Pinda apasua; Tarime, Rorya kutawaliwa kijeshi

Mpita Njia

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
6,997
1,163

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
SERIKALI itazipa wilaya za Tarime na Rorya mkoani Mara hadhi ya mkoa wa kipolisi kuimarisha ulinzi na usalama kukabiliana na wimbi la mauaji ya mara kwa mara katika maeneo hayo.
Akitangaza uamuzi huo mkoani Mara leo (Jumatano Julai 1, 2009) Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda alisema itaazishwa piakambi ya Jeshi la Kujenga Taifa na kuimarisha miundombinu ya barabara kwa madhumuni hayo hayo.
Waziri Mkuu alikuwa akihutubia sherehe za Siku ya Serikali za Mitaa kwenye uwanja wa Mkendo mjini Musoma leo na baadaye alipotembelea maeneo yaliyokumbwa na mauaji katika wilaya za Rorya na Tarime leo (Jumatano, Julai 1, 2009).
Waziri Mkuu pia alisema anatoa miezi sita kwa uongozi wa wilaya hizo na mkoa kwa jumla kuandaa mkakakati na kuuwasilisha serikalini jinsi ya kukomesha mauaji hayo ama sivyo maeneo hayo yatatawaliwa kijeshi kwa kuwa utawala wa kiraia utakuwa umeshindwa.
“Madhumuni ni kuhakikisha amani na usalama wa raia katika maeneo hayo. Serikali imechoshwa na mauaji haya,” alisema.
Katika matukio ya hivi karibuni, zaidi ya wiki moja iliyopita, mpaka sasa watu 32 wameuawa katika mapigno kufuatia wizi wa ng’ombe watano ambao kati yao ng,ombe watatu walipatikana.
Nyumba zaidi ya 400 zimechomwa na watu zaidi ya 3,000 wamekosa mahali pa kukaa.
Serikali imekwishadhibiti ulinzi na usalama katika maeneo hayo kwa kuowangeza nguvu za polisi na imeanza kutoa msaada kwa walioathirika.
Waziri Mkuu alisema ni aibu mauaji kama hayo kutokea nchini kwa hivi sasa lakini inaonekana pia kuwa viongozi wa wa kiraia wa maeneo hayo wameshindwa kazi kwani ni wajibu wao kuyazuia tangu mapema.
Alisema Serikali inachukua hatua za hadhari hivi sasa za muda mfupi, lakini za muda mrefu zitategemea mkakati wa viongozi wa wilaya hizo za Tarime na Rorya na mkoa mzima wa Mara.
Waziri Mkuu pia alitembelea kwa helikopta na kutuaalipata kwenye maeneo yaliyotokea maafa hayo katika wilaya za Rorya na Tarime na kuzungumza na wananchi. Aliambatana na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali SaidMwema ambaye amekuwepo mkoani Mara kwa siku kadhaa akiwa na baadhi ya makamanda wake wakuu.
Katika eneo la Changuge, wilayani Rorya, wananchi waliopewa nafasi na Waziri Mkuu kutoa kero zao walimthibitishia kuwa mauaji hayo siyo ya kikabila na ya koo kati ya Wakurya wa Tarime na Wajaluo wa Rorya bali ni kati ya raia wema na majambazi wezi wa mifugo.
Waliiomba Serikali kuimarisha ulinzi kwa kuongeza askari polisi na zana.
Mbunge wa Rorya, Prof. Philemon Sarungi alimwambia Waziri Mkuu kuwa zaidi ya ng’ombe 2,000 wameibiwa mpaka sasa katika wizi huo.
Katika maeneo hayo yaliyokuwa na mauaji, Waziri Mkuu alifuatana pia na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali Said Mwema.
Akizungumzia Siku ya Serikali za Mitaa, Waziri Mkuu alisema kuendeleza kwa pamoja sekta za kilimo, mifugo na uvuvi, ndiyo njia pekee ya kuondoa umasikini nchini.
Waziri Mkuu alisema kuwa kuanzia sasa, uongozi bora wa Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya,Wenyeviti wa Halmashauti na Wakurugenzi, utapimwa kwa jinsi wanavyohimiza na kusimamia kwa vitendo kilimo, ufugaji na uvuvi.
Alisema viongozi waonyeshe uongozi wao kwa vitendo huko vijijini na siyo kukaa ofisini tu mijini.
(mwisho)
Imetolewa na:
Ofisi ya Waziri Mkuu
S.L.P. 3021
DAR ES SALAAM
Jumatano Julai 1, 2009

 
Jamani....watu wanakufa, tena wanataka miezi 6 kuandaa mkakati? kwani ni kipi ambacho hakifahamiki kuhusu hayo mauaji miaka nenda rudi? kwa nini wasianze kutawala 'kijeshi' hadi hapo watakapokuwa wamekuja na 'mkakati'...kama hiyo itakuwa na maana ya kuponya maisha ya watu?
 
Jamani....watu wanakufa, tena wanataka miezi 6 kuandaa mkakati? kwani ni kipi ambacho hakifahamiki kuhusu hayo mauaji miaka nenda rudi? kwa nini wasianze kutawala 'kijeshi' hadi hapo watakapokuwa wamekuja na 'mkakati'...kama hiyo itakuwa na maana ya kuponya maisha ya watu?
Nawashangaa sana
 
Tatizo lililopo hapa ni kwa jeshi la Wananchi,mbali ya polisi ,inaonekana mipaka yetu ipo wazi wala haihitaji njia za panya kuivuka na kufanya ujangili,tuna imani kuwa kazi moja ya Jeshi letu ni kulinda mipaka na hii haimaanishi kuwepo kwenye border post ambazo huwa zinashughulikiwa na migration officers bali waweze kuweka ulinzi wa uhakika ambao utaweza kusniff movement zozote zile ambazo si za kawaida zinazofanyika katika maeneo yasio halali na kuzidhibiti.
Mipaka yetu imezungukwa na nchi ambazo zimepitia mapigano ya muda mrefu kuanzia mpaka wa Msumbiji ambako kuna majambazi yanayoishi katika vichaka vya sehemu hio hawa huweza kuingia mtwara mpaka Lindi na kufanya ujambazi kisha hukimbilia huko ,katika sehemu za mipaka ya Zambia ,Congo Burundi Rwanda nako pia kuna matokeo ya ujambazi na katika mpaka wa na Kenya hapa kuna ujangili wa wizi wa mifugo ambayo ikishaibiwa hukimbizwa kuvukishwa sehemu nyengine na kusababisha ugumu wa ufuatiliaji.
Hivyo ni lazima katika sehemu hizo zilizo critical kuwepo na kambi za kijeshi zilizojizatiti vizuri kiutendaji na ziwe na viongozi wenye kuaminiwa ndani ya jeshi letu ambao watakuwa na usongo na majambazi wa aina hii ya wanaovuka mipaka na pia kuwepo na coordination na mawasiliano ya uhakika katika kulinda pembe zote za mipaka yetu ,hivyo tatizo ni mipaka yetu kuwa na njia zisizo za kawaida ni lazima njia hizi ziwe under control na Jeshi liweze kuziziba na kumpa kisago yeyote yule ambae atakuwa akizitumia bila ya kuwa na sababu za msingi.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


SERIKALI itazipa wilaya za Tarime na Rorya mkoani Mara hadhi ya mkoa wa kipolisi kuimarisha ulinzi na usalama kukabiliana na wimbi la mauaji ya mara kwa mara katika maeneo hayo.
Akitangaza uamuzi huo mkoani Mara leo (Jumatano Julai 1, 2009) Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda alisema itaazishwa piakambi ya Jeshi la Kujenga Taifa na kuimarisha miundombinu ya barabara kwa madhumuni hayo hayo.
Waziri Mkuu alikuwa akihutubia sherehe za Siku ya Serikali za Mitaa kwenye uwanja wa Mkendo mjini Musoma leo na baadaye alipotembelea maeneo yaliyokumbwa na mauaji katika wilaya za Rorya na Tarime leo (Jumatano, Julai 1, 2009).
Waziri Mkuu pia alisema anatoa miezi sita kwa uongozi wa wilaya hizo na mkoa kwa jumla kuandaa mkakakati na kuuwasilisha serikalini jinsi ya kukomesha mauaji hayo ama sivyo maeneo hayo yatatawaliwa kijeshi kwa kuwa utawala wa kiraia utakuwa umeshindwa.
“Madhumuni ni kuhakikisha amani na usalama wa raia katika maeneo hayo. Serikali imechoshwa na mauaji haya,” alisema.
Katika matukio ya hivi karibuni, zaidi ya wiki moja iliyopita, mpaka sasa watu 32 wameuawa katika mapigno kufuatia wizi wa ng’ombe watano ambao kati yao ng,ombe watatu walipatikana.
Nyumba zaidi ya 400 zimechomwa na watu zaidi ya 3,000 wamekosa mahali pa kukaa.
Serikali imekwishadhibiti ulinzi na usalama katika maeneo hayo kwa kuowangeza nguvu za polisi na imeanza kutoa msaada kwa walioathirika.
Waziri Mkuu alisema ni aibu mauaji kama hayo kutokea nchini kwa hivi sasa lakini inaonekana pia kuwa viongozi wa wa kiraia wa maeneo hayo wameshindwa kazi kwani ni wajibu wao kuyazuia tangu mapema.
Alisema Serikali inachukua hatua za hadhari hivi sasa za muda mfupi, lakini za muda mrefu zitategemea mkakati wa viongozi wa wilaya hizo za Tarime na Rorya na mkoa mzima wa Mara.
Waziri Mkuu pia alitembelea kwa helikopta na kutuaalipata kwenye maeneo yaliyotokea maafa hayo katika wilaya za Rorya na Tarime na kuzungumza na wananchi. Aliambatana na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali SaidMwema ambaye amekuwepo mkoani Mara kwa siku kadhaa akiwa na baadhi ya makamanda wake wakuu.
Katika eneo la Changuge, wilayani Rorya, wananchi waliopewa nafasi na Waziri Mkuu kutoa kero zao walimthibitishia kuwa mauaji hayo siyo ya kikabila na ya koo kati ya Wakurya wa Tarime na Wajaluo wa Rorya bali ni kati ya raia wema na majambazi wezi wa mifugo.
Waliiomba Serikali kuimarisha ulinzi kwa kuongeza askari polisi na zana.
Mbunge wa Rorya, Prof. Philemon Sarungi alimwambia Waziri Mkuu kuwa zaidi ya ng’ombe 2,000 wameibiwa mpaka sasa katika wizi huo.
Katika maeneo hayo yaliyokuwa na mauaji, Waziri Mkuu alifuatana pia na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali Said Mwema.
Akizungumzia Siku ya Serikali za Mitaa, Waziri Mkuu alisema kuendeleza kwa pamoja sekta za kilimo, mifugo na uvuvi, ndiyo njia pekee ya kuondoa umasikini nchini.
Waziri Mkuu alisema kuwa kuanzia sasa, uongozi bora wa Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya,Wenyeviti wa Halmashauti na Wakurugenzi, utapimwa kwa jinsi wanavyohimiza na kusimamia kwa vitendo kilimo, ufugaji na uvuvi.
Alisema viongozi waonyeshe uongozi wao kwa vitendo huko vijijini na siyo kukaa ofisini tu mijini.
(mwisho)
Imetolewa na:
Ofisi ya Waziri Mkuu
S.L.P. 3021
DAR ES SALAAM
Jumatano Julai 1, 2009
Mambo yanayotokea Tarime watu wengi hawajui yanatokana na nini, lakini kwa tunaojua tunasubiri wakati ili tuwaanike viongozi wa serikali na CCM kwa jinsi wanavyo - Engineer mikakati dhidi ya Wilaya hizo na malengo yao na Barrick.

