Pinda amshukia Zitto

MwanaFalsafa1

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
5,565
836
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amemshambulia Mbunge wa Kigoma Kaskazi Zitto Kabwe na kumtaka aache kuwapotosha wananchi kuwa, jitihada zake ndiyo zilizosababisha ujenzi wa barabara ya Kigoma.

Akitoa majumuisho ya bajeti ya Wizara yake kwa mwaka 2009/10 bungeni jana Pinda alisema, ujenzi wa barabara hiyo ulikuwa kwenye ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Alisema, CCM imefanya mambo mengi mazuri ingawa wapinzani hawataki kukubaliana na ukweli huo.

"Mheshimiwa Spika rafiki yangu Zitto Kabwe alijaribu kujigamba kuwa amefanya mambo huko Kigoma mapaka wamepata barabara, lakini nilikwenda huko jimboni kwake na kuzunguka kote na kuwaahidi wananchi ujenzi wa barabara hiyo"alisema Pinda na kuongeza:

"Mheshimiwa Spika ujenzi wa barabara ya Kigoma ni mpango wa muda mrefu wa CCM na ulikuwa katika ilani yake ya uchaguzi." Pinda alisema, serikali ni ya chama tawala na fedha za barabara hiyo zimetolewa na serikali hiyohiyo.

"Mheshmiwa Spika labda niseme hivi serikali ni ya chama chetu, fedha ni za serikali ya CCM na barabara zinajengwa na CCM, labda mheshmiwa Zitto pamoja na Chadema yake wangeniambia tu, Waziri serikali yako imejitahidi sana"aliongeza Waziri Mkuu.

Pinda alisema, alitegemea Zitto angekiri kuwa serikali ya CCM imempa barabara bila ya kuonesha ubaguzi wa kiitikadi za kisiasa pamoja na kwamba Zitto ni wa chama kingine siasa.

Wakati huohuo Waziri Pinda aliahidi kuendelea kutumia upole katika kazi zake ili kuongeza tija katika ufanisi wa serikali.

"Mheshimiwa Spika wabunge wamenitaka kupunguza upole, lakini upole na ukali una karama zake nao, hivyo mimi nitaendelea kuwa mpole katika kazi zangu ili kuhakikisha kuwa ufanisi wa serikali unaongezeka na kuwa na tija kwa wananchi," alisema.

Habari hii imeandaliwa na Jackson Odoyo na Salim Said Mwisho.

Source: Mwananchi Read News
 
this is embrassing kwa PM kuingia kwenye siasa za punch and Judy

kwani kuna ubaya gani angeyamaza?

this is so low, yeye angesema wanatekeleza ilani ya chama ya 2005 kungekuwa na ubaya gani?


Hivi Zitto akiamua kujibizana naye atamweza?
 
this is embrassing kwa PM kuingia kwenye siasa za punch and Judy

kwani kuna ubaya gani angeyamaza?

this is so low, yeye angesema wanatekeleza ilani ya chama ya 2005 kungekuwa na ubaya gani?


Hivi Zitto akiamua kujibizana naye atamweza?

I agree with you on this one.
 
Pinda alisema said:
Kama Pinda ni mkweli kwa hili mbona wakati wa kampeini CCM wanawambia wananachi wakiwachagua wapinzani hawatapata maendeleao maana bila CCM mambo hayaendi. Anataka kusema jimbo la Zitto kabwe limepata barabara kwa upendeleo maalum?
 
Yani hapa Pinda kaonyesha immaturity ya hali ya juu. Inamaana sasa majimbo yenye wabunge wapinzani yata patiwa maendeleo ikipenda CCM? Zitto si mbunge wa jimbo hilo kwa hiyo kama barabara ikiletwa si na yeye itakua kaomba jimbo lake iletewe barabara? Au yeye alitegemea majimbo ya upinzani maendeleo yaletewa na pesa toka mifukoni mwa wabunge wa upinzani au vyama vya upinzani? Huyu nae siku hizi ana poteza muelekeo.
 
Hapana Shaka kuwa Kodi zetu ndio wanatumia Kujenga Barabara na Sio CCM, CHADEMA, CUF, CCM, TLP, UDP na wasio na Vyama, Maskini, Matajiri na watu wote na CCM, Pinda hakuwa sahihi by way hizo ndio Politics tu
 
PM hapa kaboa lakini hata hili nalo alitaka ashauriwe?

... Ni kule kujisahau na kutoa matamshi kama Waziri Mkuu wa CCM badala ya Waziri Mkuu wa Taifa la Tanzania.

... Inaboa kwa kweli.

... Zitto naye amwambie kuwa, HAPANA; waliojenga ni Makandarasi wakishirikiana na TanRoads!!!
 
Hapana Shaka kuwa Kodi zetu ndio wanatumia Kujenga Barabara na Sio CCM, CHADEMA, CUF, CCM, TLP, UDP na wasio na Vyama, Maskini, Matajiri na watu wote na CCM, Pinda hakuwa sahihi by way hizo ndio Politics tu

Exactly mkuu. Aache kusema kuwa ni CCM imeijenga kwa sababu ni hela za walipa kodi za Watanzania including wananchi wa jimbo la Zitto Kabwe. Aache kusema ni jitihada za serikali za CCM as if they did them some kind of favor wakati ni wajibu wa serikali kuendeleza miundombinu. It seems now CCM wanajiona kwamba wao wanajitolea msaada kuiendeleza Tanzania badala ya wajibu.
 
Exactly mkuu. Aache kusema kuwa ni CCM imeijenga kwa sababu ni hela za walipa kodi za Watanzania including wananchi wa jimbo la Zitto Kabwe. Aache kusema ni jitihada za serikali za CCM as if they did them some kind of favor wakati ni wajibu wa serikali kuendeleza miundombinu. It seems now CCM wanajiona kwamba wao wanajitolea msaada kuiendeleza Tanzania badala ya wajibu.
Wakati mwingine huwa naona kuwa Wanasiasa wa CCM kama vile wamelewa Madaraka ya uongozi na kuona kila kitu ni Chao na Kubana mambo mengine ya Upinzani, Watu wanalipa Kodi ya VAT, Wanalipa Kodi ya wafanyakazi, Hivyo Pinda aliwahi kusema kuwa wakati mwingine inakuwa vigumu sana kwa ajili ya kutenganisha Kofia Mbili za CHAMA na Serikali, Siyo Pesa na Ilani ya CCM, But ni Kodi za Watanzania. Hivyo watu wanaweza kuwaza na kujiuliza kauli kama PM Pinda, Siyo Vizuri na Ndio maana hakuna Resources kwa ajili ya upinzani na kuona ni CCM, Pia wanaona au kujenga kama Kisiasa kwa ajili ya uchaguzi Mwakani tu hakuna Jipya. Watzannia ndio wanatumia Kodi zetu
 
Ni haki yao kujenga Barabara na pia wasipojenga tutawauliza kwanini??Ni Lazima wafanye hivyo Zitto kazi yake kubwa kukumbusha na kuwasemia tu. CCM waache Majigambo yao, Basi wakubali pia madudu mengine ya ajabu katika Taifa letu pia
 
this is embrassing kwa PM kuingia kwenye siasa za punch and Judy

kwani kuna ubaya gani angeyamaza?

this is so low, yeye angesema wanatekeleza ilani ya chama ya 2005 kungekuwa na ubaya gani?


Hivi Zitto akiamua kujibizana naye atamweza?

Sure Sir, I don know when we will put clear cut between leadership and politics! in my opinion Im forced to believe these are separately two things. kuna haja gani ya waziri mkuu hata na mawaziri wengine kupiga kampeni Bungeni badala ya kuonesha what they ve done? mama Shelukindo made a great point in her contribution, alisema the problem is kila mtu serikali anaongea hakuna mtekelezaji. Hata waziri mkuu ambaye Spika alidiriki kumwita mteule Wa Mungu nae ana-fall within the category
 
Ukiona hivyo pengine wanaogopa kivuli cha Zitto. Haiwezekani akawa part of speech ya Mheshimiwa Pinda for no reason.Nakubaliana na wengi kuwa si kila ushindi unapatikana kwa kupigana vijembe au kupanga debate ndefu ndefu.Mara nyingine kukaa kimya ni dawa pia.
 
Inabidi nianze kuamini kuwa samaki mmoja akioza tupa wooooote.Sikutegemea kama Mizendo Kayanda Peter Pinda kuongea utumbo kiasi hicho.Tumsamehee na tumrekebishe
 
Hizo siasa. Usipojua utaumia. Waswahili wa pemba wale. Tunatambua mchango wa upinzani nchini. Jaribu kusikiliza kampeni utaona ya pinda madogo
 
Ukiona hivyo pengine wanaogopa kivuli cha Zitto. Haiwezekani akawa part of speech ya Mheshimiwa Pinda for no reason.Nakubaliana na wengi kuwa si kila ushindi unapatikana kwa kupigana vijembe au kupanga debate ndefu ndefu.Mara nyingine kukaa kimya ni dawa pia.
Wanaogopa Kivuli chake na ndio maana wanapiga kampeni kabla ya wakati wake. Hivyo Hii ni kufanya ya siasa, Ni lazima tuone kwanza, Kwanini naye aje na majibu kama haya kwa kumsema Zitto Kabwe
 
"Mheshmiwa Spika labda niseme hivi serikali ni ya chama chetu, fedha ni za serikali ya CCM na barabara zinajengwa na CCM, labda mheshmiwa Zitto pamoja na Chadema yake wangeniambia tu, Waziri serikali yako imejitahidi sana"aliongeza Waziri Mkuu.

Kweli viongozi wetu ni vilaza kweli na hii inatia maudhi kabisa kusikia maneno kama haya yanatoka kwa kiongozi mkuu na mwenye dhamana kubwa! Wanaoshindwa kutofautisha mambo ya chama na serikali. Je ni CCM imejenga barabara? Je ni kweli fedha ni zilizotumika ni za CCM? Je ina maana kuwa makusanyo ya kodi ni ya CCM? Hii ina maanisha kuwa kodi yetu wanaweza kuifisadisha watakavyo!
 
WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda amemshambulia Mbunge wa Kigoma Kaskazi Zitto Kabwe na kumtaka aache kuwapotosha wananchi kuwa, jitihada zake ndiyo zilizosababisha ujenzi wa barabara ya Kigoma.

Akitoa majumuisho ya bajeti ya Wizara yake kwa mwaka 2009/10 bungeni jana Pinda alisema, ujenzi wa barabara hiyo ulikuwa kwenye ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Alisema, CCM imefanya mambo mengi mazuri ingawa wapinzani hawataki kukubaliana na ukweli huo.

"Mheshimiwa Spika rafiki yangu Zitto Kabwe alijaribu kujigamba kuwa amefanya mambo huko Kigoma mapaka wamepata barabara, lakini nilikwenda huko jimboni kwake na kuzunguka kote na kuwaahidi wananchi ujenzi wa barabara hiyo"alisema Pinda na kuongeza:

"Mheshimiwa Spika ujenzi wa barabara ya Kigoma ni mpango wa muda mrefu wa CCM na ulikuwa katika ilani yake ya uchaguzi." Pinda alisema, serikali ni ya chama tawala na fedha za barabara hiyo zimetolewa na serikali hiyohiyo.

"Mheshmiwa Spika labda niseme hivi serikali ni ya chama chetu, fedha ni za serikali ya CCM na barabara zinajengwa na CCM, labda mheshmiwa Zitto pamoja na Chadema yake wangeniambia tu, Waziri serikali yako imejitahidi sana"aliongeza Waziri Mkuu.

Pinda alisema, alitegemea Zitto angekiri kuwa serikali ya CCM imempa barabara bila ya kuonesha ubaguzi wa kiitikadi za kisiasa pamoja na kwamba Zitto ni wa chama kingine siasa.

Wakati huohuo Waziri Pinda aliahidi kuendelea kutumia upole katika kazi zake ili kuongeza tija katika ufanisi wa serikali.

"Mheshimiwa Spika wabunge wamenitaka kupunguza upole, lakini upole na ukali una karama zake nao, hivyo mimi nitaendelea kuwa mpole katika kazi zangu ili kuhakikisha kuwa ufanisi wa serikali unaongezeka na kuwa na tija kwa wananchi," alisema.

Habari hii imeandaliwa na Jackson Odoyo na Salim Said Mwisho.

Source: Mwananchi Read News

Pinda kapinda ukweli wa wajibu wa serikali kwa wananchi. Wabunge wanawajibika kusimamia serikali iwajibike kwa wananchi.
Wabunge wakipigia kelele kuitaka serikali iwajibike kuendeleza maeneo yaliyosahaulika, mf. kujenga barabara, halafu serikali ikaitikia kelele hizo, na hivyo kujenga barabara ua kuchimba visima vya manji, basi huo unakuwa ushindi kwa wabunge husika. Na huu ndio ushindi wa Zitto Zuberi Kabwe kuhusiana na ujenzi wa barabara za Kigoma.

Ni dhahiri kuwa wabunge wa Kigoma (hususan wa sasa wa CCM, na wabunge wengine wa zamani katika majimbo ya mkoa wa Kigoma) hawakutimiza wajibu wao ipasavyo kuiwajibisha serikali na hivyo serikali kutowajibibika kujenga barabara hizo! Sasa Pinda anataka kupinda ukweli huu na bahati mbaya anataka watanzania tuamini; hafai kuwa waziri mkuu wala kiongozi ngazi ya uwaziri!

Si CCM wala chama kingine cha siasa chenye kumiliki rasilimali za nchi. Serikali imepewa dhamana kutumia rasilimali za nchi kupanga na kutekeleza mipango ya maendeleo. Pinda ni mwongo katika hili, hususan anaposema kuwa rasilimali za kujengea barabara ni mali ya CCM na serikali yake. Ni kweli siyo mali ya Chadema, lakini pia siyo ya CCM wala serikali. Pinda kapinda ukweli!
Akome kudharau uwezo wa watanzania kutambua masuala ya mifumo ya utawala!

Mbaya zaidi kamtetea hata Mkapa kuwa siyo fisadi wakati kila mtanzania anajua kuwa Mkapa ameliibia taifa hili na kujilimbikizia mali! ANBEN, BanK M, Lada scam rent na nyinginezo! Pinda usizuge watanzania!
 
Last edited:
Sijui kwanini alisema hivi?? Maana nakumbuka siku ile huyu Zitto alipomuliza kwanini wanatumia Pesa za Walipa Kodi kwa ajili ya Kampeni za CCM alikubali na Kumsamehe kabisa, Hapa Mtoto wa Mkulima ameshemsha labda aje huku asome watu wanasema nini, Maana hawezi kusema hivyo. Jamani ndugu zangu ndio maana mkoa wa Kigoma Upo Nyuma kwasababu ya Kuchagua Upinzani?? Kwanini anasema hivi, Tazama Maneno yote katika Majibu yake ni ya kisiasa tu na yamejaa kujibu kauli ya Zitto Kabwe!!
 
Back
Top Bottom