ya bara bara kuwekewa mkasi wa kuziondoa ilianzia katika ubomoaji wa ofisi za Tanesco jijini Dar es saam zoezi ambalo alisema litaendelea kuyakumba majengo mengi ya serikali.

 
Jk hataki watu wapige kazi kwa juhudi na kumzidi umaarufu yeye so ameona magufuli anakuja kwa kasi ya ajabu na anatishia umaarufu wake. Pia mafisadi km lowasa wanamwogopa magufuli coz wanahofia ataingia kwenye ligi ya kugombea urais 2015 so wamemsihi swaiba jk ampunguze kasi huyu mheshimiwa. Lowasa anataka awe anasikika peke yake kwenye media ili ajisafishe na agombee 2015.
 
pambaf sana ccm! always kasi ya maendeleo hamuiwezi kazi yenu kuiba mali za umma tu.
 
Wazee nimesikia kwenye taarifa ya habari usiku huu kupitia RFA kwamba Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesitisha ubomoaji wa majengo yaliyojengwa ndani ya hifadhi ya barabara nchini kote. Najua ubomoaji huo ulikuwa unafanywa kwa amri ya Mhe. Pombe Magufuli. Hii amri ya Pinda, imekaaje wazee? Au ndiyo mwendelezo wa tabia ile ile ya serikali yetu ya sasa ambapo kila kiongozi anafanya kazi na kutoa statements kadri anavyojisikia? Mhe. Magufuli atajisikiaje?

Kama hiyotarifa inaukweli ninamushauli muheshimiwa magufuri ajiuzulu kulinda eshima yake
 
Magufuli ajiuzulu kwa kuzuiwa kufanya kazi yake kwa ufanisi! That is the next step forward....
 
Mpaka miaka mitano iishe (kama itafika mitani kweli!) tutakuwa tumeona ya kuona na kusikia ya kusikia. Mawaziri wanapingana wenyewe kwa wenyewe utafikiri serikali haina kiongozi.
Sasa amesitisha kwa kumaanisha nini? Ndo kusema yeye amaunga mkono watu waliovunja sheria na kujenga barabarani?
 
Ku over-rule amri ya waziri wake hadharani ni jambo baya sana. Kwa nini wasingejadiliana halafu akamuacha Magufuli asitishe? Hii inaonesha kuwa CCM na serikali yake imechanganyikiwa, kila mtu atakuja na lake irimradi kujisafisha kumbe wanatibuana na kuadhiriana. Kama hakujadiliana na Magufuli mi nashauri Magufuli ajiuzulu tu, maana kafanywa hajui kazi.

Ndiyo maana inasemwa siku zote - ni vigumu kuwa mwadilifu ndani ya serikali isiyo na uadilifu. Hao akina Magufuli, Sita, Mwakyembe hawawezi kuwa effective ndani ya serikali ya chama cha sasa.
 
Waziri Mkuu Mizengo Pinda "Mtoto wa Mkulima", amesema Kazi ya John Pombe Magufuli ni kushughulikia Rushwa iliyokithiri Ujenzi na si kubomoabomoa Nyumba zilizojengwa kwenye hifadhi ya barabara na kwa hivyo amemtaka aache bomoabomoa.

My Take:
Pinda anataka kutuambia kwamba Magufuli kazi yake ni kupambana na rushwa ujenzi kwa hiyo tusahau ujenzi wa miundo mbinu, no wonder sijasikia ujenzi wowote uloanza pamoja na uchapakazi wa Magufuli. Ahadi hii tuisahau.

Lakini Pinda kwa matamshi yake haoni kwamba anavunja sheria kwa kuruhusu watu kujenga kwenye eneo la hifadhi ya barabara? Pinda nilitegemea awe wa kwanza kukemea uvunjaji wa sheria. Hatuna waziri mkuu.

Hivi serikalini bado hakuna collective responsibility? Mambo aliyokuwa anayafanya Magufuli ni kwa kukurupuka kwake, hawakuamua kwa pamoja. Hivi tuna serikali kweli au vurugu na fujo?

Mheshimiwa Magufuli umedhalilishwa, yaani jitihada zote hizo ni bure, ningekushauri ung'atuke, jiunge Chadema, gombea ubunge kwenye uchaguzi mdogo wa Chato utakaofanyika baada ya wewe kujiuzulu, utapewa huo uwaziri baada ya CDM kuchukua nchi.
 
ameona magufuli anamfunika.......pinda haeleweki kabisa sasa anatka kusema kazi ya pombe ni kuzuia rushwa?!!!

huyu kaona watu wanavyobomolea ndo wanazidi kuichukia serikali......
 