Kwenye uchaguzi Tarime askari polisi zaidi ya 2000 walipelekwa na kudhibiti wananchi ili kuitafutia CCM bao la mkono kama la Busanda ili kiibuke mshindi bila mafanikio, sehemu hiyo hiyo iliripotiwa kuna mapigano hadi watu wapatao zaidi ya 50 wanakufa serikali ilikuwa haijaona umuhimu wa kuchukua hatua na sasa inadanganya watu kuwa waliokufa ni 32 wakati watu wengi wanakufa na wanazikwa bila taarifa.
U guyz (CCM) have to check n tafakari about ur crazy n evil move, the life of Tanzanians is worth nothing in ur hands.
 
duh, kaaz kweli kweli..... wakuu wa wilaya, mikoa wako chini ya wizara gani??? na kama wakuu hao wameshindwa kutimiza wajibu, ni wizara gani inatakiwa iwajibike??? nadhani mkulu inabidi aangalie wizara yake, si ndio inaitwa TAMISEMI? hii si ndani ya PM's office?? ha ha haaaaa........

nimeamini sasa kwamba majukumu yetu bado yanatuchanganya.....
 
Huyu jamaa vimulimuli vimeanza kumuingia kichwani..
Pinda ameelezea kilicho kweli kabisa.Ni kitu gani kisichoeleweka juu ya wilaya hizi za watu wanaochinjana kila siku.Democracy is an assumption that can work but only where there is peace.
Kama hakuna amani all good intentions can as well be a song to the birds.
 
Pinda ameelezea kilicho kweli kabisa.Ni kitu gani kisichoeleweka juu ya wilaya hizi za watu wanaochinjana kila siku.Democracy is an assumption that can work but only where there is peace.
Kama hakuna amani all good intentions can as well be a song to the birds.

Hajaeleza chochote cha maana zaidi ya kuchemka. Kwanza kutawala kijeshi maana yake nini? Tafsri ninayopata hapa ni kuwa ni kutumia maguvu bila kujali sheria za nchi. Kama sivyo wanajeshi watafuata sheria kinachowashinda wakuu wa wilaya na mkuu wa mkoa kutumia hizo sheria ni ni? Hata hivyo gavana wa Mara si ni mjeshi mbona watu bado wanachinjana?
Kuhusu watu kuchinjana hilo halihalalishi kauli za kukurupuka kama hizi. Akichinjwa mmoja, wawili, kumi au mia ni kuchinja tu. Albino wamechinjwa sana. Huko Kilosa ni zaidi hata ya Tarime mbona hatujawahi kumsikia akisema haya?
 
wanajifanya kutokujua ni nini kinatokea mbona ze utamu amefuatiliwa kirahisi na haraka hadi kuomba msaaada wa kujasusi Israel. kwa nini wasitumie external intelligence kama jamaa wetu wa UWT wameshindwa. Hii ina mambo mawili, upande mmoja kuna majambazi wanaotokea kenya, somalia, ethiopia na uganda wanashirikiana na wafanya biashara wasio na huruma kuiba ng'ombe. Na wanawachanganya wanainchi ili wajue kuwa wanaibiana wenyewe na hivyo kuuana wao kwa wao.

Lakini tukio la majuzi ni tofauti kwani zimetumika bunduki kama AK47s na G3, hizi ni silaha ambazo wanatumia majambazi kutoka kenya, somalia, ethiopia, burundi, rwanda, na uganda.

Pia vijana wetu wa UWT naomba niwakumbushe kuwa idara za ujasusi za nchi jirani zinaishi kwa kutumia mbinu kama za marekani kwamba wana-engineer uhalifu sehemu zingine zilizo lala usingizi kama TZ ili wapate pesa za kuendesha shughuli zao, mfano ni CIA. Uganda wanaiga hiyo methodology japo kuwa bado hawaja fanikiwa sana, kenya ndo mtindo wao siku nyingi.

hatuna vita sasa hivi je, jeshi wanakazi gani? au wanakula ugali tu, make hata kutetea mabadiriko hawataki wanalea meremeta na deep green.....
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


SERIKALI itazipa wilaya za Tarime na Rorya mkoani Mara hadhi ya mkoa wa kipolisi kuimarisha ulinzi na usalama kukabiliana na wimbi la mauaji ya mara kwa mara katika maeneo hayo.
Akitangaza uamuzi huo mkoani Mara leo (Jumatano Julai 1, 2009) Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda alisema itaazishwa piakambi ya Jeshi la Kujenga Taifa na kuimarisha miundombinu ya barabara kwa madhumuni hayo hayo.
Waziri Mkuu alikuwa akihutubia sherehe za Siku ya Serikali za Mitaa kwenye uwanja wa Mkendo mjini Musoma leo na baadaye alipotembelea maeneo yaliyokumbwa na mauaji katika wilaya za Rorya na Tarime leo (Jumatano, Julai 1, 2009).
Waziri Mkuu pia alisema anatoa miezi sita kwa uongozi wa wilaya hizo na mkoa kwa jumla kuandaa mkakakati na kuuwasilisha serikalini jinsi ya kukomesha mauaji hayo ama sivyo maeneo hayo yatatawaliwa kijeshi kwa kuwa utawala wa kiraia utakuwa umeshindwa.
“Madhumuni ni kuhakikisha amani na usalama wa raia katika maeneo hayo. Serikali imechoshwa na mauaji haya,” alisema.
Katika matukio ya hivi karibuni, zaidi ya wiki moja iliyopita, mpaka sasa watu 32 wameuawa katika mapigno kufuatia wizi wa ng’ombe watano ambao kati yao ng,ombe watatu walipatikana.
Nyumba zaidi ya 400 zimechomwa na watu zaidi ya 3,000 wamekosa mahali pa kukaa.
Serikali imekwishadhibiti ulinzi na usalama katika maeneo hayo kwa kuowangeza nguvu za polisi na imeanza kutoa msaada kwa walioathirika.
Waziri Mkuu alisema ni aibu mauaji kama hayo kutokea nchini kwa hivi sasa lakini inaonekana pia kuwa viongozi wa wa kiraia wa maeneo hayo wameshindwa kazi kwani ni wajibu wao kuyazuia tangu mapema.
Alisema Serikali inachukua hatua za hadhari hivi sasa za muda mfupi, lakini za muda mrefu zitategemea mkakati wa viongozi wa wilaya hizo za Tarime na Rorya na mkoa mzima wa Mara.
Waziri Mkuu pia alitembelea kwa helikopta na kutuaalipata kwenye maeneo yaliyotokea maafa hayo katika wilaya za Rorya na Tarime na kuzungumza na wananchi. Aliambatana na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali SaidMwema ambaye amekuwepo mkoani Mara kwa siku kadhaa akiwa na baadhi ya makamanda wake wakuu.
Katika eneo la Changuge, wilayani Rorya, wananchi waliopewa nafasi na Waziri Mkuu kutoa kero zao walimthibitishia kuwa mauaji hayo siyo ya kikabila na ya koo kati ya Wakurya wa Tarime na Wajaluo wa Rorya bali ni kati ya raia wema na majambazi wezi wa mifugo.
Waliiomba Serikali kuimarisha ulinzi kwa kuongeza askari polisi na zana.
Mbunge wa Rorya, Prof. Philemon Sarungi alimwambia Waziri Mkuu kuwa zaidi ya ng’ombe 2,000 wameibiwa mpaka sasa katika wizi huo.
Katika maeneo hayo yaliyokuwa na mauaji, Waziri Mkuu alifuatana pia na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali Said Mwema.
Akizungumzia Siku ya Serikali za Mitaa, Waziri Mkuu alisema kuendeleza kwa pamoja sekta za kilimo, mifugo na uvuvi, ndiyo njia pekee ya kuondoa umasikini nchini.
Waziri Mkuu alisema kuwa kuanzia sasa, uongozi bora wa Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya,Wenyeviti wa Halmashauti na Wakurugenzi, utapimwa kwa jinsi wanavyohimiza na kusimamia kwa vitendo kilimo, ufugaji na uvuvi.
Alisema viongozi waonyeshe uongozi wao kwa vitendo huko vijijini na siyo kukaa ofisini tu mijini.
(mwisho)
Imetolewa na:
Ofisi ya Waziri Mkuu
S.L.P. 3021
DAR ES SALAAM
Jumatano Julai 1, 2009

Huyu mwana wa mkulima anachekesha kweli kweli, keshanogewa na bia ya madaraka.
Mkuu wa wilaya ya rorya ni kanali Benedict Ketenga, mkuu wa mkoa wa Mara ni Kanali Enos Mfuru, kabla yake alikuwepo Kanali Issa Machibya.List ya wanajeshi kuongoza mkoa wa mara ni ndefu mno alipata kuwepo pia shushushu Nsa Kaisi miaka ya tisini. Kwahiyo PM kusema kwamba wataanzisha utawala wa kijeshi sijui anataka kufikisha ujumbe gani lakini ukweli ni kwamba jeshi sio suluhisho kabisa nawala suala hilo haliwezi kukubalika kabisa. Serikali nashindwa kulinda raia dhidi ya majmbazi na kusingizia vita vya kikabila. Ukweli ni kuwa hakuna vita ya kikabila kati ya wajaluo na wakurya. Tatizo lililopo ni wizi wa mifugo, wezi wa mifugo toka pande zote waluo na wakurya wanashirikiana na na wezi wenzao toka kenya na somalia. Serikali imeshindwa kuwadhibiti wezi.Hebu fikiria wezi wa mifugo wanatumia silaha kali kama AK47 halafu polisi na kirungu atathubutu lini kukabiliana nao?Ili kukomesha mapigano hayo serikali inatakiwa kuhamishia kikosi cha kupambana na wizi wa mifugo wilayani tarime, hakuna sababu ya kikosi hicho kukaa arusha ilihali matatizo ya wizi wa mifugo yanaendelea kupamba moto tarime. Wizi wa mifugo ukikomeshwa wala hatukakuwa na ugomvi wa wakurya vs waluo.Na kama serikali ikifanya kazi yake ipasavyo hakutakuwa na mapigano ya koo za wakurya. Viongozi wa serikali waliopo wilayani na mkoani hawana nia njema na watu wa tarime,vinginevyo hawana uwezo wa kuongoza na kwahiyo wanapaswa watimuliwe kazi mara moja. Hao hao ndio wanaokanusha kwamba hakuna mtu aliyekufa kutokana na athari za kemikali toka mgodi wa north mara wakati maisha ya wtu, mifugo na mimea vinaangamia.
Mbona serengeti, Bunda na musoma kuna wakurya lakini hakuna huo ugomvi?kwahiyo mtu asikurupuke tu kusema napeleja jeshi tarime, anatakiwa aujue ukweli wa mambo.Tatizo hawa viongozi wetu wanawaamini mno wateule wao, wateule wao nao hawatimizi wajibu wao basi inakuwa tabu tupu.Sisi wakazi wa mkoa wa mara na hususani tarime tunafahamu kwanini serikali haichukui hatua madhubuti, siku ikiamua,mapigano hayo yatakuwa historia kwakuwa chanzo chake kinajulikana lakini kwakuwa hawana nia wacha tu watuletee majeshi kama walivyofanya kule anjuan comoro.
 
Yani I wish wangempindua jimboni kwake mwakani just to send a message. Just imagine what impact it will have for the prime minister to loose in the elections. Sema ikitokea hali kama hiyo watamfanyia tu mipango apate ubunge kama kweli JK will still want him.
 
Hajaeleza chochote cha maana zaidi ya kuchemka. Kwanza kutawala kijeshi maana yake nini? Tafsri ninayopata hapa ni kuwa ni kutumia maguvu bila kujali sheria za nchi. Kama sivyo wanajeshi watafuata sheria kinachowashinda wakuu wa wilaya na mkuu wa mkoa kutumia hizo sheria ni ni? Hata hivyo gavana wa Mara si ni mjeshi mbona watu bado wanachinjana?
Kuhusu watu kuchinjana hilo halihalalishi kauli za kukurupuka kama hizi. Akichinjwa mmoja, wawili, kumi au mia ni kuchinja tu. Albino wamechinjwa sana. Huko Kilosa ni zaidi hata ya Tarime mbona hatujawahi kumsikia akisema haya?

Tatizo kubwa kwa comments kama hizi ni za mtu kuifahamu Tanzania kupitia magazeti na Tv.
Wengi wenu hata Morogoro hamjafika , ukiacha njia kuu ndio kabisa ni sawa na kwenda mwezini.
Sehemu hizo mimi nimefika na mimeona kwa macho yangu polisi wakila milo katika haya mapigano ya kiukoo.
Ningekushauri Capt Hadock kama unabiashara hebu ipeleke huko Rorya au Tarime , pengine utaelewa kinachozungumziwa.
 
Hali kama hii ilipata kuwepo miaka ya mwanzo ya 70. Kilichofanyika wakati huo ni kuwatambua wezi SUGU wa mifugo na wafadhili wao wakuu wakasombwa, wakaenda kuhifadhiwa kusiko julikana, baadaye baadhi yao walibahatika kurudi wakiwa watu wema sana. Wengi hatunao kwa sasa lakini amani ilidumu hadi miaka ya hivi karibuni ambapo kuna OMBWE la UTAWALA na UONGOZI katika NCHI yetu kwa kisingizio cha utawala bora na haki za binadamu huku watu wakiendelea kuuwawa na mali zao zikiibiwa na makazi yao kuteketezwa.
Ifahamike tu kwamba wezi na majambazi katika jamii sio wengi hivyo kiasi cha kushindwa kudhibitiwa.
 
Mimi nimewahi kushuudia LIVE hayo mapambano.

Kabla ya kwenda kupigana kuna imani za kishrikina zinaingizwa. Watu wanajiandaa kwenda vitani kama kwenye movie za Mel Gibson za kivita za zamani. Tofauti kubwa ni kuwa wanapigana bila mpango wala mbinu maalum.

Hivi vita vimekuwa haviripotiwi tu lakini vipo tokea zamani na zinajulikana wazi kabisa.

Utawala huu umevipa uhuru zaidi vyombo vya habari ndio maana mnavisikia.

Zamani ilikuwa inasemwa ya waanchali na walinchoka (nimekosea spelling) tu lakini VITA VYA WAKURYA NA WAJALUO NI VYA KIJADI. Vilikuwepo na vinaendela.

Sababu kubwa ni Kuibiwa ng'ombe. Sitaki kuwa biased lakini si vita vya kuIBIANA bali kuibiwa. Nikiwa na maana ya kabila mmoja kuiba ng'ombe mara kwa mara za kabila nyingine.

Na hii ilianza zaidi baada ya Vita vya Kagera ambapo watu walirudi na silaha.

Jamani pamoja na yote, ALYATONGA MREMA sijui alikuwa na mbinu gani, lakini alisuluhisha migogoro na kumaliza hivi vita. Huyu jamaa ni simply waziri wa mambo ya ndani kwa kuzaliwa.
Sio huyu brother man wa sasa.

Yangu machache hayo

FP
 
Back
Top Bottom