Ishu ya kuondoa mabango yaliyowekwa kwenye milki ya barabara kinyume cha sheria inajadiliwa na baraza la mawaziri? Ili iweje? Kumbe hili ni swala la kunegotiate? Basi wawajadili na waliojenga karibu na barabara ili nao wasibomolewe..
 
Nani asiyejua kwamba tunaye the weakest waziri mkuu of all times!

Kazi ya waziri yeyote ni kusimamia sheria zilizopo na si kupambana na rushwa! Hiyo ni kazi ya Takukuru. Kwa mawaziri kusimamia sheria implication ni kwamba wataziba mianya ya rushwa. Sasa kama watu wataruhusiwa kujenga anyhow/where utapambanaje na rushwa?

Kwa kweli nimeboreka na tamko la Pinda. Nadhani bado ana kisilani cha Magufuli kupinga uuzwaji wa kiwanja cha Nyamagana ambapo Pinda akiwa waziri Tamisemi alibariki (to be price nadhani alipokea rushwa)uuzwaji wa kiwanja hicho.
 
Serikali ya Kikwete imepinda, Pinda ajui hata hiyo rushwa ndiyo imefanya watu wajenge kwenye hifadhi za barabara, kwani nani ajui zadok mwenye kampuni ya A1 OUTDOOR ambeye pia ni mfadhili wa CCM amejenga mabango yake kwenye hifadhi za barabara kwa rushwa . Nionavyo hii nchi imekosa viongozi makini kwani CDM inawachanganya mpaka wanakuwa kama wendawazimu fulani.
 
Ndicho kinachonishangaza. Serikali inayoendeshwa kwa umakini na ustaarabu, haiwezi kuwa na statements za viongozi wake waandamizi kama mawaziri zinazokinzana. Nionavyo mimi nadhani Pinda ilikuwa vizuri na hekima kumwita Mhe. Magufuli na kujadiliana nae kuhusu zoezi hilo la bomoabomoa. Baada ya majadiliano, kama ingeonekana ni muhimu zoezi lisitishwe basi amri ya kusitisha angeitoa Mhe. Magufuli mwenyewe na siyo Pinda. Njia hiyo isingejenga taswira mbaya mbele ya wananchi na kwa Magufuli mwenyewe.


Huwezi jua labda Magufuli alikataa kutii hiyo amri na akampa masharti labda atangaze mwenyewe Pinda. Unajua Magufulu hapendi kuwa kigeugeu, kwa hiyo kuna uwezekano mkubwa aliambiwa akakataa sababu kubomoa ni kutii sheria na Magufuli ni mtii sheria siku zote kwa hiyo hawezi kupindisha sheria kisiasa kama Pinda.

Pinda ni mwanasiasa wa kigeugeu tu ili mradi asimuumize mtu, anataka asilaumiwe, hatuna waziri mkuu hapo.
 
Kama anasema kazi kuu ya Magufuli ni kupambana na rushwa ujenzi; basi aanzishe kitengo cha rushwa ndani ya Takukuru na kumpa Magufuli ubosi wa hicho kitengo. Mimi nilitegemea katika misingi ya uongozi bora, mapambano dhidi ya rushwa ni jukumu ambalo should be routine na si kazi kuu ya mtu kupewa wizara. Mtu anapewa wizara kutimiza yale yanayotegemewa kutoka katika wizara huku akihakikisha kuwa hakuna mianya ya rushwa.

Wizara aliyopo Magufuli lengo lake kuu nategemea kuwa ni kuhakikisha miundo mbinu bora ndani ya nchi yetu ikiwemo uwepo wa njia zinazopitika. Kama watu wamejenga katika hifadhi ya barabara na inampasa kama waziri ahakikishe barabara inapita; Pinda anategemea nini. Aende Kenya akaone mwenzie Odinga anavyobomoa magorofa ya watu ambayo yamejengwa katika hifadhi ya barabara na for this, Kenya wako mbali sana katika miundo mbinu.

Yeye aendelee kutetea interests za mafisadi waliojenga kwenye barabara kama hiyo ndiyo kazi aliyopewa kama Waziri Mkuu mwenye dhamana ya nchi.
 
imenishangaza na kunitisha!!!!!!!!!! Kauli ya PM ni umbumbumbu mkubwa.
 
sasa mbona wanamshusha munkari,ye si anafata sheria za ardhi zinasemaje ukikiuka sheria basi haki sahihi ndo inatendeka.serikali imejishtukia ina makosa mengi kuhusu swala la ujenzi. majengo mengi ya serikali na watu mashuhuri yapo kwenye ramani za balabala.
shame on them.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom